MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Tari Ilonga yaboresha mbegu, mavuno yapanda hadi tani 3.8 kwa hekta
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Tari Ilonga yaboresha mbegu, mavuno yapanda hadi tani 3.8 kwa hekta
Habari

Tari Ilonga yaboresha mbegu, mavuno yapanda hadi tani 3.8 kwa hekta

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
MOROGORO: TAASISI ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI), imefanikiwa kuboresha aina mpya za mbegu za mtama, uwele na ulezi zenye uwezo wa kustahimili mashambulizi ya ndege na kiduha (gugu chawi), ambayo ni changamoto kubwa kwa wakulima.
Mtafiti Msaidizi kutoka TARI Ilonga iliyopo Kilosa mkoani Morogoro, David Macha amesema hayo katika Maonesho ya nanenane Kanda ya Mashariki, ambayo kilele chake kilikuwa ni jana Agosti nane, 2025.
Amesema kwa upande wa mtama, wamezalisha aina tatu mpya: aina mbili nyeupe ambazo ni fupi, na aina moja nyekundu ndefu. Aina ya ‘Macia’ ni mojawapo ya mbegu nyeupe, yenye urefu wa mita 1.5, ambayo inafanya vizuri kibiashara hasa katika utengenezaji wa bia, ikichukua nafasi ya shayiri na ngano zilizokuwa zikitumika awali.
Amesema mbegu hiyo ya macia hukaa shambani kwa siku 110 na hutoa mavuno ya tani 3.8 kwa hekta moja, ikilinganishwa na mbegu za zamani zilizokuwa zikitoa tani 2.
Ina masuke makubwa na uwezo mkubwa wa kustahimili mashambulizi ya ndege kutokana na ubunifu wa kiteknolojia unaofanya isiwe ya kuvutia kwa ndege.
Ametaja mbegu nyingine mpya kuwa ni TARI SOR 1 na TARI SOR 2, ambazo zimeundwa kuzuia mashambulizi ya kiduha, adui mkubwa wa mazao ya nafaka.
Kwa upande wa uwele, amesema  wamezalisha aina iitwayo Okoa, ambayo ina kiwango kikubwa cha madini ya zinki, muhimu kwa kinga na uzazi wa binadamu.
Amesema madini hayo ya Zinki ni nadra kupatikana kwa wingi kwenye nafaka nyingine, na hivyo aina hii ni suluhisho bora kwa lishe bora.
Katika zao la ulezi, amesema TARI Ilonga wamezalisha aina tatu, ikiwemo aina mpya iliyo na uwezo wa kutoa hadi kilo 1,200 kwa ekari moja, tofauti na aina ya P224  inayotoa kilo 700 na 415  inayotoa kilo 800.
Aina hiyo mpya imeboreshwa pia kukabiliana na ugonjwa wa ‘blast’ unaoshambulia masuke.
Ulezi pia umetajwa kuwa na virutubisho vingi vikiwemo kiwango kikubwa cha calcium, na hivyo kuwa muhimu kwa afya ya binadamu hasa watoto na wazee.

You Might Also Like

Elimu Ya Dawa Za Kulevya Kutolewa Kwa Wanafunzi

Mchengerwa Apongeza Shule Ya Sekondari Kibaha Kwa Ufaulu Wa Hali Ya Juu

Aloe Dorotheae, Mmea Unaopatikana Tanzania Pekee

Serikali Kuendelea Kuboresha Sheria za Ulinzi wa Watoto

JOWUTA Yataka Sheria Za Kazi Kuwalinda Wafanyakazi Katika Vyombo Vya Habari

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Tanzania Yaibuka Kidedea Maonesho Zambia
Next Article TARI Yaleta Mapinduzi Kilimo cha Minazi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Dkt. Ikomba wa CWT Aeleza Jinsi Elimu Ilivyobadilisha Taswira ya Tanzania kwa Miaka 64
Habari December 9, 2025
Profesa Ndunguru: Mtafiti Aliyejitoa Kusaidia Dunia Kupata Chakula Cha Baadae
Makala December 9, 2025
Profesa Ndunguru Abainisha Mwelekeo Mpya Wa Mageuzi Ya Kilimo Duniani
Habari December 9, 2025
TPDC na PURA Hakikisheni Watanzania Wananufaika na Rasilimali za Mafuta na Gesi- Salome
Habari December 8, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?