MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TEA, UNICEF na Canada waendeleza mageuzi ya elimu Sikonge
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TEA, UNICEF na Canada waendeleza mageuzi ya elimu Sikonge
Habari

TEA, UNICEF na Canada waendeleza mageuzi ya elimu Sikonge

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Atugonza David akiwa na Mkuu wa Shule ya Sekondari Pangale Mwalimu Sengi Msaru wakati wa kukagua mradi wa ukarabati wa maabara tatu za Sayansi zilizofadhiliwa na UNICEF, CANADA kwa usimamizi wa TEA. 
Na Mwandishi Wetu
TABORA: MAMLAKA ya Elimu Tanzania (TEA), kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Serikali ya Canada, wamekamilisha utekelezaji wa miradi 10 ya miundombinu ya elimu katika shule za msingi na sekondari wilayani Sikonge, mkoani Tabora.
Miradi hiyo, yenye thamani ya takriban Sh. Milioni 284, imetekelezwa katika shule sita kwa lengo la kuboresha mazingira ya ujifunzaji na kufundishi,  Kazi zilizofanyika ni pamoja na ujenzi na ukarabati wa maabara, vyumba vya madarasa na matundu ya vyoo.
Habari Picha 9791
Muonekano wa ndani wa maabara ya Sayansi shule ya Sekondari Pangale baada ya ukarabati uliofadhiliwa na UNICEF, Serikali ya CANADA na kuratibiwa na TEA 
Akizungumza katika ziara ya ukaguzi wa miradi hiyo, Ofisa Miradi kutoka TEA, Atugonza David, amesema ujenzi umekamilika na miundombinu hiyo iko tayari kutumika.
“Tumemaliza maabara nane za sayansi katika shule nne, tumejenga matundu 10 ya vyoo katika shule moja na kukamilisha vyumba vinne vya madarasa katika shule nyingine,” amesema.
Habari Picha 9792
Mkuu wa Shule ya Sekondari Kamagi,  Mwalinu Merina Mbiha (kulia) akitoa maelezo kwa Atugonza David Ofisa Miradi kutoka TEA, alipofanya ziara ya kukagua ukarabati wa maabara mbili za Sayansi shuleni hapo 
Mkuu wa Shule ya Sekondari Ngulu, Mwalimu Israel Mwambikwa, amesema shule yake imenufaika na ujenzi wa maabara mbili, hatua iliyoongeza hamasa ya wanafunzi kujifunza masomo ya sayansi, hasa kwa wasichana.
“Tuna jumla ya wanafunzi 666, nusu yao ni wasichana. Tangu kukamilika kwa maabara, wasichana wameanza kufanya vizuri zaidi kwenye masomo ya sayansi na idadi yao kwenye michepuo ya sayansi imeongezeka mara mbili,” amesema.
Habari Picha 9793
Baadhi ya walimu wa Shule ya Sekondari Kamagi wakiwa nje ya maabara ya Kemia iliyokarabatiwa na UNICEF pamoja na Serikali ya CANADA kwa uratibu wa TEA
Mpango huu ni sehemu ya makubaliano kati ya TEA na UNICEF yanayolenga kuboresha fursa za elimu kwa watoto wote wa Kitanzania, kwa kuhakikisha mazingira salama na jumuishi ya kujifunzia.
Habari Picha 9794

 

Ofisa Miradi kutoka TEA Atugonza David akiwa na Mwalimu Mkuu shule ya msingi Kiloleli Mwalimu Festo Ponela (katikati) pamoja na mjumbe wa kamati ya shule Bw. Nicholaus Mbanka wakikagua ujenzi wa matundu 10 ya vyoo yaliyofadhiliwa na UNICEF, Serikali ya CANADA na kuratibiwa na TEA 

You Might Also Like

NSSF Yajivunia Kasi Ya Ufanisi Na Mafanikio Miaka Minne Ya Rais Samia

Chalamila Akagua Miradi Jimbo La Kibamba Ubungo DSM

Uteuzi: Abubakar Mombo Ateuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa, Siwa amestaafu

Tanzania Yaibuka Kidedea Maonesho Zambia

Kingalame Aitaka Sekta Binafsi Kushirikiana na TBA Kukamilisha Mradi wa Makazi Geita

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Samia Aendeleza Kampeni Mwanza, Azungumza na Wananchi Misungwi
Next Article Wizara Ya Nishati Yaendelea Kutoa Elimu Kuhusu Matumizi Ya Nishati Safi Ya  Kupikia
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?