MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TEA Kukarabati Jengo La Bodi Ya Maktaba Kwa Milioni 300
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TEA Kukarabati Jengo La Bodi Ya Maktaba Kwa Milioni 300
Habari

TEA Kukarabati Jengo La Bodi Ya Maktaba Kwa Milioni 300

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
MAMLAKA ya Elimu Tanzania (TEA) imetenga Sh. Milioni 300 kwa ajili ya ukarabati wa jengo la Bodi ya Maktaba lililopo Kisiwani Pemba.
Ukarabati unaolenga kuimarisha miundombinu ya taasisi hiyo muhimu inayotoa huduma kwa wanafunzi na wananchi kwa ujumla.
Kaimu Mkurugenzi wa Utafutaji Rasilimali na Usimamizi wa Miradi kutoka TEA, Masozi Nyirenda amesema hayo wakati wa ziara ya ukaguzi Kisiwani Pemba.
Nyirenda amesem fedha hizo tayari zimetolewa, na ukarabati utaanza mara tu baada ya mkandarasi kusaini mkataba rasmi na kuwasilisha mpango kazi utakaoonesha hatua kwa hatua namna kazi hiyo itakavyotekelezwa hadi kukamilika kwa wakati.
Naye Mratibu wa Bodi ya Maktaba Pemba, Ahmed Hamis amesema jengo linalotarajiwa kukarabatiwa ni miongoni mwa majengo ya kihistoria yaliyojengwa kipindi cha ukoloni.
“Hata hivyo, tangu lijengwe, jengo hilo halijawahi kukarabatiwa, jambo lililosababisha uchakavu mkubwa wa jengo zima na miundombinu ya ndani, na hivyo kuathiri utoaji wa huduma kwa wananchi,” amesema.
Amesema kukamilika kwa ukarabati huo kutakuwa ni faraja kwa wakazi wa Wilaya jirani ambao hutegemea huduma za maktaba hiyo kwa ajili ya kusoma vitabu, hasa watoto wanaohitaji nyenzo za kielimu kama vile hadithi na historia za watu mashuhuri.
Mradi huo wa ukarabati unatekelezwa kama sehemu ya majukumu ya TEA kama taasisi ya Muungano, ambayo kimsingi inahusika na utafutaji wa rasilimali kutoka kwa wadau mbalimbali ili kusaidia jitihada za Serikali katika kuboresha miundombinu ya elimu.
Kupitia miradi kama hiyo, TEA inalenga kuhakikisha kuwa kila mwanafunzi anapata mazingira bora ya kujifunzia bila kujali eneo analotoka.

You Might Also Like

Tanzania, Japan Kushirikiana Ukuzaji Ujuzi Kwa Vijana

TARI Yanufaisha Wadau Wa Kilimo, Ugunduzi Wa Mbegu Bora Na Za Kisas

Kongamano La Kwanza La Kodi Kufanyika Dar es Salaam

Ufugaji wa sungura ni fursa  – UDOM

Rais Samia Kuzindua Mfuko wa Mikopo Wenye Kianzio Cha Sh. Bilioni 2.3

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Matukio Mbalimbali Katika Picha Baada Ya Waziri Mkuu Kuwasilisha Makadirio Ya Mapato Ya Bajeti
Next Article Chalamila Asema Serikali Inafanyia Kazi Changamoto, Mradi Wa Mabasi Yaendayo Haraka
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Singida Yapokea Zaidi Ya Milioni  Moja 
Habari July 5, 2025
THBUB Mdau Mkubwa Utekelezaji Wa Majukumu 
Habari July 5, 2025
NBS: Utumiaji Wa Takwimu Nyenzo Muhimu Kwa Mama Lishe
Habari July 5, 2025
FCC Yatoa Elimu Ya Ushindani Wa Kibiashara Katika Maonesho Ya  Biashara
Habari July 5, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?