MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Usafirishaji Shehena Waingiza Dola Bilioni 3.54
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Usafirishaji Shehena Waingiza Dola Bilioni 3.54
Habari

Usafirishaji Shehena Waingiza Dola Bilioni 3.54

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: MAMLAKA ya Afya ya Mmea na Viuatilifu (TPHPA), imewezesha usafirishaji wa shehena  za mazao mbalimbali tani milioni 3.5 kwenda nje ya nchi, kupitia ukaguzi wa mipaka.
Aidha usafirishaji wa shehena hizo umeingizia Tanzania Dola Bilioni 3.54 kwa mwaka kupitia ukaguzi unaofanywa mipakani.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mmea na Viuatilifu (TPHPA), Profesa Joseph Ndunguru amesema hayo alipozungumza na Mwandishi wa Mfanyakazi Tanzania.
Profesa Ndunguru amesema pia mamlaka hiyo imekamilisha nyaraka za kufungua masoko kwa mazao tisa katika nchi 14 ambazo tayari nyaraka hizo zimekabidhiwa balozi za nchi husika.
“Ufunguaji wa masoko hayo utaingizia Tanzania kiasi cha Dola Bilioni 3.5 kwa mwaka.
“Uwezeshaji wa masoko tayari shehena ya kwanza ya parachichi imesafirishwa kwenda China,” amesema.
Kwa upande mwingine Profesa Ndunguru amesema, mamlaka hiyo imewezesha upatikanaji taarifa za kufungua masoko kwa mazao tisa katika nchi 14.
Ameyataja mazao hayo kuwa ni vanilla, soya, parachichi, mananasi, viazi mviringo na mengineyo.
Amesema taarifa hizo wameshapatiwa nchi husika na tayari taratibu za kuuza mazao kwenye nchi hizo zinaendelea.
“Kwa hiyo kwa sasa hivi mamlaka kwa kuwepo kwetu mipakani ofisi 36 hizo  pamoja na mipaka ya nchi kavu na viwanja vya ndege sasa takwimu za mauzo ya mazao yanayoenda nje na kuingia ndani zinapatikana TPHPA.
“Sasa hivi unaweza kuitisha taarifa yoyote hata sasa hivi nikitaka kujua mpaka wa Tunduma mwezi huu wamepitisha mazao gani, wameingiza fedha kiasi gani unaipata kwenye kituo chetu cha Arusha.
“Kwa hiyo ukitaka kwa mwezi kwa mwaka utapata kila kitu, na kwa zao unapata data zake,” amesema.
Amesema data hizo zinatumiwa pia na Wizara ya Kilimo kwa ajili ya kupata majibu ya taarifa mbalimbali.

You Might Also Like

Maofisa Habari Watoe Taarifa Sahihi Ziwafikie Wananchi

Tafiti Katika Afya Nyenzo Muhimu

MWALIM: Njaa na Ukosefu wa Ajira Ni Matokeo ya Uongozi wa CCM

Sekta Ya Madini Yazidi Kuchangia Ukuaji Wa Uchumi – Majaliwa

Shemdoe apongeza

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TPHPA Yanunua Ndege Kudhibiti Visumbufu Vya Mazao
Next Article NHIF Kuingia Makubaliano Na Mawakala Usajili Wa Wananchi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Vitabu Vya Sauti Kuvutia Vijana, Serikali Yapongeza Ubunifu Wa Mkuki Na Nyota
Habari November 22, 2025
Ubora Wa E & D Vision Publishing Wamkuna Waziri Kabudi Maonyesho Ya Vitabu Dar
Habari November 22, 2025
Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 
Habari November 22, 2025
Kwagila Awataka Wasimamizi Wa Elimu TAMISEMI Kuwajibika Kikamilifu
Habari November 21, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?