MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wahitimu Kidato IV 2024, Washauriwa Kubadili Machaguo Ya Tahasusi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wahitimu Kidato IV 2024, Washauriwa Kubadili Machaguo Ya Tahasusi
Habari

Wahitimu Kidato IV 2024, Washauriwa Kubadili Machaguo Ya Tahasusi

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Danson Kaijage
DODOMA: WAHITIMU wa Kidato cha Nne mwaka 2024 wamepata fursa  ya kubadilisha machaguo ya tahasusi za Kidato cha Tano, Vyuo vya Kati na Elimu ya Ufundi kwenye mfumo wa kielektroniki wa uchaguzi wa wanafunzi watakaojiunga na kidato cha tano na vyuo.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais  -Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohammed  Mchengerwa, ameeleza hayo
alipozungumza na Vyombo vya Habari jijini Dodoma.
Amesema hatua hiyo ni maandalizi ya awali ya uchaguzi wa wanafunzi watakaojiunga Kidato cha tano na Vyuo vya Serikali Mwaka, 2025.
“Itakumbukwa kuwa Serikali imekuwa ikitoa fursa kwa wahitimu wa Kidato cha nne kufanya mabadiliko ya machaguo ya Tahasusi  na kozi mbalimbali walizozichagua kupitia Fomu ya Uchaguzi.
“Fursa hii huwawezesha wanafunzi kurekebisha machaguo yao kulingana na ufaulu waliopata kwenye matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne yaliyotangazwa na Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA),” amesema.
Mchengerwa amesema, serikali kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI imekamilisha kazi ya awali ya kuingiza kwenye kanzidata taarifa zilizo kwenye fomu za uchaguzi za wanafunzi kama walivyozijaza wakiwa shuleni.
Amesema kukamilika kwa kazi hiyo kunatoa fursa kwa wanafunzi kuweza kufanya mabadiliko ya machaguo, tahasusi ama kozi kwa njia ya mtandao.
“Baada ya wanafunzi kufanya marekebisho yao, kanzidata hiyo ndiyo itakayotumika kuwachagua na kuwapangia nafasi za Kidato cha tano na Kozi mbalimbali katika Vyuo vya Kati na vya Elimu ya Ufundi kwa kuzingatia sifa za ufaulu na machaguo yao.
“Ofisi ya Rais  TAMISEMI inatoa fursa kwa wahitimu wa elimu ya sekondari Kidato cha Nne, mwaka 2024 kubadili machaguo yao ili kutoa nafasi zaidi kwa mwanafunzi kusoma tahasusi au kozi itakayomwandaa kuwa na utaalamu stahiki katika maisha yake ya baadaye.
“Zoezi hili litatoa fursa zaidi ya wanafunzi kuongeza machaguo na kufanya machaguo mapya ya Tahasusi na Kozi.
“Napenda kuwasihi wazazi, walezi kushiriki katika jambo hili kwa kushauriana na watoto wao katika kufanya machaguo sahihi kulingana na ufaulu wao,” amesema.
Amesema wahitimu wote wanahimizwa kufanya marekebisho ya machaguo ya tahasusi na kozi kulingana na ufaulu wao, kwa kuingia kwenye Mfumo wa Uchaguzi wa Wanafunzi  unaopatikana kupitia kiunganishi cha selform.tamisemi.go.tz.
Amesema kazi hiyo ya kubadilisha
 tahasusi na vyuo litaanza rasmi Machi 31 Machi, 2025 hadi Aprili 30 2025.

You Might Also Like

MNH Kuvuna Mifupa Kutengeneza Taya

Shule 216 Za Serikali Zatumia Nishati Safi Ya Kupikia – Kapinga

Mwenda: Tupo kwa ajili ya kuzitatua changamoto za wananchi

TRC Yawatoa Hofu Wasafirishaji Mizigo Kwa Malori

Kipanga: Lugha ya Kichina Inakuza Diplomasia, Kuimarisha Uhusiano

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Tuwaombe Rais Samia, Mwinyi – Sheikh Swed
Next Article Matokeo Ya Usaili TRA Kutangazwa April 25,2025
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
PURA Yajipanga Gesi Asilia Itumike Kwenye Magari
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?