MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Tanzania Yaongoza Kwa Ushiriki, Makongamano Ya Ushirika Ndani, Nje Ya Nchi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Tanzania Yaongoza Kwa Ushiriki, Makongamano Ya Ushirika Ndani, Nje Ya Nchi
Habari

Tanzania Yaongoza Kwa Ushiriki, Makongamano Ya Ushirika Ndani, Nje Ya Nchi

Author
By Author
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

DODOMA: MWENYEKITI  wa Jukwaa la Ushirika Mkoa wa Dodoma, Ibrahim Sumbe amesema Tanzania imekuwa mstari wa mbele katika kushiriki makongamano ya ushirika ndani na nje ya nchi, ikiwa ni matokeo ya mshikamano na juhudi kubwa kutoka kwa vyama vya ushirika nchini.
Sumbe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya KKKT Arusha Road SACCOS, amesema hayo katika Maonesho ya Wakulima yajulikanayo kama Nanenane katika Viwanja vya Nzuguni Dodoma.
Amesema jukwaa hilo lilianzishwa miaka minne iliyopita kwa lengo la kuunganisha vyama vya ushirika wa kifedha (SACCOS) na vyama vya ushirika wa mazao (AMCOS), ili kushirikiana katika kutatua changamoto zinazowakabili kwa pamoja.
“Mafanikio yamekuwa makubwa. Kila chama hujifunza kutoka kwa kingine, na tumekuwa tukifanya shughuli mbalimbali kwa pamoja, zikiwemo za kijamii kama kutoa misaada kwenye vituo vya kulelea watoto yatima, watoto wenye ulemavu na wazee,” amesema.
Amesema Katika kipindi cha hivi karibuni, jukwaa hilo limetoa misaada yenye thamani ya zaidi ya Sh. Milioni 14 kwa Hospitali ya Mlowa, ambazo zimenunulia  vitanda, mashuka na vifaa tiba mbalimbali.
Amesena kiwango cha mafanikio yao kimewafanya kutambuliwa kitaifa, ambapo jukwaa hilo lilishinda Tuzo ya Jukwaa Bora la Ushirika Kitaifa kwa mwaka huu.
Pia, wameshiriki katika maonyesho mbalimbali ya kitaifa na kimataifa, yakiwemo yale yaliyofanyika Uganda, Rwanda, na Kenya, wakionyesha bidhaa za kilimo na mazao mbalimbali.
“Inaonyesha jinsi Tanzania ilivyo mstari wa mbele karibu nusu ya wageni waliokuwepo kwenye makongamano haya walikuwa Watanzania. Tunaishukuru serikali kwa kutuunga mkono, ikiwemo hatua ya kuanzisha Benki ya Ushirika ambayo tayari imetengewa zaidi ya Sh. Bilionitano,” amesema.
Ametoa wito kwa Watanzania wote kujiunga na vyama vya ushirika akisisitiza kuwa, “Ushirika si chombo cha wanyonge kama ambavyo wengi wanavyodhani. Ni njia ya kuleta maendeleo ya pamoja, lakini mafanikio hayawezi kufikiwa bila umoja.”

You Might Also Like

Udongo wa kupandia mboga mboga unapatikana VETA

BRT Kuimarisha Uhusiano Tanzania, China

Samia Mgeni Rasmi Mkutano Mkuu ALAT

Dar es Salaam Kuunda Kamati Ya Kupitia Majengo Chakavu

VETA Mikumi Yatengeneza Mashine Ya Kuchakata Majani Ya Mifugo

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mazao Ya Mikunde Yatajwa Kuwa Na Kiwango Kikubwa Cha Protini
Next Article Profesa Nombo Atembelea Banda la UDSM, 88 Dodoma
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

VETA Yaleta Mapinduzi ya Kilimo na Biashara Kupitia Bunifu –  Profesa Nombo
Habari August 8, 2025
Profesa Nombo Atembelea Banda la UDSM, 88 Dodoma
Habari August 8, 2025
Mazao Ya Mikunde Yatajwa Kuwa Na Kiwango Kikubwa Cha Protini
Habari August 8, 2025
Mchome: Ubunifu wa VETA Ni Mkubwa, Sasa Ni Wakati Wa Uzalishaji Kwa Wingi
Habari August 8, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?