MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: VETA Yatembelea Kiwanda Cha Kutengeneza Nyumba Bila Kutumia Tofali
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > VETA Yatembelea Kiwanda Cha Kutengeneza Nyumba Bila Kutumia Tofali
Habari

VETA Yatembelea Kiwanda Cha Kutengeneza Nyumba Bila Kutumia Tofali

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: WAFANYAKAZI kutoka Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), wametembelea kiwanda cha COTWORLD, kujifunza kuhusu teknolojia mpya ya ujenzi wa nyumba za kisasa bila kutumia tofali.
Wafanyakazi hao ni kutoka VETA Makao Makuu na Kanda ya Dar es Salaam, waliongozana na Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Anthony Kasore katika  kiwanda hicho kilichopo Kigamboni.
Mkurugenzi Mkuu huyo Kasore amesema, lengo la kutembelea kiwanda hicho ni kuangalia namna VETA na COTWORLD wanavyoweza kushirikiana ili kuwezesha wanafunzi wa vyuo vya VETA kupata mafunzo ya vitendo kuhusu teknolojia hiyo.
Amesema teknolojia hiyo inahusisha matumizi ya chuma katika kusimamisha kuta badala ya tofali, mbinu inayolenga kupunguza gharama na kuongeza ufanisi katika sekta ya ujenzi.
 Amesema VETA inaendelea kuimarisha ushirikiano na viwanda ili kuhakikisha wanafunzi wake wanapata ujuzi unaoendana na mahitaji ya soko la ajira.
“Tunahitaji kuwapa wanafunzi wetu maarifa na ujuzi wa kisasa ili waweze kushindana katika sekta ya ujenzi inayobadilika kwa kasi. Ushirikiano na viwanda kama COTWORLD ni hatua muhimu katika kufanikisha hili,” amesema.
Katika ziara hiyo, viongozi wa VETA walitembelea sehemu mbalimbali za kiwanda hicho na kushuhudia mchakato wa uzalishaji wa vifaa vya ujenzi vinavyotumika katika teknolojia hiyo mpya na kubaini fursa za mafunzo kwa wanafunzi wa VETA.
Baada ya ziara hiyo, pande zote mbili zimeahidi kushirikiana kwa karibu ili kuhakikisha vijana wanapata ujuzi wa vitendo katika ujenzi wa nyumba za kisasa.

You Might Also Like

Ridhiwani Ashiriki Mazishi Ya Mwenyekiti SHIVYAWATA

Waziri Mkuu Mstaafu Pinda Atoa Neno Kwa Vijana, Maadhimisho Miaka 30 VETA

Biteko Akaribisha Wawekezaji Sekta Ya Nishati

Mfumo Wa KieletronikiWa Albino Kurahisisha Kuwatambua – Ridhiwani

Ridhiwan Kikwete atembelea kituo cha kulelea watoto

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article ALAT Kujadili Ripoti Ya CAG
Next Article Kituo Cha Mkutano Cha Kimataifa Mlima Kilimanjaro Kuileta Dunia Tanzania
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?