MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: BRT Kuimarisha Uhusiano Tanzania, China
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > BRT Kuimarisha Uhusiano Tanzania, China
Habari

BRT Kuimarisha Uhusiano Tanzania, China

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: MRADI wa Mabasi Yaendayo Kasi (BRT), umekuwa ni sehemu muhimu ya urafiki wa  China na Tanzania, wenye kutoa mchango mkubwa katika uchumi, maendeleo na uboreshaji wa maisha.
Hayo yameelezwa na Meneja wa Usalama Tawi la Tanzania, kutoka Kampuni ya Ujenzi na Mawasiliano ya China (CCCC), Li Yuling wakati akizungumza na Waandishi wa habari katika kuadhimisha siku ya Jiao Zhu China -Tanzania.
Amesema mradi huo wa BRT, awamu ya nne sehemu ya tatu ni sehemu muhimu ya urafiki wa  China na Tanzania, na kwamba sio tu unaboresha usafiri wa umma wa Dar es Salaam ambao ni mji mkuu wa Tanzania, lakini pia unatoa mchango mkubwa katika uchumi.
 “Mradi huo unajumuisha ujenzi wa vituo muhimu vya usafiri, vituo vya mabasi na vifaa vingine vya trafiki. Unalenga kuboresha ufanisi wa usafiri wa mijini, kupunguza msongamano na kuimarisha hali ya usafiri ya wakazi wa eneo hilo,” amesema.
Amesema wameita waandishi wa habari kuonyesha watanzania juu ya dhamira ya makampuni ya Kichina katika maendeleo ya miundombinu inayoyafanya.
“Ili kuendeleza mafanikio hayo na kuadhimisha miaka 60 tangu kuanzishwa kwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya China na Tanzania, kampuni ya ujenzi ya China tawi la Tanzania imekutana na waandishi wa habari, kuzungumzia mafanikio hayo,” amesema.
Mwakilishi wa Mkandarasi katika mradi huo, You Xudong amesema mradi huo unaoendelea katika eneo la Kivukoni, utachukua miezi 18.
Amesema wanajenga jengo la ulinzi, choo, jengo la tiketi namba moja na jengo la tiketi namba mbili.
Naye Alvin Rujweka, Mwalimu kutoka Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam ( DIT), amesema wamekuwepo na wanafunzi wao wanaosomea uhandisi kwa ajili ya masomo ya vitendo katika kampuni hiyo ya kichina ya CCCC.
Amesema anafundisha ujenzi wa kutumia matofali, mawe na ufundi bomba.
“Wanafunzi wanaoandaliwa kuwa wahandisi, wanapewa elimu ya vitabu na vitendo.  Njia nyingine tunawapeleka kwenye miradi mbalimbali inayoendelea nchini, tunawaunganisha na soko kupitia fani walizosomea, ” amesema.
Mhitimu wa Diploma  DIT mwaka huu 2024, Benson Mbilinyi amesema amepata nafasi ya kujiunga na kampuni hiyo ya CCCC, anafanya kazi kama msaidizi wa mhandisi.
Amesema ametumia elimu yake ya chuo akichanganya na uzoefu wa vitendo anaoupata katika kampuni hiyo.
Ameshauri wanafunzi kujitokeza kwenye fursa kwani yeye mara ya kwanza alikutana na kampuni hiyo ilipokwenda chuoni kwao kuonyesha utendaji kazi kwa vitendo,

You Might Also Like

Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe

Wanazuoni Kujadili   Dira  Itakayojenga  Uchumi Unaofikia   Dola Trilioni Moja

Tani 27, 550  za ufuta zenye thamani ya bilioni 80 zimeuzwa

Tanzania Yalenga Kufikia Asilimia 51 Ya Ushiriki Wa Wanawake Katika Sayansi

Tanzania yaendelea kuwa Shule ya Utumishi Barani Afrika,

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Bajeti ya TUGHE 2025 Yaidhinishwa
Next Article TALGWU Chafanya Kikao Cha Baraza La Wafanyakazi Dodoma
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

VETA Kibaha Yatengeneza Simu Ya Mkononi Yenye Uwezo Wa Kupiga Na Kutuma Sms
Habari August 17, 2026
Wiki Ya Elimu, Ujuzi Na Ubunifu,UDSM Yabuni Dema La Kidigitali La Milango Sita Kusaidia Wavuvi
Habari August 17, 2026
TTCL  Yatumia Tamasha La Kizimkazi Kueleza  Wananchi Fursa Wanazotoa
Makala August 15, 2026
Rais Samia Afurahishwa Na Huduma za NSSF
Habari August 13, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?