MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Watuhumiwa 25 Wa Makosa Ya Mtandao Wakamatwa Na Polisi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Watuhumiwa 25 Wa Makosa Ya Mtandao Wakamatwa Na Polisi
Habari

Watuhumiwa 25 Wa Makosa Ya Mtandao Wakamatwa Na Polisi

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read

Na  Lucy Lyatuu

JESHI la Polisi kwa kushirikiana na mamlaka nyingine za kisheria ikiwemo Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) wamewakamata watuhumiwa 25 wanaojihulisha na makosa ya kimtandao katika maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam na mikoa mingine.

Kamanda  wa  Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema hayo Dares Salaam na kuongeza kuwa watuhumiwa hao ni pamoja na Kelvin Sauro mkazi wa Ifakara na wenzake 14.

Amesema wanatuhumiwa kuongoza kikundi cha kihalifu mtandaoni, kutumia laini za simu zisizo na usajili wao, kuingilia na kubadili namba za utambuzi halisi wa simu, (IMEI) kujipatia pesa kwa njia ya udanganyifu na kujifanya maofisa wa mfuko wa pensheni na kuwaibia wastaafu.

Kamanda Muliro amesema pia wanatenda makosa ya utakatishaji wa fedha.

Amesema watuhumiwa wamekuwa wakituma jumbe kama “tuma ile hela kwa namba hii’’ ‘’tuma kwenye namba hii ile pesa ya kodi’’. ‘Leta no za NIDA, Vitambulisho tukushughulikie mapunjo yako ya kustaafu’

Aidha amesema Jeshi hilo limemshikilia pia Enrique Adolph Ngagani na wenzake wanne  wa Sinza Kinondoni Dar es Salaam kwa tuhuma za kumiliki akaunti za mtandao wa Tiktok zinazotumika kusambaza taarifa zenye maudhui ya udhalilishaji wa watu mbalimbali kupitia Program za akili Unde (Artificial Intelligence – AI).

Amesema akametwa na kushikiliwa pia Baruani Hamisi Kateme maarufu kama Majani mkazi wa Kahororo Mkoa wa Kagera na wenzake wanne kwa tuhuma za udanganyifu  na utapeli kwa wastaafu na kuwaibia fedha kwa kujifanya kuwa ni wafanyakazi wa Mifuko ya pensheni na kuwa anashughulika na mapunjo ya wastaafu.

Amesema baadhi ya watuhumiwa wamekamatwa wakiwa na vifaa vya elekroniki kuhusiana na makosa yao kama simu janja 10, simu za kawaida 26,laini za simu 84 za kampuni mbalimbali, Memory cardy mbili, kompyuta mpakato moja, mashine ya kusajili laini mbili,gari na funguo moja.

Amesema baadhi ya watuhumiwa tayari wamefikishwa mahakamani Kisutu na wengine taratibu za kisheria zinakamilishwa ili wafikishwe mahakamani.

Kamanda Muliro amesema Jeshi hilo linatoa wito kwa wananchi kufuata sheria na kanuni za matumizi ya mitandao pia kuwatahadharisha wananchi kutokutoa vitambulisho vyao kama vya NIDA na vingine kwa watu wasiowajua.

Aidha amesema Polisi inatoa onyo kali dhidi ya wote wanaojihusisha na makosa ya kimtandao na mengine kwani watu hao watashughulikiwa vikali lakini kwa mujibu wa sheria.

 

 

You Might Also Like

Kutoka 1975 hadi 2025: TUCTA Yatimiza Ndoto Ujenzi Jengo La Biashara Arusha

UDSM Yapiga Hatua Kubwa Kuboresha Miundombinu na Mitaala kwa Mradi wa HEET

Si ruhusa kufuga, kuchunga, kuvua maeneo ya umwagiliaji

Roman Glorig Ahuisha Mkataba wa Uwakilishi wa Heshima wa Tanzania Nchini Czech

Katambi aitaka BRELA kuharakisha urasimishaji wa biashara

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article RC Dodoma Atoa Maagizo Kwa Ma – DC Kuhusu Ukame
Next Article Wanawake Taasisi za Kitafiti Watoa Furaha Kwa Waliojifungua, Madaktari, Manesi Kawe Kituo Cha Afya
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

CAG Aipongeza TARURA Kwa Ujenzi Wa Miundombinu
Habari January 9, 2026
Tuna Deni La Kusimamia Miradi Na Kusikiliza Kero za wananchi Ili Kuleta Maendeleo Ya Kweli-Salome
Habari January 9, 2026
Rais Dkt Samia Azindua Majengo Ya Kisasa
Habari January 8, 2026
TEA, UNICEF Watekeleza Miradi ya Elimu Visawani Zanzibar
Habari January 8, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?