MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Taasisi Ya Confucius Imezindua Kitabu Cha Kujifunza
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Taasisi Ya Confucius Imezindua Kitabu Cha Kujifunza
Habari

Taasisi Ya Confucius Imezindua Kitabu Cha Kujifunza

Author
By Author
Share
4 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: NAIBU Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, upande wa taaluma Profesa Bonaventure Rutinwa ametoa wito kwa Taasisi ya Kichina ya Confucius kuhakikisha kwamba vitabu vinavyozinduliwa na vitakavyoandikwa baadaye vinakuwa na rasimu ya Kiswahili.

Profesa Rutinwa ametoa wito huo wakati wa uzinduzi wa Kitabu cha kujifunza lugha ya kichina kilichotafsiriwa kwa lugha ya kiswahili chuoni hapo ili kuwawezesha wanafunzi wa kitanzania wanaojifunza lugha hiyo kuelewa kwa haraka.

Amesema, “Nimeelezwa kwamba Mheshimiwa Palamagamba Kabudi, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo amewahi kutoa ushauri kwa Taasisi ya Confucius kutafsiri hotuba za Mheshimiwa Xi Jinping kwa Kiswahili.

“Ninakuhimizeni kuupa uzito ushauri huo na kuzingatia kuwa ushauri wa Mheshimiwa Waziri ni maelekezo,”.

Amesema imani yake ni kwamba, wachapishaji kampuni ya Changjiang Publishing & Media Co. Ltd kutoka China, watakuwa tayari kuchapisha vitabu hivyo kama mchango wao katika kuimarisha uhusiano baina ya China na Tanzania.

Amesema kitendo hicho ni chachu ya kukuza ujuzi wa lugha ya Kichina miongoni mwa wanafunzi wa Tanzania.

“Uandishi wa kitabu hiki ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu ya chuo yanayohusu utafiti na uchapishaji. Hongereni sana Taasisi ya Confucius kwa kazi hii ya kutiliwa mfano,” amesema.

Amesema kitabu hicho kipya kilichoandikwa na wakurugenzi na walimu wa Taasisi ya Confucius kimepokelewa kwa matumaini makubwa kuwa kitaongeza uelewa wa Watanzania kuhusu sera za China na kuchochea tafakuri pana kuhusu ushirikiano wa nchi hizo mbili.

Mkurugenzi wa Taasisi hiyo upande wa China hapa Tanzania, Profesa Zhang Xiaozhen,, amesema Rais wa China, Xi Jinping , amekuwa akisisitiza umuhimu wa kujengwa ushirikiano wa kiutamaduni na hatimaye kuifanya jamii kuishi kwa ushirikino na kuifanya dunia kuwa sehemu salama na rafiki.

“Hivyo kupitia kitabu hiki ni mwendelezo wa kutimiza maono hayo ya Rais wetu ambapo wajifunzaji wa lugha ya kichina sio tu kitawafanya kujifunza lugha ya kichina bali kupata taarifa mbalimbali ikiwa ni pamoja na shughuli za kiutamaduni kuhusu nchi ya China.

Amesema kitabu hicho kinaitwa “Mtazamo wa jumla kuhusu China’ kitawanufaisha wanafunzi watakaojifunza lugha ya kichina wakiwemo wanaosomea stahahada na shahada ya lugha ya kichina na wale wanaosomea ngazi ya cheti na kozi fupi katika lugha hiyo.

Profesa Zhang amesema katika uandishi wa kitabu hicho, mambo yaliyozingatiwa ni pamoja na ukweli ili kuhakikisha mwanafunzi anakuwa na uelewa mzuri katika ujifunzaji wake na kuepuka kukutana na changamoto zisizo za lazima.

“Taarifa zilizopo ndani ya kitabu hicho zimetoka katika vyanzo vya kuaminika na pia vimewekwa mazoezi mbalimbali vitavyowasaidia wasomaji wake,”amesema Mkurugenzi huyo.

Naye Mkurugenzi wa Taasisi ya Kichina upande wa Tanzania, Dkt. Hans Mussa, amesema kitabu hicho kitawanufaisha wanafunzi watakaojifunza lugha ya kichina wakiwemo wanaosomea stahahada na shahada ya lugha ya kichina, wanaosomea ngazi ya cheti na kozi fupi.

Dkt. Musa amesema kitabu hicho kina sura 12 na mada 19 zinazolenga maeneo mbalimbali ikiwemo kuhusu China , lugha na maandishi ya kichina, Miji mikuu ya Kale ya China, miji maarufu nchini China.

You Might Also Like

Bodi Ya Wadhamini Ya NSSF Yaridhishwa Na Uwekezaji Wa Ubia Na Jeshi La Magereza

WCF yapongezwa kwa Ithibati ya ISO, utoaji wa huduma kwa viwango vya kimataifa

Rais Samia ashuhudia JOWUTA Ikiwa mwanachama wa  TUCTA 

Bodi ya mkonge kutoa ajira kwa watu 10,000 ifukapo 2030

Chanzo Cha Bunge Kuridhia Hoja Ya Wanaojifungua Njiti, Kilianzia Hapa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article PSPTB Yatangaza Usajili wa Mitihani ya 31 ya Kitaaluma ya Ununuzi na Ugavi
Next Article Wanafunzi UDOM Wavumbua Mafuta ya Asili Kutoka Mabaki ya Zabibu
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Watanzania Watakiwa Kuachana Na Dhana Potofu Kuwa Nishati Safi Ya Kupikia Ni Gharama
Habari July 5, 2025
Wananchi Waelimishwe Kuhusu Utendaji wa Kamati za Maadili za Maofisa wa Mahakama
Habari July 5, 2025
UDOM Yatafiti Dawa za Malaria, Vidonda vya Tumbo, Kisukari Kutoka Mimea ya Asili
Habari July 5, 2025
Wanafunzi UDOM Wavumbua Mafuta ya Asili Kutoka Mabaki ya Zabibu
Habari July 5, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?