MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Lukuvi Asema 2024 Bangi Ilivunja Rekodi, Tani Zaidi Ya 2000 Zilikamatwa
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Lukuvi Asema 2024 Bangi Ilivunja Rekodi, Tani Zaidi Ya 2000 Zilikamatwa
Habari

Lukuvi Asema 2024 Bangi Ilivunja Rekodi, Tani Zaidi Ya 2000 Zilikamatwa

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Danson Kaijage
DODOMA: KWA mwaka jana 2024 tani 2,307.37 za bangi zilikamatwa, kati ya hizo tani 2,303.2 zilitoka ndani ya nchi, na 4.17 zilikuwa skansa zilitoka Kusini mwa Afrika.
Hicho kikiwa ni kiasi kikubwa zaidi kilichokamatwa.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge na Uratibu William Lukuvi amesema hayo, mara baada kuwasilisha Bungeni Taarifa ya Hali ya Dawa za Kulevya kwa mwaka 2024.
Lukuvi amesema, Skanka, ambayo ni bangi yenye kiwango kikubwa cha kemikali ya THC, iliongezeka kwa asilimia 89.8 ikilinganishwa na mwaka juzi 2023, jambo linaloonesha kuimarika kwa udhibiti wa biashara haramu ya dawa hizo kupitia mipaka, viwanja vya ndege na bandari.
Amesema serikali ilikamata tani 1.7 za methamphetamine, kilo 433.02 za heroin, gramu 853 za cocaine, na kwa mara ya kwanza kilo tano za dawa mpya aina ya Methylene-dioxy-pyrovalerone (MDPV).
Zaidi ya hayo ameeleza kuwa tani 18.45 za mirungi, kilo 56.78 za dawa tiba zenye asili ya kulevya na tani 29.6 za kemikali bashirifu zilinaswa kwa usaidizi wa mifumo ya udhibiti wa kielektroniki.
Kwa upande mwingine amesema, Serikali imeendelea kutoa tiba kwa waraibu kupitia vituo 16 vya methadone vilivyohudumia waraibu 17,975,
Pia nyumba 62 za upataji nafuu pia zimeendelea kutoa huduma kwa waraibu 17,230 waliotambuliwa katika mikoa mbalimbali nchini.
Amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha mamlaka hiyo kwa vitendo pamoja na wataalamu wa afya, mashirika ya kiraia, vyombo vya usalama, pamoja na wananchi kwa mshikamano wa pamoja uliosaidia kufanikisha mafanikio hayo.
Amesema, suala la dawa za kulevya si tatizo la sekta moja, linahusisha afya, usalama, elimu, ajira, na ustawi wa jamii,mafanikio ya kweli yanahitaji juhudi jumuishi kutoka serikalini, kwa wananchi, sekta binafsi na wadau wa kimataifa.
Kwa upande wake Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, Aretas Lyimo, ameonya vikali tabia inayoendelea kushika kasi miongoni mwa wasanii wanaotumia kazi zao kuhamasisha matumizi ya dawa za kulevya.
Amesema, “Tunaendelea kufuatilia kwa karibu nyimbo, video na mavazi yanayochochea utumiaji wa dawa za kulevya, Serikali haitasita kuchukua hatua kali kwa wote wanaopotosha jamii, hasa vijana,”.
Amesena baadhi ya kazi za sanaa zimejaa maudhui ya kashfa, mavazi ya aibu na simulizi za kupambanua matumizi ya bangi na dawa nyingine hatarishi, hali inayochangia kuathiri maadili ya taifa na mapambano ya dawa hizo kwa ujumla.
“Sanaa si jukwaa la kutukuza mihadarati. Vijana wetu wanahitaji maudhui ya kuwajenga, si kuwaangamiza. Tutawachukulia hatua wote wanaokiuka sheria na taratibu za nchi,” amesena.
Amesema Serikali  itaendelea kuimarisha mbinu za kiintelijensia, sheria na tiba katika kukabiliana na janga hili la kimataifa, ikiwa ni pamoja na kuhimiza jamii kutoa taarifa kwa vyombo husika pindi wanapobaini au kushuku shughuli zinazohusiana na dawa za kulevya.

You Might Also Like

Shule 216 Za Serikali Zatumia Nishati Safi Ya Kupikia – Kapinga

Rais Samia azindua skuli ya maandalizi Tasani

Bahari  Ina Fursa Nyingi Zisizofahamika-Tasac

Tanzania Yaongoza Kwa Ushiriki, Makongamano Ya Ushirika Ndani, Nje Ya Nchi

Tumeleta Utulivu na Huduma kwa Walimu’ – Ikomba

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TPHPA Yapata Dawa Ya Visumbufu Vya Mazao
Next Article Taasisi Za Serikali Zapewa Wiki Tano Kujiunga Na Mfumo
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Majaliwa Apongeza Jeshi La Magereza Kurasimisha Ujuzi Kwa Wafungwa
Habari August 27, 2025
Mapokezi Ya Katibu Mkuu CCM  Dkt Migiro CCM, Aahidi Ushirikiano
Habari August 27, 2025
Majaliwa Aagiza Kuimarishwa kwa Mafunzo ya Ufundi Stadi Nchini
Habari August 27, 2025
VETA Yaanzisha Kozi Mpya ya Teknolojia ya Mifumo ya Viwandani
Habari August 26, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?