MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TARURA Yaimarisha Upitikaji Miundombinu Ya Barabara
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TARURA Yaimarisha Upitikaji Miundombinu Ya Barabara
Habari

TARURA Yaimarisha Upitikaji Miundombinu Ya Barabara

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: WAKALA wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) umeimarisha upitikaji wa miundombinu ya barabara za Wilaya wenye urefu wa kilometa zaidi ya 5000 kwa asilimia 55 kitaifa na asilimia 52 Kimkoa ambapo lengo ni kufikia asilimia 60 ifikapo mwezi Juni, 2025.

Akimwakilisha Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA), Ismail Mafita amesema hayo katika Semina ya Wanahabari wa Mitandao ya Kijamii Tanzania (JUMIKITA), iliyofanyika mkoani Dar es Salaam.

Amesema mafanikio hayo yanatokana na ongezeko kubwa la bajeti ya Wakala kutoka Sh. Bilioni 25 hadi Sh. Bilioni 52 sawa na ongezeko la asilimia 205.79 kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 hadi 2024/25.

Pia amesema mtandao wa barabara za lami katika kipindi hicho umeongezeka kutoka Kilomita 469.47 hadi 636.519, changarawe kutoka Kilomita 1,327.55 hadi 1,686.706 na barabara za udongo zimepungua kutoka Kilomita 3,260.75 hadi Kilomita 2,731.54 kwa mapato ya ndani.

“Katika ujenzi wa barabara zinazosimamiwa na Wakala tunaendelea kufanya majaribio kwa kutumia teknolojia mbalimbali ikiwemo ujenzi wa madaraja ya mawe pamoja na teknolojia nyingine katika kuboresha barabara tunazozisimamia.

“Matumizi ya teknolojia na malighafi za ujenzi zinazopatikana eneo la kazi ikiwemo mawe katika ujenzi na matengenezo ya madaraja, huongeza ufanisi, huokoa muda, hutunza mazingira kwa gharama nafuu,” amesema.

Amesema Matumizi ya teknolojia mbadala na malighafi zinazopatikana maeneo ya kazi kwa ajili ya ujenzi wa barabara na madaraja imeweza kupunguza gharama zaidi ya asilimia 50 ambapo TARURA imeweka kipaumbele cha kutumia malighafi zinazopatikana maeneo ya kazi ili kupata ufanisi wa gharama za ujenzi.

“Hata hivyo Wakala unaendelea na matumizi ya malighafi za ujenzi wa barabara zinazopatikana maeneo ya kazi na utafiti wa teknolojia mbadala za ECOROADS, Ecozyme, na GeoPolymer kwenye ujenzi wa barabara kwa lengo la kupata ufanisi wa gharama, kupunguza muda wa utekelezaji na kulinda mazingira,” amesema.

You Might Also Like

Kamati Ya Bunge Yahimiza Maslahi Ya Watumishi Wapya Yazingatiwe

Tanzania kujiimarisha zaidi kidiplomasia – Majaliwa

Tanzania, Comoro Zaongeza Ushirikiano wa Lugha

Bodi ya Maziwa Yatoa Mafunzo ya Ubora, Usalama wa Maziwa Katika Maonyesho ya Nane Nane

Thamani ya Fedha Ionekane Kwenye Utekelezaji wa Miradi-Nyamoga

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Dar Yaidhinishiwa Bil. 68 Ukarabati, Matengenezo Ya Barabara
Next Article Tanzania Kwa Mara Nyingine Mwenyeji Kongamano La eLearning Afrika
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Jamii Yatakiwa Kuzungumza Pamoja Kuhusu Maji, Masuala ya Jinsia
Habari March 16, 2026
Tume Ya Madini Yaweka Vipaumbele Kuwezesha Vijana Kushiriki Katika Uchimbaji Madini 
Habari March 16, 2026
Dawati  La Jinsia Unguja Latoa Ulinzi Na Usalama Kwa Watoto Wa Kike Kuwaepusha Na Ukatili
Habari March 16, 2026
Rais Samia Awekeza Mabilioni Kuboresha Sekta ya Uvuvi
Habari March 16, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?