MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: UDSM Yaipaisha Lugha Ya Kichina kwa Kuanzisha Digrii Ya Awali Ya Kichina, Kiingereza
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > UDSM Yaipaisha Lugha Ya Kichina kwa Kuanzisha Digrii Ya Awali Ya Kichina, Kiingereza
Habari

UDSM Yaipaisha Lugha Ya Kichina kwa Kuanzisha Digrii Ya Awali Ya Kichina, Kiingereza

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read

Digrii Nyingine Ya Kichina, Kiswahili Kuanzishwa

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: CHUO Kikuu Dar es Salaam (UDSM), kimeanzisha Digrii ya awali ya Elimu katika lugha ya Kichina na Kiingereza.

Aidha kipo katika mpango wa kuanzisha digrii nyingine itakayojikita katika masomo ya Kichina na Kiswahili.

Mkurugenzi wa Shahada ya Uzamili UDSM, Rose Upour amesema hayo alipomwakilisha Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma chuoni hapo, Profesa Bonaventure Rutinwa kwenye Mashindano ya Awali ya Lugha ya Kichina Taasisi ya Confucios.

Upour amesema chuo hicho kinatoa stashahada katika lugha ya Kichina pamoja na kozi mbalimbali za muda mfupi katika lugha ya kichina.

“Hapa nchini wazungumzaji wa lugha ya kichina ni zaidi ya 200,000 na kuna makampuni zaidi ya 500 yanayoendesha shughuli zake hapa nchini.

” Hivyo kujifunza kichina kutakuwa na manufaa makubwa kwa wajifunzaji na kufanya hivyokutawaongezea fursa ya ajira na hatimaye kupata kipato,” amesema.

Naye Mkurugenzi Mwenza wa Taasisi hiyo ya kichina, Dkt. Musa Hans amesema tangu kuanzishwa kwa mashindano hayo mwaka 2002, yamekuwa yakifanyika kila mwaka kwa awamu mbili.

“Awamu ya kwanza ni mashindano ya awali katika nchi mbalimbali duniani, awamu ya pili ni mashindano ya bara na fainali ya dunia ambayo hufanyika China,” amesema.

Amesema zaidi ya wanafunzi milioni 1.5 kutoka zaidi ya nchi 150 wameshiriki mashindano hayo ya awali na kuonesha mafanikio katika kujifunza kichina.

Amesema zaidi ya washiriki 5000 wamekwenda China kushiriki katika mashindano ya mabara na fainali ya dunia.

” Lengo la mashindano haya ni kuwapa jukwaa vijana kutoka sehemu mbalimbali duniani kuonesha ujuzi wao wa lugha ya kichina, kukuza mawasiliano baina yao, na kuwahamasisha kukifunza lugha ya kichina,” amesema.

Dkt. Hans amesema kwenye mashindano hayo walishiriki wanafunzi 16 waliotoka UDSM, Chuo cha Uhusiano wa Kidiplomasia, na Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.

Washindi watashiriki katika mashindano yatakayofanyika Mei, chuoni hapo.

Naye Mwambata wa Masuala ya Utamaduni kutoka Ubalozi wa China nchini Tanzania, Xu Yongilang amesema zaidi ya nchi 180 duniani zinafundisha lugha ya Kichina.

Amesema karibu watu milioni 200 nje ya China wanajifunza lugha hiyo.

“Tunatarajia wanafunzi waendelee kujifunza kwa bidii, walimu wazidi kung’ara na jamii iendelee kuiunga mkono Taasisi ya Confucius,” amesema.

Mwanafunzi anayejifunza lugha ya kichina UDSM, Neema Joines amesema ameanza kujifunza tokea akiwa kidato cha kwanza, na kwamba lugha hiyo inawawezesha kupata kazi, marafiki hivyo wazazi wasiwazuie watoto wao kusoma lugha hiyo.

Naye mwanafunzi mwingine anayesoma lugha hiyo chuoni hapo, Aisha Yahya amesema kuzungumza lugha ya kichina na kumpa fursa ya kushiriki mashindano hayo kunamwongezea ujasiri.

You Might Also Like

TARI Kihinga Yainua Kilimo Cha Michikichi Kigoma

Uchaguzi Serikali Ya Mitaa kufanyika Novemba 27

Majaliwa Amwakilisha Rais Samia Kwenye Kilele Cha Siku Ya Utumishi Wa Umma

VETA Yawawezesha Vijana Wenye Mahitaji Maalum Kung’ara Katika Fani za Ufundi

Kamati Ya Bunge Yakunwa Na TEA 

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Chalamila: Ujenzi Daraja La Jangwani Waanza
Next Article Ridhiwani: Maandalizi Mei Mosi  Yafikia Asilimia 88
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Vitabu Vya Sauti Kuvutia Vijana, Serikali Yapongeza Ubunifu Wa Mkuki Na Nyota
Habari November 22, 2025
Ubora Wa E & D Vision Publishing Wamkuna Waziri Kabudi Maonyesho Ya Vitabu Dar
Habari November 22, 2025
Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 
Habari November 22, 2025
Kwagila Awataka Wasimamizi Wa Elimu TAMISEMI Kuwajibika Kikamilifu
Habari November 21, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?