MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: UDSM Yaipaisha Lugha Ya Kichina kwa Kuanzisha Digrii Ya Awali Ya Kichina, Kiingereza
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > UDSM Yaipaisha Lugha Ya Kichina kwa Kuanzisha Digrii Ya Awali Ya Kichina, Kiingereza
Habari

UDSM Yaipaisha Lugha Ya Kichina kwa Kuanzisha Digrii Ya Awali Ya Kichina, Kiingereza

Author
By Author
Share
3 Min Read

Digrii Nyingine Ya Kichina, Kiswahili Kuanzishwa

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: CHUO Kikuu Dar es Salaam (UDSM), kimeanzisha Digrii ya awali ya Elimu katika lugha ya Kichina na Kiingereza.

Aidha kipo katika mpango wa kuanzisha digrii nyingine itakayojikita katika masomo ya Kichina na Kiswahili.

Mkurugenzi wa Shahada ya Uzamili UDSM, Rose Upour amesema hayo alipomwakilisha Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma chuoni hapo, Profesa Bonaventure Rutinwa kwenye Mashindano ya Awali ya Lugha ya Kichina Taasisi ya Confucios.

Upour amesema chuo hicho kinatoa stashahada katika lugha ya Kichina pamoja na kozi mbalimbali za muda mfupi katika lugha ya kichina.

“Hapa nchini wazungumzaji wa lugha ya kichina ni zaidi ya 200,000 na kuna makampuni zaidi ya 500 yanayoendesha shughuli zake hapa nchini.

” Hivyo kujifunza kichina kutakuwa na manufaa makubwa kwa wajifunzaji na kufanya hivyokutawaongezea fursa ya ajira na hatimaye kupata kipato,” amesema.

Naye Mkurugenzi Mwenza wa Taasisi hiyo ya kichina, Dkt. Musa Hans amesema tangu kuanzishwa kwa mashindano hayo mwaka 2002, yamekuwa yakifanyika kila mwaka kwa awamu mbili.

“Awamu ya kwanza ni mashindano ya awali katika nchi mbalimbali duniani, awamu ya pili ni mashindano ya bara na fainali ya dunia ambayo hufanyika China,” amesema.

Amesema zaidi ya wanafunzi milioni 1.5 kutoka zaidi ya nchi 150 wameshiriki mashindano hayo ya awali na kuonesha mafanikio katika kujifunza kichina.

Amesema zaidi ya washiriki 5000 wamekwenda China kushiriki katika mashindano ya mabara na fainali ya dunia.

” Lengo la mashindano haya ni kuwapa jukwaa vijana kutoka sehemu mbalimbali duniani kuonesha ujuzi wao wa lugha ya kichina, kukuza mawasiliano baina yao, na kuwahamasisha kukifunza lugha ya kichina,” amesema.

Dkt. Hans amesema kwenye mashindano hayo walishiriki wanafunzi 16 waliotoka UDSM, Chuo cha Uhusiano wa Kidiplomasia, na Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.

Washindi watashiriki katika mashindano yatakayofanyika Mei, chuoni hapo.

Naye Mwambata wa Masuala ya Utamaduni kutoka Ubalozi wa China nchini Tanzania, Xu Yongilang amesema zaidi ya nchi 180 duniani zinafundisha lugha ya Kichina.

Amesema karibu watu milioni 200 nje ya China wanajifunza lugha hiyo.

“Tunatarajia wanafunzi waendelee kujifunza kwa bidii, walimu wazidi kung’ara na jamii iendelee kuiunga mkono Taasisi ya Confucius,” amesema.

Mwanafunzi anayejifunza lugha ya kichina UDSM, Neema Joines amesema ameanza kujifunza tokea akiwa kidato cha kwanza, na kwamba lugha hiyo inawawezesha kupata kazi, marafiki hivyo wazazi wasiwazuie watoto wao kusoma lugha hiyo.

Naye mwanafunzi mwingine anayesoma lugha hiyo chuoni hapo, Aisha Yahya amesema kuzungumza lugha ya kichina na kumpa fursa ya kushiriki mashindano hayo kunamwongezea ujasiri.

You Might Also Like

Tanzania Mwenyeji Mkutano wa Mafuta na Gesi, 2025

Thamani ya Fedha Ionekane Kwenye Utekelezaji wa Miradi-Nyamoga

FAJ Yataka Wahamiaji Wa Kazi Wa Afrka, Wanaokwenda Maeneo Mengine Walindwe

Wenye Ulemavu Wa Ngozi Wakumbukwa Kupitia FDH, Wapewa Msaada Wa Milioni 20

Afrika ijadili changamoto sekta ya utalii – UN

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Chalamila: Ujenzi Daraja La Jangwani Waanza
Next Article Ridhiwani: Maandalizi Mei Mosi  Yafikia Asilimia 88
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?