MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Ushiriki Wa Wanawake, Wasichana Katika Sayansi Ni Mdogo
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Ushiriki Wa Wanawake, Wasichana Katika Sayansi Ni Mdogo
Habari

Ushiriki Wa Wanawake, Wasichana Katika Sayansi Ni Mdogo

Shani
By Shani
Share
2 Min Read

Na Mwandishi Wetu

 

DODOMA: TAKWIMU za elimu na ajira duniani zinaonesha kuwa ushiriki wa wanawake na wasichana katika elimu na ajira katika fani za sayansi ni mdogo ikilinganishwa na ushiriki wa wanaume.

 

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Omari Kipanga amesema

hayo leo Februari saba, 2024 alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu siku ya maadhimisho ya Kitaifa ya wanawake na wasichana katika Sayansi ambayo huadhimishwa kila ifikapo Februari 11.

 

Kipanga amesema kwa takwimu za Tanzania ushiriki wa wanawake ni asilimia 36 na wanaume ni asilimia 64, hali inayopunguza juhudi za kufikia usawa.

 

Amesema mgeni rasmi atakuwa ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknologia Profesa.Adolf Mkenda,

 

Amesema lengo la kuadhimisha siku hiyo ni kutambua na kusherehekea mchango wa wanawake na wasichana katika nyanja za sayansi, teknolojia, uhandisi na hisabati (STEM).

 

Pia amesema maadhimisho haya ni fursa ya kuhamasisha wanawake na wasichana zaidi kujiunga katika nyanja hizi ili kubadili mustakabali wao na jamii zetu kwa ujumla.

 

“Baraza Kuu la Umoja wa MATAIFA mwaka 2015, lilipitisha programu ya Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake na Wasichana katika Sayansi kwa kutangaza tarehe 11 Februari kuwa Siku ya Kimataifa ya Wanawake na Wasichana katika sayansi.,”ameeleza.

 

Amesema Tanzania inatambua kuwa usawa wa kijinsia ni muhimu sana kwa kufikia malengo ya maendeleo yaliyokubaliwa kimataifa, ikiwa ni pamoja na Ajenda ya 2030 ya Maendeleo Endelevu.

 

Kipanga amesema kutokana na maazimio hayo ya Umoja wa mataifa, Tanzania imekuwa ikiadhimisha siku ya Kimataifa ya Wanawake na Wasichana katika Sayansi kuanzia mwaka 2021.

 

“Masuala ya wanawake na wasichana ni mtambuka, hivyo yanahitaji ushiriki na mchango wa wadau wote bila kujali wako katika sekta ya umma au binafsi,

 

“Tnahitaji kuhamasisha kizazi kilichopo na kijacho cha wasichana kupenda na kujiunga na masomo ya sayansi kwa kuondoa dhana potofu na kutoa fursa sawa katika elimu na maendeleo ya kitaaluma”amesema.

You Might Also Like

Mnyororo wa Biashara Kariakoo Unafanywa Na Wageni

SIDO jengeni viwanda 20 Kila mkoa-Jafo

𝐓𝐅𝐒 Y𝐚𝐧𝐝𝐚𝐚 M𝐤𝐚𝐤𝐚𝐭𝐢 W𝐚 M𝐢𝐚𝐤𝐚 1𝟎 Ku𝐞𝐧𝐝𝐞𝐥𝐞𝐳𝐚 N𝐚 K𝐮𝐡𝐢𝐟𝐚𝐝𝐡𝐢 M𝐢𝐬𝐢𝐭𝐮 Ya Mi𝐤𝐨𝐤𝐨 𝐓𝐚𝐧𝐳𝐚𝐧𝐢𝐚 𝐁𝐚𝐫𝐚

TEA Mshindi wa Kwanza Maonyesho Ya Mfuko wa Utamaduni

TARI Yabadilisha Kilimo kwa Teknolojia Mpya, Za Kisasa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Tanzania Kuwa Mwenyeji Wa Mkutano Wa Petroli Afrika
Next Article Wachimbaji Wadogo Wafikiwa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Tume ya Kurekebisha Sheria Yaelimisha Umma Kuhusu Haki za Wanyama
Habari August 6, 2025
Bundi Wasaidia Kupambana na Panya: Teknolojia Asilia Inayobadili Maisha ya Wakulima
Habari August 6, 2025
Ofisa wa TARI Kuwapo Kila Kituo cha Umwagiliaji – Naibu Katibu Mkuu
Habari August 6, 2025
Mbinu Mpya za Kilimo kwa Vijana Zapata Umaarufu Nanenane Banda La VETA
Habari August 6, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?