MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Tanzania, Comoro Zaongeza Ushirikiano wa Lugha
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Tanzania, Comoro Zaongeza Ushirikiano wa Lugha
Habari

Tanzania, Comoro Zaongeza Ushirikiano wa Lugha

Author
By Author
Share
2 Min Read
– Kiswahili Kuanza Kufundishwa Shuleni
Na Mwandishi Wetu, 
COMORO: SERIKALI ya Tanzania na ile ya Muungano wa Visiwa vya Comoro zimekubaliana kuendeleza mashauriano yatakayowezesha kuanza kwa ufundishaji wa lugha ya Kiswahili katika shule za Comoro, ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Rais  Samia Suluhu Hassan.
Balozi wa Tanzania nchini Comoro, Saidi Yakubu ameeleza hayo akiwa pamoja na Waziri wa Elimu wa Comoro, Bacar Mvoulana, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kiswahili duniani yaliyofanyika katika mji wa Ntsaoueni, kisiwa cha Ngazidja.
Katika hotuba yake, Balozi Yakubu amesisitiza dhamira ya Rais Samia aliyoitoa mwaka jana wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya uhusiano kati ya Tanzania na Comoro, ambapo aliahidi kusaidia Comoro kwa kuipatia walimu pamoja na vifaa vya kufundishia Kiswahili.
Amesisitiza kuwa msaada huo utakuwa chachu ya kuimarisha matumizi ya Kiswahili visiwani humo, na kuongeza nafasi yake kama lugha ya mawasiliano ya kikanda.
Kwa upande wake, Waziri Mvoulana ameelezea shukrani za dhati kutoka kwa Serikali ya Comoro na kueleza kuwa tayari wizara yake imeanza maandalizi ya tathmini ya mahitaji muhimu kabla ya kuanza rasmi kwa mchakato wa ufundishaji wa lugha hiyo.
Maadhimisho hayo yalihudhuriwa pia na viongozi mbalimbali wakiwemo Gavana wa kisiwa hicho, mawaziri wa serikali ya Comoro, Balozi Mdogo wa Afrika Kusini, wawakilishi wa taasisi za kimataifa, mashirika ya kiraia, na wananchi kutoka miji 11 inayozungumza Kiswahili katika kisiwa cha Ngazidja.
Hatua hii ni mwendelezo wa juhudi za Tanzania kusambaza na kukuza lugha ya Kiswahili kimataifa, sambamba na kuimarisha diplomasia ya lugha kama chombo cha kuunganisha mataifa ya Afrika na kusukuma mbele maendeleo ya kijamii na kiutamaduni.

You Might Also Like

Maziwa Kukuza Uchumi Wa Wafugaji

Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, Laleta Furaha Kwa Watoto

Ushiriki Wa Tanzania Jukwaa La Dunia Waongeza Fursa Za Kimataifa Kukabiliana Na Maafa-Dk Yonaz

TSB yaanzisha ‘special’ Mkonge BBT

Mbunifu Alilia Uwepo Wa Miongozo Kwa Wagunduzi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TSB Yasisitiza Umuhimu Kuwekeza Kwenye Uchakataji Wa Mkonge
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

TSB Yasisitiza Umuhimu Kuwekeza Kwenye Uchakataji Wa Mkonge
Habari July 10, 2025
eGA Yatengeneza  Mifumo  Kurahisisha  Kazi
Habari July 10, 2025
July 10, 2025
Habari July 10, 2025
Wanafunzi, Watafiti, Wanataaluma Kujadili Dini, Utamaduni na Maisha ya Kisasa
Habari July 10, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?