MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Unywaji Maziwa Shuleni Kuongeza Ufaulu, Kuboresha Afya – RAS Geita
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Unywaji Maziwa Shuleni Kuongeza Ufaulu, Kuboresha Afya – RAS Geita
Habari

Unywaji Maziwa Shuleni Kuongeza Ufaulu, Kuboresha Afya – RAS Geita

Author
By Author
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

GEITA: KATIBU Tawala wa Mkoa wa Geita, Mohammed Gombati amesema unywaji wa maziwa safi na salama kwa wanafunzi wa shule ni hatua muhimu katika kuongeza ufaulu na kuboresha afya za watoto mkoani humo.

Akizungumza leo wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Wadau wa Tasnia ya Maziwa, lililofanyika katika Ukumbi wa Nyerere, Viwanja vya Maonesho vya Dkt. Samia Suluhu Hassan mjini Geita, Gombati amesema maziwa ni chanzo bora cha lishe ambacho kitasaidia wanafunzi kuepuka udumavu wa mwili na akili.

“Walimu, wazazi na walezi wana jukumu kubwa kuhakikisha watoto wanapata maziwa shuleni. Zoezi hili lazima liwe endelevu ili kuleta matokeo chanya kwa vizazi vya sasa na vijavyo,” amesema Gombati.

Kwa upande mwingine, Katibu Tawala huyo aliwataka maofisa lishe kuendelea kuelimisha jamii juu ya faida za lishe bora, hususan matumizi ya maziwa safi, huku akiagiza maofisa mifugo kuwahamasisha wafugaji kufuga kisasa ili kuhakikisha upatikanaji wa maziwa kwa mwaka mzima.

Katika kongamano hilo, Kaimu Msajili wa Bodi ya Maziwa Tanzania,  Deorinidei Mng’ong’o, amesema lengo kuu la mkutano huo ni kuandaa mpango maalum na endelevu wa kuhakikisha watoto shuleni wanapata maziwa kila siku ili kukuza ustawi wa afya zao na kuongeza uwezo wao wa kujifunza.

Kauli mbiu ya kongamano hilo ilikuwa:
‘Kwa Matokeo Mazuri Shuleni na Afya Bora, Maziwa Ndiyo Mpango Mzima’.

 

 

 

 

You Might Also Like

Vijana Wahimizwa Kushiriki Kikamilifu Soko Huru la Afrika

Waislamu Watakiwa Kusimamia Misingi Ya Upendo, Ushirikiano, Amani

VETA Mtwara Watua Na Mwani Maadhimishilo Ya Miaka 30

Umwagiliaji kumwezesha mkulima kulima mara mbili mpaka tatu kwa mwaka

Watanzania Watakiwa Kuachana Na Dhana Potofu Kuwa Nishati Safi Ya Kupikia Ni Gharama

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wananchi Wafurika Banda la REA Kupata Majiko Ya Bei Nafuu Maonesho ya Madini Geita
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Wananchi Wafurika Banda la REA Kupata Majiko Ya Bei Nafuu Maonesho ya Madini Geita
Habari September 23, 2025
TEITI Yashiriki Maonesho ya Nane ya Uwekezaji Sekta ya Madini Geita
Habari September 23, 2025
Fema Mining & Drilling Mfano wa Kuigwa – Musukuma
Habari September 23, 2025
Mgodi Wa Dhahabu Wa Nyanzaga Kunufaisha Wananchi, Ujenzi Wazidi Kupaa
Habari September 23, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?