MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Tumeanza Kufanyia Kazi Maelekezo Ya Rais Samia – Bashungwa
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Tumeanza Kufanyia Kazi Maelekezo Ya Rais Samia – Bashungwa
Habari

Tumeanza Kufanyia Kazi Maelekezo Ya Rais Samia – Bashungwa

Author
By Author
Share
2 Min Read
Awajulia Hali Majeruhi 16, Waliopoteza Maisha 11
Na Lucy Ngowi
KAGERA: WIZARA ya Mambo ya Ndani ya Nchi, imeanza kufanyia kazi maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa kufanya marekebisho ya kuwa na mfumo wa leseni za udereva ili kuwapunguzia alama madereva wanaofanya makosa yenye kuhatarisha usalama barabarani.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amesema hayo baada ya kufika eneo la Kabukome katika Kata ya Nyarubango wilayani Biharamulo mkoani Kagera, kulipotokea ajali ya basi la abiria lenye namba za usajili T857 DHW.
Pia aliwajulia hali majeruhi wanaoendelea kupewa matibabu katika Hospitali Teule ya Biharamulo, Disemba 21, 2024.
Bashungwa amesema maelekezo hayo ya Rais Samia ni pamoja na kuwafungia leseni madereva wanaofanya makosa yanayohatarisha usalama barabarani.
Basi hilo lililopata ajali lilikuwa linafanya safari kutoka Kigoma kwenda Bukoba wakati liliposimama kushusha abiria ambaye alipitilizwa kwenye kituo, lilishindwa kuondoka na kurudi nyuma kisha kuacha njia na kupinduka.
Ajali hiyo imesababisha vifo vya abiria 11 na majeruhi 16 ambapo majeruhi wanaendelea na matibabu katika  Hospitali Teule ya Biharamulo mkoani Kagera.
Bashungwa ametoa pole kwa  familia, ndugu na jamaa wote walioguswa na ajali hiyo na kutoa wito kwa watanzania kuendelea kuwaombea majeruhi wapone haraka.
Kwa Upande wake, Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo majeruhi waliko, Gresmus Sebuyoya amesema majeruhi 26 wameruhusiwa na wengine 16 wanaendelea na matibabu na ungalizi wa karibu.
“Tumebaki na watoto wanne ambao wanaendelea vizuri, wanaume tunao sita, vifo tulikuwa navyo 11, wanawake watano, wanaume wanne  na watoto wawili” amesema.

You Might Also Like

Matokeo Ya Usaili TRA Kutangazwa April 25,2025

Muswada Wa Marekebisho Ya Sheria Za Kazi 2024 Wapitishwa

TAKUKURU, Manispaa Ubungo Yawafikia Waendesha Bajaji, Bodaboda

Muswada kuja wa Watumishi Wanaofanya Kazi Eneo Zaidi ya Moja Kuanza kuchangiwa na Waajiri Wote

TRA: Serikali imemgusa mkulima kupitia mabadiliko ya sheria

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TARI Yawafikia Wakulima Kilosa, Kilimo Shadidi Cha Mpunga
Next Article Mkurugezi Mkuu LATRA, Kamanda Ng’anzi Wafanya Ukaguzi Wa Kushtukiza Stendi Ya Magufuli
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Utafiti Wa Nguvu Kazi, Mapato Ya Kaya Kutoa Taswira Mpya Ya Maendeleo
Habari July 15, 2025
Majaliwa Aituza UDSM kwa Kuongoza Eneo La Elimu, Utafiti, Ubunifu Sabasaba 2025
Habari July 14, 2025
Nyanya Cheri na Ngogwe Chungu Zarejea 
Habari July 13, 2025
NFRA Yawaalika Wadau Kununua Nafaka kwa Masoko ya Ndani na Nje
Habari July 13, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?