MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wafanyabiashara 45 Wa Tanzania Wameanza Kutumia Soko La Eneo Huru La Afrika
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wafanyabiashara 45 Wa Tanzania Wameanza Kutumia Soko La Eneo Huru La Afrika
Habari

Wafanyabiashara 45 Wa Tanzania Wameanza Kutumia Soko La Eneo Huru La Afrika

Author
By Author
Share
2 Min Read

Na Lucy Lyatuu

WAFANYABIASHARA  45  wa Tanzania ndio waliotumia soko la eneo huru la Biashara la Afrika (AfCFTA)  kuanzia  mwaka jana 2023 hadi sasa.
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF) Raphael Maganga amesema hayo Dar es Salaam katika warsha ya mafunzo kwa wadau kuhusu fursa zilizopo AfCFTA.Warsha hiyo imeandaliwa na Baraza la Biashara la Afrika Mashariki (EABC).
Akizungumza Maganga amesema Tanzania ilijiumga na soko hilo mwaka 2021 na Kwamba biashara zimeanza kufanyika 2023 ambapo wafanyabiashara wanapeleka vitu tofautitofauti.
Amezitaja baadhi ya bidhaa zinazokwenda katika soko hilo kuwa ni mbolea, nafaka, Kahawa, katani,viungo  na hata bidhaa za kilimo na mchele.
Amesema mbali na Kampuni hizo lakini wanataka wasukume zaidi kampuni ambazo zina ongeza thamani kwenye bidhaa zao, nazo ziweze kushiriki kwa kuwa Tanzania haitaki kuendelea kukuza malighafi Bali kukuza bidhaa ambazo zitaongeza ushindani.
“Lazima na sisi tuchangamkie, muda umefika biashara za Tanzania zitoke,tusiwaogope wenzetu tayari serikali imesaini mikataba mbalimbali hivyo muhimu kuzifikia fursa hizo,” amesema Maganga.
Aidha amewahamasisha Watanzania kutumia muda huo ambao wamepewa wa kipekee (GTI) wa nchi nane  kuanza kupeleka bidhaa zao katika soko hilo badala ya kusubiria nchi zote  55 za Afrika kuanza.
‘Tanzania ni miongoni mwa nchi nane kati ya hamsini na tano za Afrika zilizochaguliwa kuanza kulitumia soko hilo,ambapo ni fursa muhimu ili kampuni nyingi zijitokeze Kwa wingi,” amesema.
Kwa upande mwingine amezitaka kampuni za kitanzania kuchangamkia mtaji  wa Dola bilioni moja uliotolewa na benkibya AfriExim Kwa ajili ya kuhakikisha zinafanya biashara katika soko hilo.
Kwa upande wake, Meneja wa Wanachama na Maendeleo ya Biashara kutoka EABC,Zefania Shaidi amesema lengo la warsha hiyo kujadili kuhusu  mfumo mzima wa biashara katika soko hilo Kwa kuwa tayari wapo wafanyabiashara wanapeleka bidhaa nchi za Moroco,Aljeria na hata Nigeria.
Amesema wamewakutanisha wafanyabiashara ambao tayari wameanza kutumia soko hilo Ili watoe  uzoefu wao pamoja na changamoto wanazokutana nazo Ili kutafuta ufumbuzi pia.

You Might Also Like

Wizara ya Nishati Yajivunia Jitihada Katika Kulinda Haki, Usawa na Kuwawezesha Wanawake

NSSF Kutekeleza Mradi Wa Uwekezaji Wa Jengo La Kitega Uchumi Dodoma

Mwongozo wa Mafunzo Elekezi Kwa Walimu Wapya Kazini Mbioni Kukamilika

Aliyeachishwa kazi kulipwa miezi 12, stahiki nyingine

Mpango Asema Tanzania, Korea Kubadilishana Wafanyakazi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Majaliwa Amwakilisha Rais Samia Kilele Kongamano la TEHAMA
Next Article Ulega: Miaka 50 ya ILRI imeinufaisha Tanzania 
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Miaka Minne Ya Samia Na Sekta Ya Elimu
Habari May 28, 2025
Chalamila Atoa Wiki Mbili Wafanyabiashara Ndogo Ndogo Kufungua Njia Kariakoo
Habari May 28, 2025
Mtanda Akagua Maendeleo Ya Mradi YA Hoteli Ya Nyota Tano Ya NSSF
Habari May 27, 2025
UDSM  Kujenga Jengo La Kisasa La Bil 8.3
Habari May 27, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?