MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, Laleta Furaha Kwa Watoto
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, Laleta Furaha Kwa Watoto
Habari

Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, Laleta Furaha Kwa Watoto

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: KITUO cha Afya Kimara kilichopo Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Dar es Salaam, kimekabidhiwa vifaa tiba vyenye thamani ya sh. Milioni 91 kwa watoto wachanga baada ya ujenzi wa ghorofa ya pili kukamilika.
Aidha kufanya jumla ya misaada yote iliyotolewa na Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho katika kituo hicho kufikia Sh. Milioni 688.
Mganga Mfawidhi wa Kituo hicho, Dkt. Malamla Chaulenzi amesema hayo, wakati akitoa taarifa fupi ya kituo hicho leo Januari 27, 2025.
Chaulenzi amesema ghorofa hiyo ya pili inazinduliwa rasmi leo baada ya vifaa vyote kukamilika kwa msaada wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho.
“Ukamilifu wa ghorofa ya pili umesaidia sana kutatua tatizo la ufinyu wa eneo la kituo kwa sehemu kubwa na kutoa nafasi ya huduma za matibabu ya watoto na kliniki za kibingwa kufanyika  na kuanzisha wodi ya watoto wachanga ambayo siku ya leo inazinduliwa rasmi,” amesema.
Amekiri kuwa kuwepo kwa wodi hiyo ya watoto wachanga kutarahisisha matibabu ya watoto wachanga hasa ikizingatiwa kituo hicho kinazalisha idadi kubwa ya watoto.
“Pia itaokoa gharama na usumbufu wa kwenda mbali kufuata huduma za afya katika vituo vingine,” amesema.
Amesema kanisa hilo kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo, walisaidia uboreshaji wa miundombinu kwa kujenga ngazi  ya kupandia iliyogharimu zaidi ya Shilingi milioni 100.
Pia walianza ujenzi wa ghorofa ya pili wenye thamani ya Sh. Milioni 495.
Rais wa Kanisa hilo, Juventenious Rubona amesema mpaka sasa miradi iliyokamilika katika halmashauri hiyo imegharimu sh. Milioni 753.
Ameitaja miradi hiyo kuwa ni Shule ya Msingi Kibamba iliyofanyiwa ukarabati, Kituo cha Afya Kimara na Kituo cha Afya Makuburi.
Amesema miradi inayokaribia kukamilika kuwa imegharimu Sh. Milioni 522, pamoja na shule zilizoanza kukarabatiwa zinagharimu zaidi ya Sh. Bilioni 1.1.
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Ubungo, Dkt. Tulitweni Mwinuka ameshukuru kwa msaada huo na kuahidi kusimamia matumizi yake visiharibiwe.

You Might Also Like

Rafiki Mkubwa wa Trump, Elon Musk atanufaika vipi baada ya kumuunga mkono?  

Wanawake Tumieni Fursa Zilizopo Kufanya Biashara

Biashara kidijitali inawezekana soko huru la Afrika

REA Yapamba Moto Uhamasishaji Matumizi Ya Umeme

Vipaumbele Vilivyopo Kwenye Mpango Wa Maendeleo Vitafsiriwe – Majaliwa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Kamishna TRA Atua Kwa Malasusa Kushirikiana Elimu Kwa Mlipa Kodi
Next Article Ridhiwani Ashiriki Kikao Cha Kazi Na Ajira Saudi Arabia
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?