MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Tafiti Katika Afya Nyenzo Muhimu
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Tafiti Katika Afya Nyenzo Muhimu
Habari

Tafiti Katika Afya Nyenzo Muhimu

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read

Na Danson Kaijage

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe amesema tafiti katika sekta ya afya ni nyenzo muhimu kuhakikisha huduma bora zenye tija kwa wananchi.

Dkt. Shekalaghe ametoa kauli hiyo jijini Dodoma, Aprili nne, 2025 wakati wa Ufunguzi wa Mdahalo wa Kitaaluma katika Maadhimisho ya Wiki ya Afya Kitaifa.

Amesema tafiti mbalimbali katika maeneo ya magonjwa yakiwemo malaria, kifua kikuu na yale ya kuambukiza, zimekuwa chachu ya mabadiliko chanya kwenye sera na mbinu za utoaji huduma.

Amesena serikali imeendelea kushirikiana na taasisi za utafiti, wadau wa maendeleo na sekta binafsi ili kuhakikisha tafiti zinazofanyika nchini zinagusa mahitaji halisi ya wananchi na kuchangia utekelezaji wa mipango ya maendeleo.

“Tafiti zimetuwezesha kuwa na ushahidi wa kisayansi unaoongoza matumizi ya dawa mpya, mbinu bora za kinga na pia kubaini maeneo yenye changamoto kubwa zaidi kiafya,” amesema.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt. Grace Magembe amesema mdahalo huo wa kitaaluma utasaidia katika kusukuma mbele maendeleo ya sekta ya afya nchini.

Naye, Mkurugenzi wa Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe kutoka Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Dkt. Rashid Mfaume amesema hakuna halmashauri nchini isiyokuwa na hospitali, jambo linalothibitisha mafanikio ya uwekezaji mkubwa wa Serikali katika sekta ya afya.

Maadhimisho ya Wiki ya Afya kitaifa yenye Kauli mbiu isemayo, ‘Tulipotoka, Tulipo, Tunapoelekea; Tunajenga Taifa Imara Lenye Afya’ yanafayika kuanzia Machi tatu hadi nane, Aprili 2025
katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete, jijini Dodoma,

Yanahusisha utoaji wa huduma za afya bure, maonesho ya taasisi, vipimo, chanjo pamoja na mijadala ya kitaalam.

You Might Also Like

Njaa, Mafao Ya Wakulima Vyatikisa Kampeni Za Ubunge Dodoma Mjini

MAIPAC Yagawa Makoti Ya Usalama Kwa Wanahabari Kuelekea Uchaguzi Mkuu.

UDSM,YULHO kujenga kituo cha kupima madini

Wanufaika wa SDF Waeleza Mafaniko Waliyoyapata

Ofisi Zote Dodoma Kutoa Ushirikiano Kwa Watangazaji-RC

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Maofisa Habari Watoe Taarifa Sahihi Ziwafikie Wananchi
Next Article Rais Samia Azindua Makao Makuu Ya Mahakama Tanzania
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Nchimbi Ahimiza Ushirikiano wa Wizara Katika Uhifadhi wa Mazingira
Habari March 10, 2026
Mtaka, Ndunguru Wakubaliana Ujenzi wa Maabara ya Kimkakati Njombe
Habari March 10, 2026
Wataalamu wa Fedha SADC Wakutana Pretoria Kujadili Bajeti
Habari March 9, 2026
TASFAM Yawawezesha Wanawake wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Kuadhimisha Siku ya Mwanamke
Habari March 9, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?