MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: VETA Yaanzisha Kozi Mpya ya Teknolojia ya Mifumo ya Viwandani
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > VETA Yaanzisha Kozi Mpya ya Teknolojia ya Mifumo ya Viwandani
Habari

VETA Yaanzisha Kozi Mpya ya Teknolojia ya Mifumo ya Viwandani

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imeanzisha kozi mpya ya Teknolojia ya Mifumo ya Viwandani ‘Mechatronics’ katika baadhi ya vyuo vyake, ikiwemo Chuo cha VETA Kipawa kilichopo Dar es Salaam.
Akizungumza kuhusu kozi hiyo, katika kongamano la kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW), mtaalamu wa fani hiyo, Joshua Kingu kutoka VETA Kipawa MKoani Dar es Saalam amesema,
Habari Picha 9149
Kozi hiyo ni ya kisasa na inalenga kutoa ujuzi wa kiteknolojia unaoendana na mahitaji ya sasa ya viwanda.
Amesema zamani mitambo mingi ya viwandani ilikuwa inaendeshwa na binadamu, lakini sasa imebadilika na kuendeshwa na mifumo ya kielektroniki na kompyuta.
Amesema mabadiliko haya yamezua hitaji kubwa la wataalamu waliobobea katika teknolojia ya mechatronics.
Ameeleza kuwa kozi hiyo inalenga kuwapa wanafunzi wa VETA na watu wazima ujuzi wa kisasa, ili wanapopata ajira viwandani wawe tayari kufanya kazi kwa vitendo na kuendana na teknolojia mpya.
“Mitambo ya kisasa, kama ile inayotumika kwenye viwanda vya maji na saruji, imekuwa ya kielektroniki zaidi.
Wafanyakazi wanapaswa kuwa na uwezo wa kufunga, kutengeneza, na kutatua matatizo ya mitambo hiyo,” amesema.
Kwa upande wake, Ofisa Habari na Uhusiano wa VETA, David Mpondyo, amesema lengo la mamlaka hiyo ni kuwafikia Watanzania wote wanaotaka kupata mafunzo ya ufundi, bila kujali kiwango chao cha elimu au ujuzi wa awali.
“Tunataka kuhakikisha vijana wanapata ujuzi unaokidhi mahitaji ya soko la ajira, hasa katika kipindi hiki cha ukuaji wa viwanda vinavyotumia teknolojia ya kisasa,” amesema Mpondyo.
Amesisitiza kuwa zamani baadhi ya viwanda vililazimika kuagiza wataalamu kutoka nje kufundisha wafanyakazi wao, lakini sasa VETA inatoa mafunzo hayo nchini, jambo linalosaidia kupunguza gharama.
Mpaka sasa, VETA ina jumla ya vyuo 80 vya ufundi vilivyopo kwenye kila mkoa nchini, na vingine 65 vikiwa katika hatua mbalimbali za ujenzi.
“Kozi hii mpya haijamlenga kijana mwenye ujuzi tu, bali pia wale ambao hawajawahi kupata nafasi ya kujifunza. Lengo ni kuwaandaa vijana kujiajiri, kuajiriwa, au hata kuwaajiri wengine,” amesema Mpondyo, na kuongeza kuwa VETA itaendelea kuhimiza matumizi ya teknolojia bunifu ili kuchochea maendeleo ya viwanda hapa nchini.

You Might Also Like

Benjamini Mkapa Yapandikiza Mimba 21, Watano Waongezewa Nguvu Za Kiume

Waziri Mkuu Majaliwa Akoshwa Na Tafiti Ya Mhitimu OUT

Kongamano La Kwanza La Kodi Kufanyika Dar es Salaam

TUCTA Yaitaka Jamii Kuwapa Nafasi Vijana Wenye Changamoto za Kimwili

Wagonjwa 472 Waonwa Na Daktari Wa Mifupa MOI, 40 Wapendekezwa Kufika Dar kwa Matibabu

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Bodi Ya  Bima Ya Amana Yapata Mkurugenzi  Mkuu
Next Article Majaliwa Aagiza Kuimarishwa kwa Mafunzo ya Ufundi Stadi Nchini
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?