MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wafanyakazi Wapongeza Uzinduzi wa Miongozo, Mifumo ya Kielektroniki ya Ofisi ya Waziri Mkuu
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wafanyakazi Wapongeza Uzinduzi wa Miongozo, Mifumo ya Kielektroniki ya Ofisi ya Waziri Mkuu
Habari

Wafanyakazi Wapongeza Uzinduzi wa Miongozo, Mifumo ya Kielektroniki ya Ofisi ya Waziri Mkuu

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA:SHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), limesema uzinduzi wa miongozo na mifumo ya kielektroniki ya Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, inaweka historia mpya kwa wafanyakazi nchini.
Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa Tanzania (TALGWU), Rashid Mtima aliyemwakilisha Katibu Mkuu TUCTA, Very Mkunda amesema hayo wakati wa uzinduzi huo uliofanyika jijini Dodoma.
Habari Picha 9110
Mtima amesema uzinduzi huo unaweka historia kwa sababu mifumo hiyo inaleta uwazi na uwajibikaji zaidi katika utendaji wa wizara hiyo muhimu.
“Wafanyakazi wa Tanzania wanajivunia hatua hii muhimu. Miongozo na mifumo hii ya kielektroniki si tu kwamba inarahisisha kazi, bali pia inaleta utaratibu na uwazi unaotegemewa katika usimamizi wa kazi na ajira nchini,” amesena.
Ameongeza kuwa miongozo hiyo ni sehemu ya kutekeleza mkataba wa Shirika la Kazi Duniani (ILO), na hivyo Tanzania inaendelea kuonesha mfano mzuri wa utekelezaji wa haki na usawa mahali pa kazi kimataifa.
Mtima amesisitiza kuwa mifumo hiyo itawezesha majadiliano ya wazi kati ya serikali, waajiri na wafanyakazi, jambo ambalo halikuwepo kwa uwazi wa kiwango hicho hapo awali.
“Tumeweka historia kwa kuweka mifumo rasmi ya majadiliano, jambo ambalo halikuwahi kutekelezwa kwa uwazi huu. Sasa wafanyakazi wanapata mwongozo wa wazi kuhusu haki zao na wajibu wao, na hii ni hatua kubwa sana,” amesema.
Wafanyakazi nchini pia wamepongeza juhudi za serikali kurahisisha namna ambavyo wadau mbalimbali wanashirikiana, hasa katika kusimamia haki za wafanyakazi na kuhakikisha mazingira bora ya kazi.
Katika hatua nyingine, Mtima amewaasa wafanyakazi kuendelea kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan kwa juhudi zake za kuboresha maslahi ya wafanyakazi, akitolea mfano ongezeko la asilimia 35 la mishahara ambalo limekuwa ni la kihistoria.
“Hatujawahi kuona ongezeko la asilimia 35 kwa mara moja, na hii inaonesha dhamira ya kweli ya serikali katika kuimarisha maisha ya wafanyakazi. Tunatambua na kuthamini sana hatua hiyo,” amesema.

You Might Also Like

Balozi Sirro: Bila Amani, Maendeleo Hayapo Kigoma

Rais Wa CWT Suleiman Ikomba Sasa Ni Daktari

UDOM Yatafiti Dawa za Malaria, Vidonda vya Tumbo, Kisukari Kutoka Mimea ya Asili

BRAC Tanzania: Upo Umuhimu Sekta Binafsi, Serikali Kushirikiana

Ridhiwani: Maandalizi Mei Mosi  Yafikia Asilimia 88

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article JOWUTA Yakutana na Waziri Ridhiwani, Kamishna wa Kazi Kujadili Changamoto za Wanahabari
Next Article Majaliwa: Elimu Ya Watu Wazima, Silaha Ya Mapinduzi Ya Maendeleo
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?