MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Yonaz akabidhi boti ya doria kukabili vitendo vya kiuhalifu
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Yonaz akabidhi boti ya doria kukabili vitendo vya kiuhalifu
Habari

Yonaz akabidhi boti ya doria kukabili vitendo vya kiuhalifu

Author
By Author
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: KATIBU Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu ( Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonazi amekabidhi boti ya doria ya kukabiliana na vitendo vya kiuhalifu katika bahari na maziwa makuu nchini, kwa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania   (TASAC),
Akikabidhi boti hiyo Dkt.Yonazi amesema doria hizo ni mwendelezo wa juhudi za serikali za kukabiliana na vitendo vya kiuhalifu ikiwemo uvuvi haramu na uhamiaji haramu.
Vitendo vingine vya kiuhalifu ni usafirishaji wa dawa za kulevya, biashara za magendo na utoroshwaji wa nyara za serikali.
“Hivyo ni matumaini yangu kuwa boti hii itatimiza lengo hilo na kuimarisha juhudiza serikali za kukabiliana na vitendo vya kihalifu katika eneo letu la bahari,” amesema.
Pia amesema serikali ina imani kubwa na uwezo wa TASAC katika usimamizi, uendeshaji na utunzaji wa boti hii. Hiyo ndiyo sababu iliyofanya boti hii kukabidhiwa kwa shirika hili.
“Ni imani yetu kuwa mtaitunza vizuri boti hii ikiwa ni pamoja na kuifanyia matengenezo kinga kwa wakati na hivyo kuwaongezea ufanisi katika kazi zenu za kila siku hususan katika ukaguzi kwa meli zinazoingia kwenye maji yetu ya ndani,” amesema.
Naye Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi Ludovick Nduhiye ameagiza TASAC, kuhakikisha boti hiyo inasimamiwa na wataalam wenye weledi, taaluma na uzoefu.
Pia ameagiza TASAC kuhakikisha boti inapata matengenezo ya kinga kwa kuzingatia ratiba itakayopangwa.
Vile vile kuhakikisha boti inakuwa na teknolojia ya kisasa na vitendea kazi vitakavyowezesha watumiaji kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.
Awali Mkurugenzi Mkuu wa TASAC, Mohamed Salum amesema upatikanaji wa boti hiyo umefanyika katika wakati muafaka kwani utachagiza shughuli nyingi muhimu za utekelezaji wa vipaumbele vya Mradi wa Kukabiliana na Vitendo vya Kihalifu Bahari na Maziwa Makuu.
“Boti hii itasaidia utekelezaji wa majukumu ya TASAC iliyokasimiwa kisheria, hususan jukumu la usimamizi wa usalama, ulinzi na utunzaji mazingira dhidi ya uchafuzi utokanao na shughuli za meli.
“Boti tunayokabidhiwa leo itasaidia utekelezaji wa jukumu hili,”amesema.

You Might Also Like

Mawaziri Tanzania Profesa Mkenda, Silaa Mkutanoni Rwanda

Rais Samia Amehakikisha Elimu Ya Ufundi Stadi Inafikia Vijana Wote – Mkenda

Kuelekea Uchaguzi Mkuu, Wanaotumika Vibaya Waonywe

Serikali Kupeleka Umeme Maeneo Ya Kimkakati

Maofisa Habari Watoe Taarifa Sahihi Ziwafikie Wananchi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mkongo Wa Mawasiliano Unalenga Kuleta Tija Kwa Wananchi
Next Article Ujenzi Kiwanda cha Chumvi Waanza Lindi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Tume ya Kurekebisha Sheria Yaelimisha Umma Kuhusu Haki za Wanyama
Habari August 6, 2025
Bundi Wasaidia Kupambana na Panya: Teknolojia Asilia Inayobadili Maisha ya Wakulima
Habari August 6, 2025
Ofisa wa TARI Kuwapo Kila Kituo cha Umwagiliaji – Naibu Katibu Mkuu
Habari August 6, 2025
Mbinu Mpya za Kilimo kwa Vijana Zapata Umaarufu Nanenane Banda La VETA
Habari August 6, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?