MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: VETA Kujenga Mahusiano Na Wenye Ujuzi, Wabunifu
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > VETA Kujenga Mahusiano Na Wenye Ujuzi, Wabunifu
Habari

VETA Kujenga Mahusiano Na Wenye Ujuzi, Wabunifu

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda amesema Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), imepewa maelekezo mahsusi ya kujenga mahusiano na wenye viwanda na wazalishaji wa  bidhaa ambazo zinahitaji ufundi au ufundi stadi.

Profesa Mkenda amesema hayo mkoani Dar es Salaam alipokuwa akizungumzia maadhimisho ya miaka 30 ya VETA pamoja na miaka 50 ya utoaji wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi kupitia taasisi mbalimbali za serikali nchini

Amesema, “Maadhimisho hayo yamekuja wakati mamlaka hiyo ina maelekezo mahsusi ya kujenga mahusiano na wale wenye viwanda na wazalishaji wa  bidhaa ambazo zinahitaji ufundi au ufundi stadi ambao unatolewa VETA,”.

Amesema wamekubaliana na mamlaka hiyo kwamba ndani ya miezi mitatu itakuwa na ‘frame work’ ya mahusiano kati ya vyuo vya VETA na viwanda au wazalishaji wa bidhaa zinazohitajika nchini ili kutoa fursa kwa wanafunzi wa mamlaka hiyo  kujifunza kwa vitendo,

Kwa wazalishaji au wenye viwanda kusaidia kutoa mafunzo kwa vijana na vile vile kunufaika na uwepo wa nguvu kazi hiyo katika vyuo.

“Utaratibu huu utahusisha na urasimishaji wa utaalam uliopo katika maeneo mbalimbali ya viwanda au uzalishaji,

“Kwa mfano wako watanzania sasa hivi wanatengeneza suti nzuri kwa muda mfupi ambazo zina hadhi ya kimataifa ni wajuzi ni wabunifu inawezekana hawajasomea mahali popote ubunifu wakati mwingine ni utundu wa mtu tunawahitaji hawa waweze kutusaidia katika vyuo vyetu vya VETA,

“Kwa kuwachukua vijana wanaosoma katika vyuo vyetu kufanya nao kazi wajifunze kutoka kwa hawa watu mahiri wachukue utaalam wao kwa vitendo na wakati huo huo watoe nguvu kazi kwa wazalishaji ili waweze kuzalisha kwa wingi zaidi kuhakikisha tunakidhi soko la ndani hata kwenda kuuza nje ya nchi,” amesema.

Waziri Mkenda amesema ili kufikia huko lazima kuwe na makubaliano maalum na utaratibu wa wazi ambao unaruhusu yeyote mzalishaji au mwenye kiwanda anaweza akaingia katika utaratibu huu kwa ushindani unaokubalika.

 

You Might Also Like

DIT kudhibiti nzi wa maembe kisasa

Waziri Mkuu Majaliwa aitaka uchukuzi lusimamia kwa karibu TRC

TARI Yawafikia Wakulima Kilosa, Kilimo Shadidi Cha Mpunga

Majaliwa Asema Sekta ya Uvuvi Yaingiza trilioni 2.9 kwa Mwaka 

COSTECH yazindua program kuwajengea uwezo wanawake kidijitali

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Rais Samia Amehakikisha Elimu Ya Ufundi Stadi Inafikia Vijana Wote – Mkenda
Next Article MOI Yaokoa Bilioni 150 Matibabu Ya Kibingwa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?