MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Waziri Mkuu Aagiza Kuimarisha Ufuatiliaji Na Tathmini Kuleta Maendeleo
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Waziri Mkuu Aagiza Kuimarisha Ufuatiliaji Na Tathmini Kuleta Maendeleo
Habari

Waziri Mkuu Aagiza Kuimarisha Ufuatiliaji Na Tathmini Kuleta Maendeleo

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Mwandishi Wetu

NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe.Dkt. Doto Biteko amezitaka taasisi za ufutiliaji na tathmini kufanya kazi kwa weledi na kuimarisha eneo hilo ili kuendana na mahitaji yanayolenga kuleta tija katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Hayo yameelezwa leo Septemba 20, 2024 Zanzibar na Dkt. Biteko wakati akimwakilisha Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika Kongamano la Tatu la Ufuatiliaji, Tathmini na Kujifunza.

Amesema wataalam wa ufuatiliaji na tathmini wanawajibika kuilinda taaluma hiyo na kuwashawishi kwa hoja wakuu wa taasisi husika kupenda kazi zinazotokana na taaluma hiyo badala ya kujisikia wanyonge kitaaluma.

Aidha, Dkt. Biteko amewataka washiriki muda wote kusisitiza misingi ya taaluma hiyo na baadaye kuleta matokeo chanya kwa maendeleo ya Taifa na watu wake.

 

“Inawezekana katika maeneo yenu ya kazi wakawepo wakuu wa taasisi au viongozi wa serikali ambao hawapendi mfanye kazi yenu vizuri, kukubaliana na hilo ni kujiua wenyewe. Mnapotoka hapa mkafanye mkuu wa taasisi au kiongozi aone umuhimu wenu katika shirika.” Amesema Dkt. Biteko.

Aidha, amewataka wataalamu hao kusema ukweli na kusimamia taaluma yao.

“ Nataka niwaombe mkajiamini Rais Samia ameahiza na kuelekeza uwepo wa vitengo mbalimbali
mfuatilie fedha zinazopelekwa kwenye miradi na matokeo yake kwenye kubadilisha hali za maisha ya watu.” Amesisitiza Dkt. Biteko.

Kupitia kikao hicho, ametoa maagizo matano yakilenga kuboresha ufuatiliaji, tathmini na kujifunza.

Aidha ameielekeza Ofisi hiyo kukamilisha Sera ya Kitaifa ya Ufuatiliaji na Tathmini ili iwezeshe utekelezaji sahihi wa eneo la ufuatiliaji na tathmini nchini.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, William Lukuvi amesema Kongamano hilo la tatu la Ufuatiliaji, Tathmini na Kujifunza.

Amesema kauli mbiu ya kongamano ni ‘Kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi kwa kutumia teknolojia katika ufuatiliaji na tathmini na matumizi ya matokeo ya tathmini katika kufanya maamuzi’ limepata mwitikio mkubwa kutoka kwa wadau na washiriki.

 

Ametaja lengo la Kongamano hilo kuwa ni kuweka msisitizo kwenye lengo kuu la Serikali la kutoa huduma bora na kwa wakati kwa wananchi .

Naye, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, Dkt. Jim Yonazi amesema kupitia Kongamano hilo wamepata fursa mbalimbali ikiwemo kuwa na mchango mkubwa katika kuongeza uwezo wa wataalamu.

“ Kongamano hili limesisitiza umuhimu wa wananchi kushiriki katika mchakato mzima wa Ufuatiliaji na Tathmini ili kuimarisha uwazi, uwajibikaji na kuhakikisha Serikali na wahisani wanatoa huduma zenye tija. .” Amesema Dkt. Yonazi.
.

You Might Also Like

TASU yaiomba serikali inunue meli kutoa ajira kwa mabaharia

Biteko Agongea Msumari Elimu Ya Ufundi Stadi

TMA yatoa mwelekeo mvua za vuli 2024

Elimu Itolewe Kuhusu Ufahamu Wa Kuwepo Kwa Fedha Maalum – Ridhiwani

DAWASA na TARURA Kuendeleza Ushirikiano Ulinzi wa Miundombinu

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Muhimbili yarejesha tabasamu kwa Karume baada ya miaka 25 ya mateso
Next Article Rais Mwinyi aipongeza Airpay kudhamini tamasha la fahari ya Zanzibar, kusaidia wananchi kupata mikopo kidigitali
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?