Na Lucy Lyatuu,Dodoma
KATIKA kipindi cha mwaka 2025 Taasisi ya Mifupa Muhimbili ( MOI ) imeanzisha huduma mpya tisa za kibobezi ambazo hapo awali ziliwalazimu wagonjwa kuzifuata nje ya Tanzania.
Huduma zilizoanzishwa ni pamoja na
Upasuaji wa ubongo kwa kutumia akili unde ,upasuaji wa mgongo kwa njia ya matundu ,huduma ya kuchukua sampuli za vipimo kwa njia ya matundu, huduma ya kuweka tiba simenti kwenye pingili za mgongo zilizovunjika na huduma ya tiba ya maumivu.
Mkurugenzi Mtendaji wa MOI,Balozi Dkt Mpoki Ulisubisya amesema hayo wakati akitoa taarifa kuhusu maendeleo ya Taasisi hiyo na kuongeza Huduma nyingine bobezi iliyotolewani ya upasuaji rekebishi wa viungo vilivyopooza na huduma ya upasuaji wa uvimbe na ubongo kwa kutumia teknolojia ya fluorescein.
Amesema huduma nyingine ni kuanza kwa wodi mpya za kisasa za premier kwa ajili ya wagonjwa maalum na wakimataifa ili kukidhi mahitaji ya wagonjwa maalum na wakimataifa na
Kuanza kwa mfumo wa kuweka miadi kwa njia ya mtandao.
Dkt Mpoki Ameongeza kuwa Taasisi ya MOI imeendelea kutoa huduma nyingine za kibingwa Bobezi na kupunguza rufaa za kupeleka wagonjwa nje ya nchi ikiwa ni pamoja na upasuaji na uchunguzi wa mishipa ya damu kwenye ubongo bila kufungua fuvu na upasuaji wa Nyonga na magoti wa marudio.
Amesema wagonjwa 31 wa
Matibabu ya kiharusi kwa kupitia mishipa mikubwa ya damu
Upasuaji wa kunyoosha mgongo uliopinda (Kibiongo)
Kuondoa uvimbe kwenye ubongo kupitia tundu la pua, na Huduma ya maumivu sugu ya mgongo.
Amesema pia ipo huduma ya wagonjwa maalum na wagonjwa wa kimataifa, wagonjwa wamehudumiwa kutoka mataifa ya Congo, Comoro, Uganda, South Sudan, Burundi na mataifa mengine nje ya bara la afrika.
Aidha amesema MOI inatoa huduma ya mkono wa umeme na kutengeneza viungo bandia kwa kutumia teknolojia ya 3D,Upandikizaji wa nyonga bandia, Upandikizaji wa goti bandia,Upasuaji wa magoti kwa njia ya matundu, Upasuaji wa kuondoa vivimbe vya mishipa ya damu kwenye ubongo na
Upasuaji wa mfupa wa kiuno.
Amesema Katika kipindi cha mwaka mmoja, Taasisi ya MOI imefanikiwa kutoa huduma za kibobezi kwa wagonjwa 2,228 ambapo huduma hizo zimeiwezesha MOI kuokoa kiasi kikubwa cha fedha ambazo zingetumika kupeleka wagonjwa nje ya nchi.
Kadhalika amesema MOI Ina mpango wa Kusogeza huduma katika jengo lililokuwa la Hospitalibya Tumaini Upanga,Dar es Salaam ili baadhi ya wagonjwa wa nje waanze kupata huduma katika jengo hilo na kupunguza msongamano MOI.

