MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TPHPA: Toeni taarifa mapema milipuko ya kwelea kwelea, nzige, viwavijeshi vamizi inapotokea
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TPHPA: Toeni taarifa mapema milipuko ya kwelea kwelea, nzige, viwavijeshi vamizi inapotokea
Habari

TPHPA: Toeni taarifa mapema milipuko ya kwelea kwelea, nzige, viwavijeshi vamizi inapotokea

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
WANANCHI wametakiwa kujenga utamaduni wa kutoa taarifa mapema, pindi wanapoona ndege aina ya kwelea kwelea au wadudu waharibifu nzige au viwavijeshi vamizi wameingia shambani ili zichukuliwe hatua haraka za kuwadhibiti kabla ya kufanya uharibifu wa chakula.
Hayo yameelezwa na Ofisa kutoka Mamlaka ya Mimea na Viuatilifu nchini (TPHPA), Godlove Kirimbo katika maonesho ya Wakulima, Wafugaji na Wavuvi yanayoendelea jijini Dodoma.
Amesema wananchi wanapoona visumbufu hivyo ,watoe taarifa kwa halmashauri husika ambayo pia itatoa taarifa kwenye Mamlaka hiyo kisha hatua za kuwadhibiti zinafuata .
Amevitaja visumbufu hivyo vya mlipuko kuwa ni ndege aina ya kwelea kwelea, panya waharibufu wa mazao, nzige na viwavijeshi kwamba hutokea kwa ghafla vikiwa katika makundi makubwa na kusababisha uharibifu wa chakula ndani ya muda mfupi.
Kirimbo amesema kuanzia Februari mwaka huu, kulikuwa na mlipuko mkubwa wa kwelea kwelea kwenye halmashauri 24 nchini  ambapo zaidi ya kwelea kwelea milioni 70 walivamia na  kushambulia mazao ya nafaka mtama,uwele,mpunga na alizeti.
“Mwaka huu tumerekodi kwelea kwelea zaidi ya milioni 70 walikuwa Tanzania na kundi sogo la kweleakwelea lenye milioni moja linaweza kuharibu tani 25 kwa siku moja,
“Lakini kundi dogo la nzige milioni 40 linaweza kuharibu chakula ambacho kingeweza kuliwa na watu 35,000 kwa siku,kwa hiyo unaona kwamba viumbe hivi wakiachwa ,nchi itaingia kwenye baa kubwa la njaa,” amesema.
Amesema visumbufu vya mlipuko  ni hatari kwa usalama wa chakula nchini huku akisema TPHPA wana jukumu la kuhakikisha usalama wa chakula nchini unalindwa kwa kuvidhibiti visumbufu hivyo.
Kwa mujibu wa Kirimbo,visumbufu aina ya kweleakwelea ni hatari kwa usalama wa chakula kwa sababu wana tabia ya kuishi kwenye makundi makubwa  ya kuanzia milioni moja kuendelea.

You Might Also Like

Ajali ya treni Kigoma , abiria 70 wajeruhiwa

Aliyeachishwa kazi kulipwa miezi 12, stahiki nyingine

Rais Samia Akabidhi Tuzo Kwa NSSF Ya Usimamizi,  Uratibu Wa Hifadhi Ya Jamii Kw Sekta Binafsi

Ridhiwani Kikwete Azindua Miradi Ya Thamani Ya Bil. 1.7 Songwe

DIT kudhibiti nzi wa maembe kisasa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wakulima wafunzwa kuhusu mlipuko wa panya TPHPA
Next Article Mikoa mitatu kuanzishwa vituo vya gesi asilia
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

JAB Yatoa Mwezi Moja Kuthibitishwa, kupewa vitabulisho
Habari May 22, 2025
Hali Ya Ulinzi Na Usalama Wa Mipaka Ni Salama
Habari May 22, 2025
Ulega Ataka Ushirikiano Miradi Ya Kimkakati Ikamilike Kwa Wakati
Habari May 22, 2025
Aloe Dorotheae, Mmea Unaopatikana Tanzania Pekee
Habari May 22, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?