MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Utafiti Wa Nguvu Kazi, Mapato Ya Kaya Kutoa Taswira Mpya Ya Maendeleo
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Utafiti Wa Nguvu Kazi, Mapato Ya Kaya Kutoa Taswira Mpya Ya Maendeleo
Habari

Utafiti Wa Nguvu Kazi, Mapato Ya Kaya Kutoa Taswira Mpya Ya Maendeleo

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: OFISI ya Taifa ya Takwimu ( NBS), inafanya utafiti nchi nzima katika maeneo ya ajira, mapato ya kaya, huduma za kijamii, na matumizi ya nishati safi.

Aidha utafiti wa kitaifa wa nguvu kazi unaendelea, ukikusudia kutoa takwimu sahihi kuhusu watu wenye uwezo wa kufanya kazi nchini kujua umri wao, jinsi na maeneo wanakoishi.

Ofisa Masoko Mwandamizi wa Takwimu wa NBS, Andrew Punjila amesema hayo katika Maonesho ya 49 ya Kitaifa ya Biashara yajulikanayo kama Sabasaba yaliyomalizika jana Julai 13, 2025 mkoani Dar es Salaam.

Amesema utafiti huo ni nyenzo muhimu kwa Serikali katika kupanga na kuboresha mikakati ya ajira, ikiwa ni pamoja na programu za kukuza ajira katika sekta mbalimbali.

Amesema NBS imeendelea kuelimisha umma kuhusu matumizi ya takwimu rasmi kupitia maonyesho mbalimbali.

Pia amesema taarifa kutoka kwenye sensa na tafiti zingine zinaonyesha hali ya kijamii katika jami ikiwa ni pamoja na hali ya elimu, huduma za afya, nishati safi, na changamoto kama ukataji miti unaochangia uharibifu wa mazingira.

“Tunazo takwimu za hali ya uoto wa asili kuanzia mwaka 2002 hadi 2022, ambazo zinaonyesha kupungua kwa misitu na uoto wa asili kutokana na matumizi makubwa ya kuni na mkaa.

“Serikali kwa sasa inahamasisha matumizi ya nishati safi, na takwimu hizi zina msaada mkubwa katika kubaini maeneo yenye changamoto zaidi na kuweka mikakati ya kuboresha hali hiyo,” amesema Punjila.

Amesena NBS inatekeleza utafiti wa mapato na matumizi ya kaya ambao unapita kaya kwa kaya katika maeneo yote ya nchi, hadi kwenye ngazi ya maeneo ya kuhesabia.

Utafiti huo unalenga kutoa picha ya ustawi wa jamii, upatikanaji wa huduma za kijamii, na hali ya kiuchumi ya Watanzania.

Amesema takwimu hizo pia hutumika katika kukokotoa mfumuko wa bei, hali ya umasikini, na viashiria vingine vya maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Amesema Ofisi ya Taifa ya Takwimu inaendelea kutoa wito kwa wananchi na taasisi mbalimbali kuvitumia vyanzo hivyo vya taarifa kwa ajili ya maendeleo binafsi na ya kitaifa.

Amevitaka vyombo vya habari kushirikiana na NBS katika kuelimisha umma juu ya umuhimu wa takwimu rasmi, kwa kuwa ni msingi imara wa mipango yenye tija.

Kwa upande wake Mtaalamu wa Mfumo wa Taifa wa Kijiografia NBS, Andrew Gondwe amesema ofisi hiyo huzalisha takwimu muhimu za kijiografia ambazo huchambua hali ya upatikanaji wa huduma mbalimbali kama vile elimu, afya, maji, na hata huduma za kifedha katika maeneo mbalimbali ya nchi.

Amesisitiza umuhimu wa wadau, wakiwemo wawekezaji na watunga sera, kutumia takwimu hizo katika kupanga maendeleo.

“Takwimu hizi si tu kwa ajili ya Serikali. Zinawafaa pia wajasiriamali na wawekezaji. Kwa mfano, mfanyabiashara anaweza kutumia takwimu hizi kupanga mahali pa kufungua huduma fulani kulingana na upatikanaji au ukosefu wa huduma hiyo katika eneo husika,” amesema Gondwe.

You Might Also Like

Watanzania wasisitizwa kulinda mazingira ya miundombinu ya umeme

Vyama Vya Wafanyakazi Vihimize Waajiri Kutoa Taarifa WCF, Zinazohusu Wafanyakazi Wanaopata Ajali, Ugonjwa Kazini

Wakulima wafunzwa kuhusu mlipuko wa panya TPHPA

Watumishi wa Umma wafahamu haki ya rufaa Kwa mujibu wa sheria

BRAC Tanzania: Upo Umuhimu Sekta Binafsi, Serikali Kushirikiana

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Majaliwa Aituza UDSM kwa Kuongoza Eneo La Elimu, Utafiti, Ubunifu Sabasaba 2025
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Majaliwa Aituza UDSM kwa Kuongoza Eneo La Elimu, Utafiti, Ubunifu Sabasaba 2025
Habari July 14, 2025
Nyanya Cheri na Ngogwe Chungu Zarejea 
Habari July 13, 2025
NFRA Yawaalika Wadau Kununua Nafaka kwa Masoko ya Ndani na Nje
Habari July 13, 2025
Kafulila: Ushirikiano wa Sekta Binafsi na Umma Kuboresha Huduma
Habari July 13, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?