MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Serikali Yawapeleka Wauguzi 101 Nchini Saudi Arabia
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Serikali Yawapeleka Wauguzi 101 Nchini Saudi Arabia
Habari

Serikali Yawapeleka Wauguzi 101 Nchini Saudi Arabia

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Ridhiwani Kikwete amesema kwa mara ya kwanza serikali inapeleka wauguzi 101 nchini Saudi Arabia kwa ajili ya kwenda kufanya kazi huko.
Ridhiwani amesema hayo leo Novemba 28, 2024 katika hafla ya kuwaaga watanzania wanaoenda kufanya kazi nchini Saudi Arabia.
“Tukio hili ni la kipekee sana, kwa kuwa ni mara ya kwanza kwa nchi yetu kupeleka watanzania wataalam kwenda kufanya kazi nje ya nchi kwa utaratibu rasmi unaoratibiwa na serikali.
“Aidha ni la kipekee kwa kuwa ni matunda ya kazi kubwa inayofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan kuwezesha watanzania kunufaika na diplomasia ya kiuchumi,” amesema.
Amesema kupelekwa kwa wauguzi hao ni matokeo ya kusainiwa kwa hati mbili za ushirikiano kati ya Tanzania na Saudi Arabia Novemba mwaka jana kuhusu uratibu wa ajira za watanzania nchini Saudi Arabia.
“Watanzania hawa tunaowaaga ni sehemu tu ya watanzania wengi watakaokwenda kufanya kazi nchini Saudi Arabia,” amesema.
Ridhiwani amesema suala la kuwezesha watanzania kunufaika na fursa za ajira nje ya nchi ni moja ya vipaumbele vya serikali katika kuongeza fursa za ajira kutoka watanzania 556,065 mwaka 2022 hadi milioni moja ifikapo 2028.
Pia kuongeza fedha zinazohamishwa na watanzania wanaofanya kazi nje ya nchi kutoka dola za kimarekani milioni 697.9 mwaka 2022 hadi bilioni 1.5 mwaka 2028.
Naye Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia, Mohamed Juma Abdalah amewakaribisha wauguzi hao, pia amewataka kulinda maadili na utamaduni wa kitanzania.
Pia amewataka kuzingatia taratibu, sheria na kanuni za nchi husika.

You Might Also Like

Kasekenya: Barabara ya Kakonko–Muhanga Ipo Katika Hatua za Awali za Kujengwa

Ajali ya treni Kigoma , abiria 70 wajeruhiwa

Watafiti Watumia Mbinu Mpya Kudhibiti Mdudu Kantangaze Kwenye Nyanya Bila Viuatilifu

Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, Laleta Furaha Kwa Watoto

DC Twange Apongeza Wananchi Kuchangia Maendeleo 

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wananchi Wachagua Viongozi Serikali Za Mitaa
Next Article Zuhura Yunus Atoa Neno Kwa Madereva 
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Nchi za SADC Zahimizwa Kuimarisha Umoja Kukabili Changamoto
Uncategorized July 17, 2026
Wananchi Washauriwa Kutumia  Wataalam Wa Ujenzi Kuepuka Madhara
Habari July 14, 2026
July 14, 2026
Uncategorized July 14, 2026
TANESCO Kutambulisha Mfumo Wa Kufunga Nyaya Kwenye Nyumba Ukifuatilia Matumizi Ya Umeme
Habari July 13, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?