MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: CHAUMMA YAAPA KUJENGA BUNGE LA WABUNGE WA HOJA, SI MACHAWA
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > CHAUMMA YAAPA KUJENGA BUNGE LA WABUNGE WA HOJA, SI MACHAWA
Habari

CHAUMMA YAAPA KUJENGA BUNGE LA WABUNGE WA HOJA, SI MACHAWA

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
TABORA: MGOMBEA urais kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalim, amesema hataki wabunge ‘machawa’ bali wabunge madhubuti watakaokwenda kujenga hoja bungeni.
Mwalim amelsema, endapo atapata ridhaa ya kuongoza nchi, atahakikisha Bunge linakuwa na wabunge wenye uwezo wa kufanya utafiti ili kujenga hoja zenye tija kwa Taifa.
“Kama mbunge atakuwa na msaidizi mwenye uwezo mzuri wa kufanya utafiti, Bunge letu litakuwa la hoja, si la vihoja,” amesema.
Ameongeza kuwa wananchi wakichagua kwa mazoea, wataendelea kuongozwa kwa mazoea, hivyo aliwasisitiza wamchague mbunge anayefanya kazi, anayetoa hoja na kushika shilingi hadi hoja yake ipite.
Mwalim amewataka wakazi wa Urambo kutochagua kwa ushabiki bali kwa mabadiliko katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu.
Amesema kiwango cha umaskini na tatizo la ajira mkoani Tabora kinaongezeka, lakini wananchi bado wanaendelea kuikumbatia CCM licha ya kukosa maendeleo.
“Tangu dunia imeumbwa, Urambo ipo chini ya CCM, haijabadilika zaidi ya mikopo ya kausha damu. Badilikeni! Umaskini unakithiri, maisha ni magumu, halafu mnaichekea CCM — ikataeni,” amesema.
Mwalim amehoji mchango wa Urambo katika maendeleo, akisema:
“Mzee Samweli Sitta aliongoza Bunge vizuri na alijenga Bunge jipya, je, Urambo imefanyiwa nini?”
Amesema hana tatizo na Mama Magreth Sitta, lakini kama amechoka kisiasa ni heri atangaze kustaafu, kwani amekuwa madarakani kwa muda mrefu.
Amehitimisha kwa kuwataka wananchi wa Urambo kutofanya kosa katika uchaguzi huu, ili kupata majibu sahihi kuhusu dhahabu ya tumbaku na kuinua uchumi wa eneo hilo.

You Might Also Like

Imarisheni Mkakati Wa Kusimamia Usafi Wa Mazingira-Mhagama

Ridhiwani  Azindua Hafla ya Kuupandisha Mwenge, Mlima Kilimanjaro

Biteko Aiwakilisha Tanzania, Uapisho Wa Rais Boko, Botswana

Majaliwa ataka kuondolewe vikwazo vya rufaa za matibabu Afrika Mashariki

Mchengerwa Aongoza Ujumbe Wa Tanzania Kwenye Uzinduzi Wa Mkutano Wa Dunia Wa Tiba Asili

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article CWT Yatoa Wito Kwa Walimu Kujitokeza Kupiga Kura Oktoba 29 
Next Article VIONGOZI WA DINI WAONYA: ‘TUMIENI BUSARA, LINDENI AMANI WAKATI WA UCHAGUZI’
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Waziri Mbarawa Aagiza Adhabu Kali kwa Madereva, Makondakta Wanaonyanyasa Wanafunzi
Habari February 4, 2026
Mbunge Asisitiza Sheria za Majiko Safi Ili Kulinda Mazingira
Habari February 3, 2026
Mwalunenge: Bila Rasilimali Watu Na Mtaji, Mipango Ya Kilimo Haitafanikiwa
Habari February 3, 2026
Gulamali Ahoji Bungeni Changamoto ya Mawasiliano Ilongelo
Makala February 3, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?