MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Tani 27, 550  za ufuta zenye thamani ya bilioni 80 zimeuzwa
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Tani 27, 550  za ufuta zenye thamani ya bilioni 80 zimeuzwa
Habari

Tani 27, 550  za ufuta zenye thamani ya bilioni 80 zimeuzwa

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu, Mtwara
TANI 27,550 za ufuta zenye thamani ya sh bilioni 80 zimeuzwa na wakulima wa Mtwara, kupitia minada inayofanyika kwa kutumia mfumo wa Soko la Bidhaa Nchini (TMX).
Ofisa usimamizi wa Fedha kutoka TMX Prince Philimon amesema hayo  wakati akizungumza na Mwandishi wa habari hii, kuhusu maendeleo ya minada ya ufuta ambayo inafanyika Mkoani hapa.
Philimon amesema tangu kuanza msimu  wa  uuzaji wa ufuta 2024/2025, minada sita imefanyika ambapo wakulima waliuza ufuta kwa bei ya juu ya shilingi 3,570  kwa kilo na bei ya chini ya shilingi 3,350.
Minada hiyo ambayo inaendeshwa na Chama Kikuu cha Ushirika cha Masasi, Mtwara na Nanyumbu (TMX) ilizinduliwa June nne mwaka huu ambapo kwa mara ya kwanza walianza kutumia mfumo wa TMX.
Wakizungumza katika mnada wa sita ambao ulifanyika Wilaya ya Nanyumbu Mkoani Mtwara, wakulima wa ufuta walieleza kufurahishwa na uuzaji wa ufuta kupitia mfumo huo wakisema unahamasisha upatikanaji wa bei nzuri Kwa kuleta wanunuzi wengi kwa wakati mmoja.
“Kwa kweli tunatamani mfumo huu utumike pia kwenye uuzaji wa mazao kama Korosho, mbaazi pia kwa sababu una manufaa sana hasa kwenye suala la bei, kama ulivyosikia bei inapanda kadri tunavyoendelea na minada, ” amesema Mkulima wa ufuta Nanyumbu Ally Omary.
Serikali ilitangaza utaratibu wa kununua zao la ufuta kupitia mfumo wa huo msimu 2024/2025 ili kuleta bei zenye ushindani, haki, uwazi, na kupunguza gharama za ununuzi wa zao hilo la ufuta Nchini.
Akizungumzia mienendo ya bei , Ofisa Usimamizi wa Fedha TMX Philimon amesema bei inapanda kadri minada unavyozidi kuendelea ambapo kwa sasa imefikia shilingi 3570 bei ya juu kwa kilo na 3350 ya chini.
Alisema mwanzo wa kutumia mfumo wa TMX wakulima walionyesha kutofurahishwa na mfumo lakin kadri minada ilivyozidi kufanyika kupitia mfumo huo na kuona manufaa yake wamekubali na kuomba utumike hata kwenye mazao mengine kama Korosho.

You Might Also Like

VETA Yatafiti Dawa Ya UTI, Fangasi

Wananchi Washauriwa Kujiunga Na Chuo Cha Ualimu Na Ufundi Stadi Morogoro

Vyama Vya Wafanyakazi Kujadili Hatma Ya Wafanyakazi TAZARA

Tanzania Ina Utolevu Wa Chakula Kwa Miaka Minne Uongozi Wa Samia

TTCL Yaweka Punguzo Kubwa Kwa Vifaa Vya Mobile Kwenye Sabasaba

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Fanyeni kazi kwa bidii kulinda taswira ya TARURA
Next Article Wadau wa uchukuzi zingatieni maslahi ya wafanyakazi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Waziri Mkuu Majaliwa Akabidhi Tuzo kwa BoT Geita
Habari September 22, 2025
BoT Yarahisisha Uuzaji wa Dhahabu kwa Wachimbaji, Yatoa Punguzo La Mrabaha
Habari September 22, 2025
Waziri Mkuu Apongeza Huduma Kidijitali za NSSF, Maonesho Ya Madini Geita
Habari September 22, 2025
Mkuu Wa Mkoa Shinyanga Asifu Kazi Ya Bodi Bima Ya Amana
Habari September 22, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?