MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Serikali Imetoa Ruzuku Ya Asilimia 20 Hadi 50 Kwenye Mitungi YA Gesi – Kapinga
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Serikali Imetoa Ruzuku Ya Asilimia 20 Hadi 50 Kwenye Mitungi YA Gesi – Kapinga
Habari

Serikali Imetoa Ruzuku Ya Asilimia 20 Hadi 50 Kwenye Mitungi YA Gesi – Kapinga

Author
By Author
Share
4 Min Read
Na Danson Kaijage
DODOMA: NAIBU Waziri wa Nishati,  Judith Kapinga amesema serikali imetoa ruzuku ya asilimia 20 hadi 50 kwenye mitungi ya gesi ya LPG  452,445 kwa watumiaji wa mwisho ikiwa ni jjtihada za kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.
Kapinga ameyasema hayo jijini Dodoma wakati akijibu swali la  Mbunge wa Viti Maalum, Grace Tendega aliyetaka kufahamu Serikali ina mkakati gani wa muda mfupi wa kuhakikisha Wananchi wa Vijijini wanatumia Nishati Safi ya kupikia badala ya Kuni na Mkaa.
“Mheshimiwa Mwenyekiti Serikali kupitia REA pia  itasambaza majiko banifu 200,000 yenye bei ya punguzo la hadi asilimia 75 pamoja na kuwezesha ufungaji wa mifumo ya nishati safi ya kupikia katika Taasisi za Umma zinazohudumia watu zaidi ya 100,” amesema.
Vile vile amesema Serikali imekamilisha kazi ya usambazaji umeme katika vijiji vyote hivyo kwa sasa inaendelea kuhimiza matumizi ya majiko ya kupikia yanayotumia umeme ikiwa ni njia mojawapo ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa wananchi wa vijijini badala ya kutumia kuni na mkaa.
Amesema Mkakati wa Taifa wa  Nishati Safi ya Kupikia ni wa miaka 10 lakini serikali inao mkakati wa matumizi bora ya nishati ambao unahusisha pia sekta binafsi kwa ajili ya kusaidia kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.
Akijibu swali la Mbunge wa Mbulu,  Zacharia Isaay aliyeuliza Serikali imejipangaje kuhakikisha Vitongoji vyote vilivyokusudiwa katika mwaka huu wa bajeti kufikiwa  na umeme katika kipindi cha mwezi mmoja uliobaki, Kapinga amesema Serikali inayo mikakati na miradi mbalimbali ya kupeleka umeme katika Vitongoji.
Amesema kuwa, moja ya mikakati hiyo ni kupeleka umeme katika Vitongoji 15 kwa kila Jimbo, na pia  Serikali ina mkakati wa kupeleka umeme katika Vitongoji 20,000 ambapo   awamu ya kwanza inaanza kupeleka umeme katika Vitongoji 9000 na hatua iliyopo ni utafutajj wa wakandarasi.
Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Anatropia Theonest aliyeuliza bei ya Serikali ya ruzuku imeanza kutumika lini kutokana na mitungi ya gesi kuendelea kuuzwa kati ya Sh. 22,000 na 25,000 na kwa mitungi mikubwa ya kilo 15 Sh.  50,000 na 60,000.
Amesema maeneo ya mjini Serikali imepeleka ruzuku hadi asilimia 25 na maeneo ya Vijijini ni kati ya asilimia 50 hadi 75 na kutolea mfano iwapo mtungi ulikuwa unauzwa Sh. 45,000 kwa bei ya ruzuku inapatikana kwa Sh. 17,000 hadi 21,000 na kusema ni zaidi ya nusu ya bei yake.
Amesema katika kila Wilaya kuna takribani mitungi 3,255 inayopatikana kwa ruzuku na kuongeza kuwa ndio kwanza mkakati umeanza.
Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Yustina Rahhi aliyeuliza mpango wa Serikali kuwapelekea jamii ya wafugaji teknolojia ya biogas au kuwajengea majiko yanayotumia samadi ya gesi ambayo ni rahisi, Kapinga amesema Serikali inatekeleza mradi huo kupitia umoja wa Ulaya (mfuko wa UNCDF) ambao una teknolojia alizozitaja  Mbunge.
Akijibu swali la Mbunge wa Nyang’wale, Hussein Amar aliyeuliza kuhusu mpango wa Serikali kuzipelekea nishati safi ya kupikia  Shule za Sekondari 19 na Sekondari 12 za bweni zilizo Wilaya ya Nyang’wale ili kulinda mazingira, Kapinga amesema Wizara ya Nishati inaompango wa kuzipelekea nishati safi ya kupikia Taasisi za umma kwa kushirikiana na TAMISEMI.
Katika hatua nyingine Kapinga amezishauri Halmashauri  kufunga mifumo ya nishati safi ya kupikia  katika Taasisi zilizopo katika Halmashauri wanazoziongoza kwa kutumia mapato ya ndani.

You Might Also Like

Erio atoa elimu ya bidhaa bandia kwenye mabanda nanenane

Wasilisheni Migogoro Yenu Tume ya Usuluhishi na Uamuzi – Massawe

Rais Samia Awatega Wateule Wake

Mpango Mkakati wa Takwimu wazinduliwa

CCM yavunja rekodi – Makala

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Program Ya Maeneo Yaliyochakaa Nchini Yaandaliwa
Next Article Michezo Yapunguza Uhalifu Dodoma
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Michezo Yapunguza Uhalifu Dodoma
Habari May 25, 2025
Program Ya Maeneo Yaliyochakaa Nchini Yaandaliwa
Habari May 25, 2025
CCM Kuwezesha Wananchi Kufuatilia Mkutano Mkuu Maeneo Ya Wazi
Habari May 25, 2025
Soko La Kisasa La Nyamachoma Lazinduliwa Vingunguti
Habari May 25, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?