MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mwalunenge: Bila Rasilimali Watu Na Mtaji, Mipango Ya Kilimo Haitafanikiwa
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mwalunenge: Bila Rasilimali Watu Na Mtaji, Mipango Ya Kilimo Haitafanikiwa
Habari

Mwalunenge: Bila Rasilimali Watu Na Mtaji, Mipango Ya Kilimo Haitafanikiwa

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: MBUNGE wa Mbeya Mjini, Patrick Mwalunenge, amesema changamoto kubwa katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo nchini ni uhaba wa rasilimali watu wenye uelewa na fikra za kibiashara, hususan katika ngazi za halmashauri.
Ameeleza hayo bungeni jijini Dodoma wakati akichangia mipango ya utekelezaji ya Dira ya Taifa 2050.
Mwalunenge amesema licha ya mipango mizuri inayowasilishwa na Serikali, utekelezaji wake umekuwa dhaifu kwa sababu watendaji waliopo chini hawana uwezo wala mtazamo wa kibiashara, ilhali mpango huo kwa kiasi kikubwa unajikita kwenye dhana ya uchumi na biashara.
Amesema maoni yake yamejikita zaidi katika sekta ya uzalishaji, hususan kilimo ambacho kinaajiri kati ya asilimia 75 hadi 80 ya Watanzania.
Amekumbusha kuwa Serikali imejiwekea lengo la kufanya sekta ya kilimo kuchangia angalau asilimia 10 ya Pato la Taifa ifikapo mwaka 2030, akisisitiza kuwa lengo hilo halitafikiwa bila dhamira ya dhati katika utekelezaji.
Mwalunenge amesema sekta ya kilimo ndiyo nguzo kuu ya ajira nchini, lakini bado bodi za mazao ya kimkakati kama pamba, korosho, kahawa, kokoa, alizeti na ufuta hazijawezeshwa kifedha.
Ametolewa mfano Bodi ya Pamba ambayo kwa miaka mitano imekuwa ikihangaika kufikia uzalishaji wa tani laki tano, huku zaidi ya watu milioni 15 wa Kanda ya Ziwa wakitegemea zao hilo.
Aliongeza kuwa Tanzania inaendelea kutumia fedha nyingi kuagiza nguo kutoka nje, ilhali ina uzalishaji wa pamba, lakini ukosefu wa mtaji umezuia kufikiwa kwa uzalishaji unaohitajika kuanzisha viwanda vya nguo kuanzia ngazi ya nyuzi hadi bidhaa kamili.
Mwalunenge ameishauri Wizara ya Fedha kuziwezesha bodi za mazao kwa mitaji na kutoa dhamana maalum kwa uwekezaji wa kilimo.
Amesema mafanikio ya zao la korosho, ambapo uzalishaji umeongezeka na wakulima kupata zaidi ya Sh. Trilioni 1.5, ni ushahidi kuwa uwekezaji wa makusudi katika kilimo unaweza kutatua changamoto nyingi ikiwemo ajira, mapato na hata bima ya afya kwa wakulima.
Aidha, amesisitiza umuhimu wa Serikali kuweka mkakati mahsusi wa kutafuta masoko ya mazao nje ya nchi kwa kushirikisha balozi zake.

You Might Also Like

Atoa Maelekezo Kwa Chuo Cha Hombolo Kuwajengea Uwezo Viongozi Wa Mitaa Na Vijiji -Kapinga

Kiwanda cha Sukari Mkulazi Chaanza Kuleta Tija, Sangu Apongeza Uwekezaji wa NSSF na Magereza

Shilingi bilioni 4.6 kupeleka umeme maeneo ya migodi

Mdemu Azindua Utafiti Uliofanywa na FES Kwa Kushirikiana Na COTWU – T

Elimu Ya Fedha Yafika Makanya Same

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Gulamali Ahoji Bungeni Changamoto ya Mawasiliano Ilongelo
Next Article Mbunge Asisitiza Sheria za Majiko Safi Ili Kulinda Mazingira
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mbunge Asisitiza Sheria za Majiko Safi Ili Kulinda Mazingira
Habari February 3, 2026
Gulamali Ahoji Bungeni Changamoto ya Mawasiliano Ilongelo
Makala February 3, 2026
Serikali Yaendelea Kuimarisha Uhuru wa Mahakama – Nchimbi
Habari February 2, 2026
Mbarawa Aitaka Jamii Kulinda Miundombinu ya Uchukuzi
Habari February 1, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?