MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: UDSM Yamtunuku Rais AfDB Shahada Ya Heshima Ya Sayansi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > UDSM Yamtunuku Rais AfDB Shahada Ya Heshima Ya Sayansi
Habari

UDSM Yamtunuku Rais AfDB Shahada Ya Heshima Ya Sayansi

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: CHUO Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), kimemtunuku Shahada ya Heshima ya Sayansi, Rais na Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Dkt. Akinwumi Ayeodeji Adesina leo Juni 13, 2025.
Makamu Mkuu Mstaafu UDSM, Profesa Rwekaza Mukandala ameeleza hayo katika mahafali ya 55 ya chuo hicho Duru ya Kwanza Yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City.
Profesa Mukandala amesema, kwa mujibu wa kanuni za tuzo ya shahada za Heshima za UDSM za mwaka 2014,
” Shahada ya heshima inaweza kutolewa kwa mtu mwenye angalau shahada ya kwanza ambaye, amechangia kipekee katika kuendeleza tasnia ya ujifunzaji,
” Ametoa mchango mkubwa na wa kipekee katika matumizi ya maarifa kutatua tatizo halisi,
“Ametoa mchango mkubwa na wa kipekee katika kutetea haki za binadamu,” amesema.
Amesema akiwa Rais wa Benki ya AfDB, Dkt. Akinwumi amekuwa kiungo kikuu katika kuleta misaada ya benki hiyo katika maendeleo ya Tanzania.
“Wakati wa uongozi wake benki ilipitisha mkakati wake wa kuchangia maendeleo ya Tanzania ambao unalenga kujenga uchumi imara na unaostahimili misukosuko, kuboresha maisha ya watanzania na kuendeleza ushirukiano wa kikanda.
“Mkakati huo una maeneo mawili ya kipaumbele. Kipaumbele cha kwanza Miundombinu endelevu kwa ajili ya uchumi shindani, na cha pili mazingira bora ya sekta binafsi kwa ajili ya ajira,” amesema.
Amesema benki hiyo imeunga mkono miradi mbalimbali ikiwemo uendelezaji wa miundombinu ya kisasa ya usafiri kwa njia mbalimbali kama barabara, usafiri wa majini, reli na viwanja vya ndege.
Ametolea mfano kwamba benki hiyo ilishiriki kugharamia mradi wa barabara ya mzunguko ya nje ya Jiji la Dodoma yenye urefu wa kilomita 112.3, ambapo gharama ya mradi ilikuwa dola za Kimarekani milioni 214.69.
“Benki ilichangua asilimia 64 ya fedha hizo, jambo lililosaidia kuboresha miunganisho na shughuli za kiuchumi makao makuu ya nchi,” amesena.
Pia benki hiyo imeunga mkono mradi wa reli ya kisasa ( SGR),  wa Tanzania ambao ni miongoni mwa njia za usafiri wa haraka na za kuaminika, zenye malengo ya kuiunganisha nchi na majirani kama Jamhuri ya Kidemokrasua ya Kongo ( DRC), Burundi na Rwanda, hivyo kuimarisha utangamano wa kikanda.
Vile vile AfDB inashirikiana na serikali ya Tanzania katika kugharamia ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato jijini Dodoma.
Pia amesema Benki hiyo imekuwa mstari wa mbele katika kusaidia nageuzi ya kilimo, hatua iliyowezesga Tanzania kufikia asilimia 128 ya utoshelevu wa chakula.

You Might Also Like

Rais Samia akisikiliza jambo

Japan Yatoa Bilioni 27 Kuboresha Sekta Ya Afya

Chagueni Viongozi Wanaofaa-Biteko

Kituo Cha Mkutano Cha Kimataifa Mlima Kilimanjaro Kuileta Dunia Tanzania

Theluthi mbili ya nguvu kazi ya taifa ipo kwenye kilimo

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Dkt. Adesina Wa AfD Avutiwa Na Mwenendo Uchumi Wa Tanzania
Next Article Miradi Dodoma Yamkuna Rais Samia
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
PURA Yajipanga Gesi Asilia Itumike Kwenye Magari
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?