Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: CHUO Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), kimemtunuku Shahada ya Heshima ya Sayansi, Rais na Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Dkt. Akinwumi Ayeodeji Adesina leo Juni 13, 2025.
Makamu Mkuu Mstaafu UDSM, Profesa Rwekaza Mukandala ameeleza hayo katika mahafali ya 55 ya chuo hicho Duru ya Kwanza Yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City.

Profesa Mukandala amesema, kwa mujibu wa kanuni za tuzo ya shahada za Heshima za UDSM za mwaka 2014,
” Shahada ya heshima inaweza kutolewa kwa mtu mwenye angalau shahada ya kwanza ambaye, amechangia kipekee katika kuendeleza tasnia ya ujifunzaji,
” Ametoa mchango mkubwa na wa kipekee katika matumizi ya maarifa kutatua tatizo halisi,
“Ametoa mchango mkubwa na wa kipekee katika kutetea haki za binadamu,” amesema.
Amesema akiwa Rais wa Benki ya AfDB, Dkt. Akinwumi amekuwa kiungo kikuu katika kuleta misaada ya benki hiyo katika maendeleo ya Tanzania.

“Wakati wa uongozi wake benki ilipitisha mkakati wake wa kuchangia maendeleo ya Tanzania ambao unalenga kujenga uchumi imara na unaostahimili misukosuko, kuboresha maisha ya watanzania na kuendeleza ushirukiano wa kikanda.
“Mkakati huo una maeneo mawili ya kipaumbele. Kipaumbele cha kwanza Miundombinu endelevu kwa ajili ya uchumi shindani, na cha pili mazingira bora ya sekta binafsi kwa ajili ya ajira,” amesema.
Amesema benki hiyo imeunga mkono miradi mbalimbali ikiwemo uendelezaji wa miundombinu ya kisasa ya usafiri kwa njia mbalimbali kama barabara, usafiri wa majini, reli na viwanja vya ndege.
Ametolea mfano kwamba benki hiyo ilishiriki kugharamia mradi wa barabara ya mzunguko ya nje ya Jiji la Dodoma yenye urefu wa kilomita 112.3, ambapo gharama ya mradi ilikuwa dola za Kimarekani milioni 214.69.

“Benki ilichangua asilimia 64 ya fedha hizo, jambo lililosaidia kuboresha miunganisho na shughuli za kiuchumi makao makuu ya nchi,” amesena.
Pia benki hiyo imeunga mkono mradi wa reli ya kisasa ( SGR), wa Tanzania ambao ni miongoni mwa njia za usafiri wa haraka na za kuaminika, zenye malengo ya kuiunganisha nchi na majirani kama Jamhuri ya Kidemokrasua ya Kongo ( DRC), Burundi na Rwanda, hivyo kuimarisha utangamano wa kikanda.
Vile vile AfDB inashirikiana na serikali ya Tanzania katika kugharamia ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato jijini Dodoma.
Pia amesema Benki hiyo imekuwa mstari wa mbele katika kusaidia nageuzi ya kilimo, hatua iliyowezesga Tanzania kufikia asilimia 128 ya utoshelevu wa chakula.