MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: UDSM Yaanzisha Mkakati Kuokoa Nyuki Wadogo
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > UDSM Yaanzisha Mkakati Kuokoa Nyuki Wadogo
Habari

UDSM Yaanzisha Mkakati Kuokoa Nyuki Wadogo

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA:  CHUO Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kimetafiti suluhisho la kielimu na utafiti kuhakikisha nyuki wadogo hawapotei kwa kuwa moja ya kazi wanayoifanya ni uchavushaji wa mimea mbalimbali.
Mwanasayansi wa nyuki kutoka UDSM, Gabriel Mwambogela amesema hayo alipozungumza na Mwandishi wa Habari kuhusu suluhisho hilo.
Amesema njia mojawapo ya kuhakikisha nyuki hao wadogo wanaendelea kuwepo ni kubaini maeneo wanapopatikana na kutoa elimu sahihi kwa jamii kuhusu umuhimu wao.
Amesema nyuki wadogo hawa wana uwezo wa kuchavusha maua yenye saizi tofauti tofauti, jambo linalosaidia  katika kuongeza wingi na utofauti wa mazao.
“Aidha, asali inayotokana na nyuki hawa ina virutubisho vingi na hutumika kama tiba katika maeneo mbalimbali.
“Katika baadhi ya maeneo nchini, jamii imekuwa ikiwachukulia nyuki hawa kama wa laana kwa imani kuwa asali yao husababisha kuharisha au kutoa mimba,” amesema.
Ameongeza kuwa,  baada ya kupewa elimu, mitazamo hiyo imebadilika na jamii sasa imeanza kuwaacha nyuki hao waendelee kuchangia kwenye mfumo wa ikolojia.
Amesena Ulimwenguni kuna aina 605 za nyuki wadogo, huku Afrika Bara ikiwa na aina 33. Tanzania ina jumla ya aina 12, ambazo zote zina mchango mkubwa katika uchavushaji wa mimea.
Ripoti ya utafiti huo imeonyesha kuwa maeneo ya ukanda wa mashariki mwa Tanzania yana idadi kubwa ya nyuki wadogo.
Amesema kupitia elimu na uhamasishaji, watafiti wa UDSM wanasisitiza umuhimu wa kuwalinda wadudu hao kwa mustakabali wa usalama wa chakula na mazingira.

You Might Also Like

Maofisa Tarafa na Watendaji wa Kata Waaswa kuwa wabunifu

Wizara Ya Kilimo Yajipanga Vema Maonesho ya Kimataifa Ya Biashara

Kutoka 1975 hadi 2025: TUCTA Yatimiza Ndoto Ujenzi Jengo La Biashara Arusha

Ubunifu Na Kufanya Tafiti Kwawezesha UDOM Kupokea Tuzo

Waziri Mkuu Majaliwa Akoshwa Na Tafiti Ya Mhitimu OUT

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article UDSM Imekuja Na App Inayounganisha Wakulima na Watoa Huduma za Kilimo kwa Haraka
Next Article VETA Yatahadharisha Changamoto ya Kuzidisha Uchanganyaji wa Chakula Cha Mifugo
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Waziri Mkuu Majaliwa Akabidhi Tuzo kwa BoT Geita
Habari September 22, 2025
BoT Yarahisisha Uuzaji wa Dhahabu kwa Wachimbaji, Yatoa Punguzo La Mrabaha
Habari September 22, 2025
Waziri Mkuu Apongeza Huduma Kidijitali za NSSF, Maonesho Ya Madini Geita
Habari September 22, 2025
Mkuu Wa Mkoa Shinyanga Asifu Kazi Ya Bodi Bima Ya Amana
Habari September 22, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?