MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Toleo La Sheria Zilizotafsiriwa Kwa Kiswahili Kutoka Agosti
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Toleo La Sheria Zilizotafsiriwa Kwa Kiswahili Kutoka Agosti
Habari

Toleo La Sheria Zilizotafsiriwa Kwa Kiswahili Kutoka Agosti

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: TOLEO la Sheria ambazo zimetafsiriwa kwa lugha ya Kiswahili zitaanza kutoka Agosti mwaka huu 2025.

Mwandishi Mkuu wa Sheria, Onorius Njole, amesema hayo katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara maarufu kama Sabasaba yanayoendelea mkoani Dar es Salaam.

Njole amesema hatua hiyo ni utekelezaji wa agizo la Rais Samia Suluhu Hassan, ambaye aliagiza sheria za nchi kutafsiriwa ili kuwawezesha wananchi wa makundi yote kuzielewa kwa urahisi.

“Pamoja na hatua kubwa ya urekebu wa sheria iliyofanyika, Rais aliagiza pia kukamilishwa kwa zoezi la kutafsiri sheria kwa Kiswahili. Hii ni kwa sababu wananchi wengi hawana uelewa wa lugha ya kisheria ya Kiingereza,” amesema.

Kwa mujibu wa Njole, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imefanya kazi kubwa ya kurekebisha sheria zilizopo ili ziendane na mazingira ya sasa ya kijamii, kiuchumi na kiteknolojia, ikiwa ni pamoja na kuanza mikakati ya kutunga sheria mpya zitakazodhibiti matumizi ya teknolojia ya Akili Bandia.

“Tunaandaa mfumo maalum wa kisheria wa kusimamia matumizi ya Akili Mnemba (AI), na utakapokamilika, Miswada ya sheria itapelekwa bungeni kwa ajili ya kuundwa sheria kamili,” amesema.

Kwa upande wake, Mwandishi Mkuu Msaidizi wa Sheria, Rahema Katuga amesema marekebisho ya sheria yaliyokamilika hivi karibuni yameanza kutumika rasmi tangu Julai mosi mwaka huu, 2025, na sheria za zamani ambazo hazijafanyiwa urekebu hazitatumika tena.

“Kuanzia sasa, mtu yeyote anayetaja kifungu cha sheria katika mazingira ya kimahakama au kiofisi, anatakiwa kutumia marejeo ya sheria mpya zilizorekebishwa,” amesema.

Hatua hii inaelezwa kuwa sehemu ya jitihada za serikali za kukuza ushirikishwaji wa wananchi katika masuala ya kisheria, kuimarisha utawala wa sheria na kukuza matumizi ya Kiswahili kama lugha ya kisheria na ya taifa.

You Might Also Like

Usekelege: Kati ya Migogoro Tunayoipokea Ipo ya Wafanyakazi Majumbani

Serikali Yaendesha Warsha Kujenga Ushirikiano Na washirika Wa Maendeleo  

TEITI Yashiriki Maonesho ya Nane ya Uwekezaji Sekta ya Madini Geita

Kamishna TRA Atua Kwa Malasusa Kushirikiana Elimu Kwa Mlipa Kodi

Dodoma Yazizima Wakati Samia, Nchimbi  Wakichukua Fomu Ya Urais

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Waendelezaji Majengo 103 Kesi Ziko Mahakamani, -AQRB
Next Article ‘Jichunge’ Programu Ya Simu Yenye Mafanikio Katika Kuboresha Matumizi Ya Dawa Kinga Dhidi Ya VVU
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Ziwa Ngozi Lavuta Mamia Sabasaba, Wageni Washangazwa Na Ramani Ya Afrika Juu Ya Mlima
Habari July 9, 2026
Shirika La Uzalishaji Mali La Polisi Kujenga Vituo Vya Ukaguzi Wa Vyombo Vya Moto
Habari July 9, 2026
Watumishi 7881 Watakaostaafu 2026/27 Watambuliwa Kupitia Kampeni Ya Tunalipa Jana-PSSF
Uncategorized July 8, 2026
Katambi Apongeza Zimamoto Kwa Uwekezaji Wa Vifaa Vya Kisasa
Uncategorized July 7, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?