MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Uzinduzi wa Ubia Wiki Ya Ubunifu Tanzania 2025 Wafanyika
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Uzinduzi wa Ubia Wiki Ya Ubunifu Tanzania 2025 Wafanyika
Habari

Uzinduzi wa Ubia Wiki Ya Ubunifu Tanzania 2025 Wafanyika

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: UZINDUZI wa ushirikiano wa wabia katika Wiki ya Ubunifu Tanzania 2025, Umefanyika leo mkoani Dar es Salaam.

Wabia hao ni Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo  (UNDP) Tanzania, Vodacom Tanzania na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia ( COSTECH).
Mkuu wa Uhusiano na Vyombo vya Habari Vodacom Tanzania, Annette Kanora amesema uzinduzi huo umefanywa na wabia muhimu katika eneo la teknolojia.
Amesema UNDP kupitia Program ya Ufunguo Innovation, COSTECH  na wao Vodacom Tanzania wamezindua ubia huo kwa ajili ya wiki hiyo ya ubunifu itakayofanyika Mei 12 mpaka 16, Dar es Salaam.
“Wiki ya ubunifu ni jukwaa linaloleta pamoja taasisi mbalimbali, wabunifu mbalimbali katika kupeleka tasnia nzima ya ubunifu na teknolojia hapa Tanzania.
“Kupitia ubia wao kama Voda  tunaongeza nguvu, tunapata wazungumzaji mbalimbali toka ndani na nje ya nchi ili tuweze kubadilishana uzoefu wengine wanafanya nini.
“Tunaenda kujenga taifa ambalo ni endelevu, na linakuwa ni la kibunifu,” amesema.
Kwa upande wake, Mratibu wa Programu ya Funguo Innovation ambayo ipo chini ya UNDP inayoshirikiana na Umoja wa Ulaya na Serikali ya Uingereza, Joseph Evarest amesema ubia uliozinduliwa utakuwa ni jukwaa la kuonyesha nini kinafanyika katika eneo la ubunifu na teknolojia.
“Tunaamini kupitia ubunifu kuna biashara nyingi zinachipuka, kuna biashara mpya, kuna teknolojia nyingi zinakuja kwa hiyo ni kwa ajili ya kutoa nafasi kwa wadau mbalimbali ambao wako katika nafasi hiyo kuonyesha wanafanya nini.
“Lakini vile vile kusikiliza kuna mahitaji gani ya kiubunifu na kiteknolojia katika nafasi ya Tanzania.
“Tunajua Tanzania inakuwa kwa kasi sana na uchumi unabadilika. Shabaha  ya Funguo ni kusaidia  vijana wanaibua biashara bunifu katika mitaji, msaada wa kiufundi pia masuala ya kusera yaliyopo ambayo yanakwamisha,” amesema.
Naye Kiongozi katika Mashirikiano, Promise Mwakale kutoka COSTECH amesema ubia walioingia utanufaisha vijana kwa kuwa Wiki hiyo ya ubunifu itakuwa na majadiliano kwa ajili yavwanafunzi, pia itawawezesha kupata nafasi mbalimbali.
“Huu ni muda wa kukutana na wabunifu. Kama COSTECH tuna furaha kuwa sehemu ya huu ushirikiano kwa kuifanya Wiki ya Ubunifu kuwa Kubwa zaidi,” amesema.

You Might Also Like

Afrika ijadili changamoto sekta ya utalii – UN

Watahiniwa 72 wa kidato cha nne wafutiwa mtihani kwa udanganyifu, kuandika lugha za matusi

Baraza La Madiwani Lampongeza Rais Samia Kwa Utekelezaji Wa Ilani

Waziri Mkuu Mstaafu Pinda Atoa Neno Kwa Vijana, Maadhimisho Miaka 30 VETA

Sera mpya ya viwanda kuzinduliwa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Serikali Yaahidi Kupatia Dawa Kilio Cha Ushuru Kwa Malori
Next Article Wanachuoni Katika Mawasilianao ya Utamaduni kati ya China na Afrika
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?