MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Tanzania, Belarus Zaanza Ukurasa Mpya wa Ushirikiano wa Kimkakati
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Tanzania, Belarus Zaanza Ukurasa Mpya wa Ushirikiano wa Kimkakati
Habari

Tanzania, Belarus Zaanza Ukurasa Mpya wa Ushirikiano wa Kimkakati

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Mwandishi Wetu
MINSK: ZIARA ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa nchini Belarus imefungua ukurasa mpya wa ushirikiano baina ya mataifa hayo mawili, baada ya kusainiwa kwa Hati Nne za Makubaliano katika sekta za mashauriano ya kisiasa, kilimo, elimu na biashara.
Makubaliano hayo yamesainiwa katika mji mkuu wa Belarus, Minsk, yalifikiwa baada ya mazungumzo rasmi baina ya Waziri Mkuu Majaliwa na mwenyeji wake Alexander Turchin, Waziri Mkuu wa Belarus.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mazungumzo hayo, Majaliwa amesema makubaliano hayo ni ishara ya utashi wa kisiasa uliopo baina ya Tanzania na Belarus katika kujenga ushirikiano wa kimkakati kwa manufaa ya wananchi wa pande zote mbili.
“Hii ni ziara ya kwanza ya ngazi ya juu tangu tuanzishe uhusiano wa kidiplomasia mwaka 1996. Kusainiwa kwa hati hizi ni mwanzo wa ukurasa mpya wa ushirikiano unaolenga kuendeleza rasilimali zilizopo na kuleta maendeleo ya pamoja,” amesema.
Amesema kuwa kutokana na hatua kubwa za maendeleo zilizofikiwa na Belarus katika nyanja mbalimbali kama kilimo, elimu, Tehama, afya, nishati, viwanda na utalii, Tanzania imefungua milango kwa wawekezaji kutoka Belarus kuwekeza nchini.
Majaliwa ametaja maboresho ya sera na sheria za uwekezaji, miundombinu ya kisasa pamoja na motisha za kikodi kama sababu kuu zinazowavutia wawekezaji wa kimataifa.
“Tanzania ni lango la kibiashara Afrika. Tuna fursa ya soko la watu zaidi ya bilioni 1.6 kupitia Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), na Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA),” amesema.
Katika ziara hiyo, ujumbe wa Waziri Mkuu pia ulitembelea kiwanda cha kutengeneza dawa na vifaa tiba pamoja na kiwanda cha kutengeneza matrekta, ambapo walijionea teknolojia ya kisasa inayotumika katika uzalishaji.
Viongozi wa viwanda hivyo walieleza nia yao ya kushirikiana na Tanzania na wameahidi kufanya ziara ya kibiashara nchini hivi karibuni ili kuchunguza fursa zilizopo.
Ujumbe wa Waziri Mkuu uliambatana na viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Zanzibar, Kazi, Uchumi na Uwekezaji,  Shariff Ali Shariff, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,  Cosato Chumi, pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Urusi, Fredrick Kibuta.

You Might Also Like

China Yafundisha Wanafunzi DIT kuzifikia fursa

Kongamano La Kwanza La Kodi Kufanyika Dar es Salaam

Miaka Minne Ya Samia Na Sekta Ya Elimu

Kampeni ya Mama Samia imewafikia zaidi ya watu 4000 mikoa saba

LHRC Kushirikiana  Na JOWUTA Kuwajengea Uwezo Wanahabari Katika Masuala Ya Haki Zao Na Sheria Za Kazi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Rais Samia Atoa Bil. Nne Ujenzi Kiwanda Cha Kuzalisha  Nishati Mbadala  
Next Article TSLB Yatakiwa Kuimarisha Huduma za Kidijitali Ili Kukidhi Mahitaji ya Karne ya 21
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Maliasili Yapongezwa Kwa Kutekeleza Maono Ya Rais Samia  
Habari July 23, 2025
Tanzania, Uturuki Zaweka Dira Mpya ya Biashara ya Dola Bil. Moja
Habari July 23, 2025
TUICO Arusha Yapongezwa Na AUWSA
Habari July 23, 2025
TSLB Yatakiwa Kuimarisha Huduma za Kidijitali Ili Kukidhi Mahitaji ya Karne ya 21
Habari July 23, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?