MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Rais Samia Aridhia Malipo Ya Fidia Barabara Ya Afrika Mashariki
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Rais Samia Aridhia Malipo Ya Fidia Barabara Ya Afrika Mashariki
Habari

Rais Samia Aridhia Malipo Ya Fidia Barabara Ya Afrika Mashariki

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
PWANI: RAIS Samia Suluhu Hassan ameridhia  malipo ya Sh. Milioni 800 kwa wananchi 429 wa Kata ya Mkange wanaopisha ujenzi wa Barabara ya Afrika Mashariki inayojengwa toka Tanga kupita Kata hiyo hadi Makurunge Bagamoyo.
Mbunge wa Jimbo la Chalinze ambaye pia ni Waziri Wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana,Ajira na wenye Ulemavu, Ridhiwani Kikwete amesema hayo wakati wa mkutano aliofanya na wananchi wa vijiji vitano.
Katika mkutano huo, Ridhiwani ameishukuru serikali kwa kuendelea kutatua kero za wananchi, pia amemshukuru Rais Samia kwa kuridhia fedha hizo zilipwe ili wananchi wapishe na kupata maendeleo.
Vile vile ameishukuru serikali kwa kutenga fedha kwa ajili ya barabara mbalimbali katika halmashauri hiyo zitakazoongeza tija kiuchumi kwa wananchi wanaopitiwa na miundombinu hiyo.
Pia Ridhiwani ameishukuru serikali kwa matayarisho ya ujenzi wa barabara toka Mandera hadi Saadan ambayo inakwenda kufungua fursa kiuchumi.
Wakizungumza baada ya mkutano huo wananchi wa Mkange, wameeleza furaha yao na kumshukuru Mbunge wao  Ridhiwani ambaye siku zote amekuwa akipambana kuhakikisha anatatua changamoto zao.
Sheikh wa Mkange, Alhaj Khamis Nassor, ameelezea kuridhishwa namna mbunge wa jimbo hilo anavyoshughulika na changamoto za wananchi.
Akizungumza kwa niaba ya Chama Cha Mapinduzi, Mwenyekiti wa Chama  hicho Mwidadi Mauya amesema amepokea taarifa hiyo kwa furaha kubwa, akisema hivi sasa atakwenda kukisimamia chama kwakuwa jambo hilo lilimnyima uhuru wa kuzungumza.
 ”Mbunge huyu ni wa mfano wa kuigwa kwa jinsi anavyopigania maendeleo ya watu hasa watu wa Mkange. Sisi tutamuunga mkono na tuko naye na Mheshimiwa Rais ametuheshimisha Chama Cha Mapinduzi.
” Hakuna shida mwaka huu tutashinda kwa ukubwa sana,” amesema.
Serikali imeendelea kutenga fedha za maendeleo katika halmshauri hiyo, kwani zaidi ya Sh.Bilion 130 za miradi mbalimbali zimepelekwa wilayani hapo zikiwemo fedha za Elimu, Maji na Barabara.

You Might Also Like

UDSM Yaanzisha Mkakati Kuokoa Nyuki Wadogo

Mawakili Wa Serikali Watakiwa Kuzingatia Katiba Ya Nchi Wanapoandika Sheria

TEA Kukarabati Jengo La Bodi Ya Maktaba Kwa Milioni 300

Serikali Sekta Binafsi Kuimarisha Huduma Za Fedha Nchini

December 5, 2024

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Kanisa CAG Kuombea Uchaguzi Mkuu 2025
Next Article Serikali Inatoa Kipaumbele Kufikisha Umeme Taasis Zinazotoa Huduma Kwa Jamii- Kapinga
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Tume Ya Ulinzi Wa Taarifa Binafsi Yatoa Siku Saba Kwa Taasisi Kujisajili
Habari June 12, 2026
Teknolojia Ya Juisi YA Ndizi Kali Yafungua Fursa Mpya Za Viwanda, Ajira
Makala Uncategorized June 12, 2026
Serikali Yaingia Makubaliano Ya Ushirikiano Na DIT Kuimarisha Usimamizi Wa Mataifa
Habari June 8, 2026
Wananchi Waelimishwa Masharti ya Kubadilisha Noti Zilizochakaa, Kuungua na Kuchanika
Habari June 7, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?