MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wananchi Waelimishwe Kuhusu Utendaji wa Kamati za Maadili za Maofisa wa Mahakama
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wananchi Waelimishwe Kuhusu Utendaji wa Kamati za Maadili za Maofisa wa Mahakama
Habari

Wananchi Waelimishwe Kuhusu Utendaji wa Kamati za Maadili za Maofisa wa Mahakama

Author
By Author
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: WANANCHI wengi nchini wanakumbwa na changamoto ya kutokujua utaratibu sahihi wa kuwasilisha malalamiko yao dhidi ya ukiukwaji wa maadili unaofanywa na baadhi ya maofisa wa mahakama, jambo linalokwamisha upatikanaji wa haki kwa wakati.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Tume ya Utumishi wa Mahakama, Lidya Churi amesema changamoto hiyo inatokana na uelewa mdogo miongoni mwa wananchi kuhusu majukumu ya Tume pamoja na kamati zake za maadili.
“Tume ya Utumishi wa Mahakama inatekeleza majukumu muhimu ya kusimamia maadili ya maofisa wa mahakama, lakini bado wananchi wengi hawajui ni wapi wanapaswa kuelekeza malalamiko yao. Hali hii inaweza kusababisha kuwepo kwa malalamiko ambayo hayawasilishwi,” amesema
Amesema pamoja na kuwepo kwa mifumo ya kushughulikia malalamiko, ukosefu wa uelewa kuhusu kazi na mamlaka ya tume umekuwa kikwazo kikubwa katika kuhakikisha uwajibikaji na utoaji wa huduma bora kwa wananchi kupitia vyombo vya utoaji haki.
Churi amesisitiza kuwa ili wananchi waweze kufaidika ipasavyo na huduma zitolewazo na mahakama, ni muhimu kwao kufahamu kazi zinazofanywa na Tume ya Utumishi wa Mahakama, pamoja na kamati zake, ikiwemo Kamati ya Maadili.
Ametoa wito kwa taasisi za habari na wadau wa sheria kushirikiana katika kutoa elimu kwa umma kuhusu utendaji wa Tume na namna ya kuwasilisha malalamiko ya ukiukwaji wa maadili kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa kisheria.
“Wananchi wana haki ya kupata huduma ya haki kwa wakati, na hii inawezekana tu iwapo wataelewa mifumo ya uwajibikaji iliyo ndani ya mahakama zetu,” amesema.
Tume ya Utumishi wa Mahakama ni chombo huru kilichoanzishwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, chenye jukumu la kuhakikisha kuwa utumishi ndani ya mahakama unaendeshwa kwa weledi, uwazi na kwa kuzingatia maadili ya taaluma ya sheria.

You Might Also Like

Takukuru Kinondoni Yapokea Malalamiko 46 Kuhusu Rushwa

Wataalamu wa Tanzania, Kenya Watoa Ufafanuzi Kuhusu Maana Na Matarajio Ya Jumuiya Ya China, Afrika yenye Mustakabali wa Pamoja

VETA Shinyanga Yatumia Kompyuta Kubuni Bidhaa 

Wagonjwa Wenye Maumivu Makali Kupatiwa Tiba Radiolojia MNH

Waziri Ridhiwani Awataka Wafanyakazi Kuongeza Bidii Katika Kazi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article UDOM Yatafiti Dawa za Malaria, Vidonda vya Tumbo, Kisukari Kutoka Mimea ya Asili
Next Article Watanzania Watakiwa Kuachana Na Dhana Potofu Kuwa Nishati Safi Ya Kupikia Ni Gharama
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

FCC Yatoa Elimu Ya Ushindani Wa Kibiashara Katika Maonesho Ya  Biashara
Habari July 5, 2025
Watanzania Watakiwa Kuachana Na Dhana Potofu Kuwa Nishati Safi Ya Kupikia Ni Gharama
Habari July 5, 2025
UDOM Yatafiti Dawa za Malaria, Vidonda vya Tumbo, Kisukari Kutoka Mimea ya Asili
Habari July 5, 2025
Wanafunzi UDOM Wavumbua Mafuta ya Asili Kutoka Mabaki ya Zabibu
Habari July 5, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?