MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Tanzania Na Italy Wasaini Makubaliano Kuongeza Ubora Mafunzo Ya Ukarimu
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Tanzania Na Italy Wasaini Makubaliano Kuongeza Ubora Mafunzo Ya Ukarimu
Habari

Tanzania Na Italy Wasaini Makubaliano Kuongeza Ubora Mafunzo Ya Ukarimu

Author
By Author
Share
4 Min Read
Na Lucy Lyatuu

TANZANIA kupitia Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) na  Taasisi ya zinazoongoza katika mafunzo ya sekta ya ukarimu  nchini Italia ( ENAIP) zimesaini hati ya makubaliano ikiwa ni mkakati mahsusi wa kuongeza ubora wa mafunzo kwa  vitendo katika eneo la ukarimu na utalii nchini.

Makubaliano hayo yanatokana na maadhimisho ya wiki ya vyakula vya Kiitaliano duniani, ikiambatana na matukio  mbalimbali nchini Tanzania.

Hafla ya kusaini makubaliano hayo imefanyika jana Dar es salaam katika ukumbi wa ikishuhudiwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Pindi Chana.

Akizungumza katika  hafla hiyo, Balozi Chana amesema makubaliano hayo yamefikiwa baada ya maono yaliyofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan ya kutengeneza filamu ya Royal Tour kwa  lengo la kuongeza wigo wa watalii nchini.

Amesema serikali ina mkakati wa kuongeza watalii kufikia mil tano ifikapo mwaka 2025 na kuongeza pato la Taifa kufikia dola za marekani bilioni sita kwa mwaka 2025.

Amesema pia kupitia filamu hiyo imejikita kuboresha huduma za kitalii na ndio maana NCT imeingia makubaliano  na Taaisi ya ENAIP   kwa lengo la kuongeza ujuzi, ufahamu wa vyakula n ahata lugha mbalimbali.

Amesema makubaliano hayo nimuhimu kwa Taifa kwa kuwa kwa sasa Utalii unachangia asilimia 17 ya pato la Taifa huku ikiingiza fedha za kigeni kwa asilimia 25 huku shilingi ya Tanzania ikiendelea kuimarika.

Waziri  Pindi amesema makubaliano hayo ni muhimu kwa taifa ambapo yatawajengea uwezo walimu,wanafunzi na menejimenti ya NCT katika kupika vyakula mbalimbali, lugha,suala la ukarimu kwa wageni na utalii.

“Kipaumbele chetu ni kuongeza idadi ya watalii kutoka mataifa yote duniani ikiwemo soko la Italia hivyo makubaliano hay ani mojawapo ya mkakati wa kutoa huduma bora kwa watalii hatimaye kuongeza idadi  ya watalii nchini,”amesema.

Naye Mkuu wa NCT, Dk Florian Mtey amesema kuwa makubaliano hayo yatasaidia katika ukuzaji  na utekelezaji wa mitaala katika Nyanja za ukarimu na utalii, kubadilishana uzoefu kuhusu mbinu za kufundisha ukarimu na usimamizi wa vyuo vya utalii na ukarimu

“Juhudi hizi za ushirikiano zitaimarisha kwa kiasi kikubwa utoaji wa mafunzo katika sekta ya utalii na ukarimu na hivyo kuchangia ukuaji wa sekta  hiyo ambayo inabakia kuwa kipaumbele katika uchumi wan chi  yetu”,amesema.

Aidha amesema makubaliano hayo yatasaidia katika kubadilishana uzoefu wa ubunifu na kusasisha teknoloji za ufundishaji na maabara kuongeza ujuzi katika ukarimu na utalii sambamba na kubadilishana uzoefu na ujuzi wa mbinu bora katika mafunzo ya kiufundi ya utalii na ukarimu

Kwa upande wake Balozi wa Italia nchini Glussepe Sean Coppcla amesema kuwa kubadilishana uzoefu baina ya nchi hizo mbili ni muhimu katika kukuza sekta ya utalii ambayo ni sekta  muhimu kwa maendeleo ya Taifa

Hafla hiyo imehudhuriwa na Rais wa ENAIP Veneto Impresa Sociate, Antonino Ziglio, Maofisa kutoka ubalozi wa italia nchini Tanzanaia, viongozi  kutoka ENAIP na  wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara ya maliasili na utalii.

 

Maadhimisho ya  msimu wa tisa wa wiki y a vyakula kiitaliano duniani yameanza Novemba 16-23,2024  na kwa Tanzania watashirikiana na migahawa kadhaa ya Kiitaliano kutoka Tanzania Bara na Visiwani Pamoja na wakala wa Biashara wa Italia (ITA) kuhamasisha vyakula vyenye madhari ya kiitaliano katika migahawa  kutoka  Dar es Salaam, Iringa, Arusha na maeneo mbalimbali Zanzibar.

You Might Also Like

Wakulima Wa Mahindi Mvomero Walia Na Viwavijeshi Vamizi, Watafiti SUA kupitia Mradi Wa AGRISPARK Kuokoa Jahazi

Majaliwa ataka kuondolewe vikwazo vya rufaa za matibabu Afrika Mashariki

LHRC Kushirikiana  Na JOWUTA Kuwajengea Uwezo Wanahabari Katika Masuala Ya Haki Zao Na Sheria Za Kazi

Tani 27, 550  za ufuta zenye thamani ya bilioni 80 zimeuzwa

Chalamila Akabidhi milioni 100, saruji Kukamilisha Zahanati

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Sagini Amwelezea Kaluta Amir Abeid Ni Alama Ya Kuigwa
Next Article PSSSF Yaanza Kulipa Mafao Kwa Kikokotoo  Kipya Kilichoboreshwa – Ridhiwani
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?