MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Tari Ilonga yaboresha mbegu, mavuno yapanda hadi tani 3.8 kwa hekta
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Tari Ilonga yaboresha mbegu, mavuno yapanda hadi tani 3.8 kwa hekta
Habari

Tari Ilonga yaboresha mbegu, mavuno yapanda hadi tani 3.8 kwa hekta

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
MOROGORO: TAASISI ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI), imefanikiwa kuboresha aina mpya za mbegu za mtama, uwele na ulezi zenye uwezo wa kustahimili mashambulizi ya ndege na kiduha (gugu chawi), ambayo ni changamoto kubwa kwa wakulima.
Mtafiti Msaidizi kutoka TARI Ilonga iliyopo Kilosa mkoani Morogoro, David Macha amesema hayo katika Maonesho ya nanenane Kanda ya Mashariki, ambayo kilele chake kilikuwa ni jana Agosti nane, 2025.
Amesema kwa upande wa mtama, wamezalisha aina tatu mpya: aina mbili nyeupe ambazo ni fupi, na aina moja nyekundu ndefu. Aina ya ‘Macia’ ni mojawapo ya mbegu nyeupe, yenye urefu wa mita 1.5, ambayo inafanya vizuri kibiashara hasa katika utengenezaji wa bia, ikichukua nafasi ya shayiri na ngano zilizokuwa zikitumika awali.
Amesema mbegu hiyo ya macia hukaa shambani kwa siku 110 na hutoa mavuno ya tani 3.8 kwa hekta moja, ikilinganishwa na mbegu za zamani zilizokuwa zikitoa tani 2.
Ina masuke makubwa na uwezo mkubwa wa kustahimili mashambulizi ya ndege kutokana na ubunifu wa kiteknolojia unaofanya isiwe ya kuvutia kwa ndege.
Ametaja mbegu nyingine mpya kuwa ni TARI SOR 1 na TARI SOR 2, ambazo zimeundwa kuzuia mashambulizi ya kiduha, adui mkubwa wa mazao ya nafaka.
Kwa upande wa uwele, amesema  wamezalisha aina iitwayo Okoa, ambayo ina kiwango kikubwa cha madini ya zinki, muhimu kwa kinga na uzazi wa binadamu.
Amesema madini hayo ya Zinki ni nadra kupatikana kwa wingi kwenye nafaka nyingine, na hivyo aina hii ni suluhisho bora kwa lishe bora.
Katika zao la ulezi, amesema TARI Ilonga wamezalisha aina tatu, ikiwemo aina mpya iliyo na uwezo wa kutoa hadi kilo 1,200 kwa ekari moja, tofauti na aina ya P224  inayotoa kilo 700 na 415  inayotoa kilo 800.
Aina hiyo mpya imeboreshwa pia kukabiliana na ugonjwa wa ‘blast’ unaoshambulia masuke.
Ulezi pia umetajwa kuwa na virutubisho vingi vikiwemo kiwango kikubwa cha calcium, na hivyo kuwa muhimu kwa afya ya binadamu hasa watoto na wazee.

You Might Also Like

Ridhiwani Awataka Wananchi Kuboresha Taarifa Zao Tayari Kwa Uchaguzi Mkuu

Hali Ya Ulinzi Na Usalama Wa Mipaka Ni Salama

Watanzania Washauriwa Kula Senene, Kumbikumbi, Msusa, Ngogwe Kuepuka Udumavu

Mikataba ya zaidi ya bilioni 50 kuhamasisha nishati salama

Mwenda: Tupo kwa ajili ya kuzitatua changamoto za wananchi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Tanzania Yaibuka Kidedea Maonesho Zambia
Next Article TARI Yaleta Mapinduzi Kilimo cha Minazi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?