Na Lucy Lyatuu,Dodoma
WIZARA ya Viwanda na Biashara imeeleza kuwa raia wa kigeni hawaruhusiwi kujihusisha na biashara 15 zinazostahili kufanywa na watanzania ikiwa ni hatua za kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara nchini.
Waziri wa Viwa da na Ujenzi,Judith Kapinga amesema hayo jijini hapa wakati akiwasilisha bajeti ya Wizara hiyo Bungeni na kuongeza kuwa katika mwaka 2025/2026 Wizara imefanikiwa kudhibiti raia wa kigeni kufanya biashara zinazostahili kufanywa na Watanzania kupitia Tangazo la Serikali Na. 487A la tarehe 28 Julai, 2025.
Amesema tangazo hilo linatoa katazo kwa raia wa kigerni kujihusisha na biashara 15 zinazostahili kufanywa na Watanzania.
Amezitaja biashara hizo ni pamoja na uUzaji wa bidhaa kwa jumla na rejareja, huduma za watalii wa ndani, huduma za fedha kwa njia ya simu (Mawakala), saluni, usafirishaji wa mizigo, uuzaji wa vinyago, uchimbaji mdogo wa madini, uanzishaji na uendeshaji wa vituo vya redio na runinga, uendeshaji wa viwanda vidogo, kampuni za huduma ya usafi na uuzaji wa nyumba na viwanja.
Amesema katika utekelezaji wa Sheria ya Katazo hilo, Wizara kwa kushirikiana na mamlaka mbalimbali imechukua hatua madhubuti za kisera, kisheria na kiutendaji ambapo hadi kufikia Aprili, 2026, Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imezuia uhuishaji wa leseni za biashara 907.
Amesema Kati ya hizo, leseni 737 ni za biashara za uingizaji na uuzaji wa bidhaa, leseni tano katika huduma za posta na utoaji wa vifurushi ndani ya mipaka ya itaifa, leseni 119 za uwakala au udalali katika biashara na sekta ya mali isiyohamishika na leseni 46 za huduma ya utoaji na usafirishaji wa shehena.
Kapinga amesema hatua hii imerejesha imani ya wazawa kwa Serikali kwa namna inavyosaidia kutatua changamoto za kibiashara; imeboresha mazingira ya biashara kwa wazawa na hivyo kuongeza uwekezaji kwenye biashara; na imeongeza uwezo wa ushindaji kwa wazawa kwenye biashara. Katika kuboresha utekelezaji wa katazo hilo, Serikali imefanya marejeo na kuandaa rasimu ya katazo ambayo ipo katika hatua ya uidhinishwaji.
Amesema amesema hadi kufikia Aprili, 2026, jumla ya maombi 373 ya vibali vya kazi kwa raia wa kigeni wanaokuja kufanya kazi nchini katika tasnia ya biashara hayakuidhinishwa kutokana na kutokukidhi vigezo vilivyowekwa kwa mujibu wa Sheria.
Amesema Vilevile, Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam na Mbeya zimezuia uhuishaji wa leseni za biashara 191 kwa biashara ya uuzaji wa bidhaa kwa jumla, uuzaji wa bidhaa kwa rejareja, uchimbaji mdogo wa madini na biashara ya maghala/stoo ambazo zinamilikiwa na wafanyabiashara/kampuni wasio raia wa Tanzania kwa kuzingatia amri iliyotolewa.
Ameongeza kuwa Biashara 13 kati ya 191 zilizozuiwa kuhuishwa au kupewa leseni zilikuwa katika eneo la kariakoo.

