MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wakulima Wa Mahindi Mvomero Walia Na Viwavijeshi Vamizi, Watafiti SUA kupitia Mradi Wa AGRISPARK Kuokoa Jahazi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wakulima Wa Mahindi Mvomero Walia Na Viwavijeshi Vamizi, Watafiti SUA kupitia Mradi Wa AGRISPARK Kuokoa Jahazi
Habari

Wakulima Wa Mahindi Mvomero Walia Na Viwavijeshi Vamizi, Watafiti SUA kupitia Mradi Wa AGRISPARK Kuokoa Jahazi

Author
By Author
Share
4 Min Read

Na Mwandishi Wetu

MOROGORO: WAKULIMA wa mahindi Wilayani Mvomero Mkoani Morogoro wameiomba Serikali kupitia watafiti wake kutafuta suluhisho la kudumu la namna ya kuwakabili viwavi jeshi vamizi wanaoharibu zao la mahindi, huku familia zikikabiliwa na njaa pamoja na umaskini.

Wakizungumza na watafiti wa Mradi wa Mbinu Shirikishi za Wanafunzi na Wakulima Katika Uvumbuzi na Uhaulishaji  wa Maarifa na Teknolojia za Kilimo (AGRISPARK)  kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), wilayani humo wamesema kila mwaka hali inakuwa mbaya kwa kushindwa kuwadhibiti wadudu hao hatari,

Ambao sasa wanashambulia na mazao mengine ya kijani pale mahindi yanapokauka shambani.

Akizungumza kwa niaba ya wakulima wengine, Mkulima wa mahindi kutoka Kata ya Wami Dakawa wilayani Mvomero Mkoani Morogoro, Salehe Mwendi amesema kwa sasa kilimo kimekuwa kigumu, changamoto za wadudu na ukame vinawaacha masikini wakulima wengi kwenye maeneo mengi.

“Jamani tunaiomba serikali kupitia watafiti wake na mamlaka zingine zenye uwezo wa kusaidia kupata ufumbuzi wa wadudu hawa, miaka ya nyuma tulizoea ukilima mahindi unasubiria kuvuna lakini kwa sasa hali imekuwa mbaya sana bila kupuliza dawa hupati chochote shambani,

“Tunatumia nguvu kubwa kulima lakini wadudu wanatunyima mazao yetu hasa kwa sisi ambao hatuna uwezo wa kununua dawa,” amesema.

Amesema, “Kwa sasa tunalima shamba tunapanda na kuhudumia kwa kupalilia kisha tunaacha wadudu wale na kile watakachobakisha shambani ndicho na sisi mwisho tunaenda kuokoteza na kurudisha nyumbani kula na familia yetu,

“Maana tulikimbilia kwenye zao la mpunga ambalo nalo haliathiriwi na wadudu hawa lakini sasa kwa miaka mitatu mfululizo ndege wanakuja makundi kama mchanga wakishuka shambani siku moja wanamaliza hata ekari 12, yani tunateseka sana,”.

Naye mkulima mwingine Mzee Mohamed Kigonile ameomba watafiti wa Mradi wa AGRISPARK – SUA waandike vitabu na juu ya elimu sahihi ya kukabiliana na wadudu hao,vinavyoweza kutoa maelekezo sahihi ya namna ya kufanya ili kuokoa mazao yao.

“Tunajua ninyi watafiti kutoka kwenye Chuo chetu kikuu cha Sokoine Cha Kilimo (SUA) mnafanya kazi nzuri na tafiti nzuri kutusaidia wakulima tuzalishe kwa tija,

“Sasa tusaidieni kama kuna tafiti mlizofanya kuhusu wadudu hawa mtuletee tujifunze ili zitusaidie kuwatokomeza maana kwa uwezo wetu sisi tumefika mwisho tunahitaji msaada wenu na serikali. Mtuokoe njaa itatumaliza,” amesema.

Akizungumzia tatizo hilo Mtafiti Mkuu Mwenza wa Mradi wa AGRISPARK kutoka SUA Dkt. Nicholaus Mwalukasa amewaambia amepokea maombi yao, wanakwenda kutafuta machapisho ya kisayansi mbalimbali ambayo yamefanyika kuhusu namna ya kupambana na wadudu hao,

Wakiyapata wataandika vitabu vidogo ambayo vitaelezea na kufundisha namna ya kuwadhibiti wadudu hao.

“Tulipokuwa kwenye Kata ya Nyandira pia wakulima wametoa kilio hicho kwa wadudu hao katika zao la mahindi hivyo sisi kama watafiti tunalichukua na kwenda kulifanyia kazi maana tunamini zitakuwepo tafiti ambazo zimefanyika na kuchapishwa kwenye majarida ya kisayansi ya kimataifa ambayo sio rahisi nyinyi kuyafikia,

 

“Lakini sisi tutafanya hivyo kwa niaba yenu na kuwaletea kwa lugha rahisi ili muweze kuelewa,” amesema.

Watafiti hao wa mradi wa AGRISPARK kutoka SUA wametembelea wakulima kwenye wilaya ya Mvomero, Morogoro Manispaa na Halmashauri ya wilaya ya Morogoro Vijijini na kukutana na wakulima na kuungumza nao kuhusu mahitaji yao ya elimu kwenye shughuli za kilimo.

Pia changamoto zinazowakabili ili waweze kuwatafutia ufumbuzi wa changamoto zao kwa kuandaa vitabu vidogo vya kuwaelimisha kuhusu mahitaji yao.

Mradi wa AGRISPARK unafadhiliwa na serikali kupitia SUA ikiwa ni maono mapana ya uongozi wa chuo wa kutenga fedha za ndani kwa ajili ya kuwawezesha watafiti wake kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili.

 

You Might Also Like

Askofu Akemea Midoli Kuvishwa Nguo Za Ndani

GST Yaelezea Mafanikio Yake

DART Toeni Fursa Kwa Watanzania Kuwekeza kwenye Mwendokasi -Mchengerwa

Biteko Akaribisha Wawekezaji Sekta Ya Nishati

TAKUKURU kuelimisha madhara ya rushwa wakati wa uchaguzi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article COSTECH Yasaini Mkataba Ujenzi Jengo La Sayansi, Teknolojia, Ubunifu
Next Article VETA yafadhili mafunzo kwa wanawake 3000 jijini Dodoma
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?