MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wanufaika wa SDF Waeleza Mafaniko Waliyoyapata
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wanufaika wa SDF Waeleza Mafaniko Waliyoyapata
Habari

Wanufaika wa SDF Waeleza Mafaniko Waliyoyapata

Author
By Author
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: “BAADA ya kupata mafunzo kwa miaka mitatu nimeweza kukua kibiashara kwa sababu mwanzoni niliweza kuuza bidhaa zangu za viungo vya chakula mkoa mmoja. Lakini sasa nauza nchi nzima hata nje ya nchi,”.

Mnufaika wa Mfuko wa Kuendeleza Ujuzi ( SDF), ulioko chini ya Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Geshoni Muni ameeleza hayo katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara yajulikanayo kama Sabasaba mkoani Dar es Salaam alipozungumza na Mfanyakazi Tanzania katika Banda la TEA.

Amesema mwanzoni alipoanza usindikaji wa viungo aliuza katika mkoa wa Iringa pekee, lakini sasa anauza mikoa yote bidhaa zake za tangawizi, mdalasini, viungo vya pilau, viungo vya chai na vinginevyo.

“Pia nimebahatika kuuza tangawizi kavu nchi ya Afrika Kusini tani 20 pamoja Zambia.

“Kuwa na TEA kumenisaidia kutambulika na kupata masoko kwa ukubwa kiasi hicho,” amesema.

Ameshukuru kwa kuwa biashara hiyo imemwezesha kuendesha maisha yake, hategemei kuajiriwa wala hawazi kufanya hivyo kwa kuwa anaiamini biashara anayoifanya.

Amekiri maisha yake yameboreshwa kutokana na biashara hiyo.

Naye Mkulima wa Uyoga, Esther Shebe amesema kwamba, naye ni mnufaika wa mfuko huo wa kuendeleza ujuzi.

“Kwa miaka mitatu nimenufaika. Ninashukuru TEA kwa kuniwezesha kunitangaza kwenye maonesho mbalimbali yakiwemo haya ya sabasaba kwa mwaka huu 2025.

“TEA imenipa nafasi ya kuonesha bidhaa zangu na watu wananunua. Lakini nimenufaika kwa kupata ujuzi mpaka nina bidhaa karibia 10 ninazozitengeneza. Lakini hii yote ni kutokana na mfuko wa kuendeleza ujuzi nilipoenda kujifunza SIDO,” amesema.

Amesema kwa sasa anatengeneza losheni ya uyoga, shower jelly pamoja na sabuni ya uyoga na mafuta ya mgando ya uyoga, wine ya uyoga, biskuti, keki na uyoga wenyewe.

Pia ametengeneza mkaa mbadala kwa kutumia mabaki ya uyoga ambao hauna moshi na ni mzuri kwa matumizi.

You Might Also Like

Mwongozo wa Mafunzo Elekezi Kwa Walimu Wapya Kazini Mbioni Kukamilika

BUWSSA Yapewa Bilioni 28 Kutatua Tatizo La Maji

REA Yapamba Moto Uhamasishaji Matumizi Ya Umeme

Tanzania, Ufini Kushirikiana Teknolojia Za Kisasa Sekta ya Misitu

Wiki ya kudhibiti bidhaa bandia kuhitimishwa DSM

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article VETA Dodoma Waleta Mashine Kurahisishia Upekechuaji Wa Alzeti
Next Article TEA Yawaalika Wananchi Kujifunza SDF Unavyofanya Kazi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

TEA Yawaalika Wananchi Kujifunza SDF Unavyofanya Kazi
Habari July 3, 2025
VETA Dodoma Waleta Mashine Kurahisishia Upekechuaji Wa Alzeti
Habari July 3, 2025
VETA Shinyanga Waja Na Mafunzo Ya Saluni, Mapambo, Urembo
Habari July 3, 2025
UDSM Yaja Na Bajaji Inayotumia Maji Na Mafuta
Habari July 3, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?