MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Tume ya Kurekebisha Sheria Yatoa Onyo Kali kwa Wanaovunja Sheria za Umwagiliaji
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Tume ya Kurekebisha Sheria Yatoa Onyo Kali kwa Wanaovunja Sheria za Umwagiliaji
Habari

Tume ya Kurekebisha Sheria Yatoa Onyo Kali kwa Wanaovunja Sheria za Umwagiliaji

Author
By Author
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

DODOMA: TUME ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT) imewataka wananchi na vyama vya umwagiliaji kufuata masharti ya kisheria katika matumizi ya rasilimali za umwagiliaji, kwa kuwa kuna makatazo yaliyoainishwa kisheria yanayolenga kulinda mazingira na kuongeza tija katika kilimo nchini.

Wakili wa Serikali kutoka Tume hiyo, Baraka Chipamba, amesema hayo katika maonesho ya wakulima ya Kitaifa yanayoendelea mkoani Dodoma,

Amesema Sheria ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Na. 4 ya mwaka 2013, iliyotokana na Sera ya Umwagiliaji ya mwaka 2010, imeweka masharti madhubuti kwa ajili ya kusimamia shughuli za umwagiliaji nchini.

“Sheria hii imeweka makatazo muhimu kama uvamizi wa maeneo ya umwagiliaji, matumizi ya kemikali katika vyanzo vya umwagiliaji, uvuvi bila kibali katika maeneo hayo, na uchepushaji wa maji kinyume na utaratibu,” amesema Chipamba.

Amesema makatazo hayo yanahitajika kuzingatiwa kwa sababu uvunjaji wake unaathiri moja kwa moja tija ya kilimo na uhifadhi wa mazingira.

Aidha, ameviomba vyama vya umwagiliaji ambavyo vina nafasi kubwa katika utekelezaji wa sheria hiyo, kusaidia kutoa elimu kwa wanachama wao na kuhakikisha taratibu zinafuatwa.

“Kuna watu wanajitokeza na kuingilia skimu za umwagiliaji bila kuwa sehemu ya mradi, wanachepusha maji au wanafanya uvuvi bila kibali hii ni kinyume cha sheria,” amesema.

Kwa upande wake, Wakili wa Serikali kutoka Tume hiyo, Vicky Mbunde, amesema jukumu kuu la Tume ya Kurekebisha Sheria ni kufanya mapitio ya sheria zilizopo ili kuhakikisha zinaendana na wakati na mazingira ya sasa, pamoja na kutoa elimu ya sheria kwa umma.

Amesema Tume hufanya tafiti za kisheria ili kubaini kama sheria fulani bado inafaa kwa mazingira ya sasa au ina upungufu unaohitaji kurekebishwa. Kazi hiyo hufanyika kwa kushirikisha wananchi moja kwa moja.

“Sisi hatupendekezi sheria kutoka kichwani, tunashirikiana na wananchi. Tunataka kusikia wanasema nini kuhusu sheria zilizopo – ndipo tunapata maoni halisi ya kile kinachohitaji kuboreshwa,” alisema Mbunde.

Pia alieleza kuwa Tume hushiriki kwenye maonyesho mbalimbali ya kitaifa ili kuwafikia wananchi na kuwaelimisha juu ya mchakato wa maboresho ya sheria na namna wanavyoweza kushiriki kikamilifu katika mabadiliko hayo.

 

 

You Might Also Like

Mawaziri Tanzania Profesa Mkenda, Silaa Mkutanoni Rwanda

Serikali Inaboresha Miundombinu Ya Umeme Kibiti Kuondoa Changamoto Za Umeme – Kapinga

Nzega Kujenga Barabara za Lami, Soko la Kisasa ili Kukuza Uchumi

Waajiri Wathamini Taaluma Ya Uandishi Wa Habari – Dkt. Mkoko

VETA Yatahadharisha Changamoto ya Kuzidisha Uchanganyaji wa Chakula Cha Mifugo

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article DC Atoa Wito kwa Tume ya Kurekebisha Sheria Kuzingatia Sheria Ndogondogo za Halmashauri
Next Article Zimbabwe Yakabidhi Uenyekiti Kwa Madagascar
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Waziri Mkuu Majaliwa Akabidhi Tuzo kwa BoT Geita
Habari September 22, 2025
BoT Yarahisisha Uuzaji wa Dhahabu kwa Wachimbaji, Yatoa Punguzo La Mrabaha
Habari September 22, 2025
Waziri Mkuu Apongeza Huduma Kidijitali za NSSF, Maonesho Ya Madini Geita
Habari September 22, 2025
Mkuu Wa Mkoa Shinyanga Asifu Kazi Ya Bodi Bima Ya Amana
Habari September 22, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?