Na Lucy Lyatuu
TUME ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) imetoa nyongeza ya ya muda wa miezi mitatu kuanzia Januari 8,2026 hadi April 8,2026 kwa taasisi zote za umma na binafsi zinazokusanya na kuchakata taarifa binafsi ambazo bado hazijakamilisha usajili ziwe zimejisajili.
Mkurugenzi Mkuu wa Tumehiyo, Dkt Emmanuel Mkilia amesema hay oleo Dar es Salaam wakati Tume hiyo ikitoa taarifa ya utekelezaji wa maagizo ya serikali kuhusu uzingatiaji wa sheria ya ulinzi wa taarifa binafsi sura ya 44.
Amesema katika kipindi hicho taasisi za umma na binafsi zinatakiwa kuhakikisha zinakamilisha usajili kwa hiari ndani ya kipindi hicho.

Amesema Tume inasisitiza kuwa katika kipindi hicho cha nyongeza hakimaanishi kusitishwa kwa utekelezaji wa Sheria, bali ni dirisha la mwisho la muda wa hiari kabla ya hatua kali kuchukuliwa kwa taasisi ambazo zitakuwa hazijakamilisha usajili kwa mujibu wa Sheria.
“PDPC inapenda kuujulisha umma kuwa, baada ya dirisha la mwisho la muda wa hiari kuisha itaanza mara moja ukaguzi wa uzingatiaji wa Sheria kwa taasisi za umma na binafsizinazokusanya na kuchakata taarifa binafsi,” amesema.

Amesema ukaguzi huo utahusisha kubaini taasisi za umma na binafsi zinazokukusanya, kuhifadhi,kuchakata, na kusafirisha taarifa binafsi nje ya nchi bila kuzingatia matakwa ya Sheria va Ulinzi wa Taarifa Binafsi, Sura ya 44 na Kanuni zake.
“PDPC inatoa taarifa kwamba hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya mtu yeyote, taasisi au kampuni itakayobainika kukiuka Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, Sura ya 44 katika utekelezaji wa shughuli zake,” amesema na kuongeza kuwa hadi sasa ni taasisi 10,000 ndizo zilizojisajili.
Amesema kwa mujibu wa Sheria iliyotajwa, hatua hizo ni pamoja na kutozwa faini, kifungo, au vyote kwa pamoja, pamoja na kulipa fidia kwa wote watakaoathirika kutokana na ukiukwaji wa matakwa ya Sheria.
Vilevile,amesema mtu au taasisi yoyote itakayobainika kuvunja faragha au kutumia taarifa binafsi bila kujali hadhi au ukubwa wake.
“PDPC inatoa wito kwa taasisi zote za umma na ridhaa ya mhusika wa taarifa hizo, au kinyume na utaratibu uliowekwa kisheria, atawajibishwa binafsi kuchukua hatua za haraka kujisajili, kuimarisha mifumo yao ya ulinzi wa taarifa binafsi, na kuhakikisha uzingatiaji kamili wa Sheria ikiwa ni wajibu wao kwa Serikali wa kulinda haki za kikatiba za wananchi, hususan haki ya faragha katika uchumi wa kidijitali,” amesema.

Katika hatua nyingine Tume imesema katika kuimarisha uelewa wa umma na wadau kuhusu haki na wajibu unaotokana
Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) itaungana na mataifa mengine duniani kuadhimisha Wiki ya Faragha na Ulinzi wa Taarifa Binafsi.
Amesema maadhimisho hayo hufanyika kimataifa kwa lengo la kukuza uelewa na mshikamano wa dunia katika kulinda haki ya faragha.

Dkt Mkilia amesema kwa mwaka 2026, maadhimisho hayo yatafanyika kuanzia Januari 26, 2026 hadi Januari 30,2026 huku kilele chake kikiwa ni Januari 28 , 2026.

