MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Serikali kuleta kicheko kwa TASU 
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Serikali kuleta kicheko kwa TASU 
Habari

Serikali kuleta kicheko kwa TASU 

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Lucy Ngowi

SERIKALI imetoa zabuni kwa kampuni ya kizalendo kwa ajili ya kufanya utafiti katika Bahari ya Hindi ili kujua ni aina gani ya meli ya mizigo inapaswa kuwepo kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya nchi.
Utafiti huo utahusu ukubwa wa meli inayopaswa kuwepo kutokana na soko lilivyo, ambayo itakuwa na uwezo wa kufanya kazi kwenye mwambao, Bahari ya Hindi ama nje ya nchi.
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Huduma za Meli nchini, Eric Hamissi amesema hayo alipozungumza na Mwandishi Gazeti la Mfanyakazi.
Amesema meli hiyo itafanya kazi ya kubeba mizigo lakini pia wanafunzi wanaosoma Chuo cha Bahari watafanya mazoezi ya vitendo kupitia meli hiyo.
Wakati Mkurugenzi huyo akielezea hayo katika siku za karibuni Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha Mabaharia Tanzania (TASU), Hamis Urembo aliiomba serikali inunue meli au kutengeneza kwa ajili ya kupeleka mizigo nje ya nchi na kuileta Tanzania ili vijana wanaomaliza chuo wapate ajira.
Urembo alitoa ombi hilo kwa kuwa hivi sasa ajira za mabaharia zimekuwa chache, ilhali chuo cha baharia kikiwa kinazalisha wanafunzi wengi kila mwaka ambao wanazagaa mitaani kwa kuwa hakuna meli ya kuwasaidia.
Kwa maelezo ya Urembo, zamani kulikuwa na kampuni ya ushirikiano ya meli ya China na Tanzania, kulikuwa na meli nyingi, hivyo kupitia chama cha mabaharia kila baada ya miezi sita, mabaharia wa Tanzania walienda China, walifanya kazi kwa kupokezana na wengine kwa mkataba wa miezi sita.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Huduma za meli nchini Hamissi amesema, utafiti huo utakapokamilika, mwaka ujao wa fedha 2025/ 2026 watakuwa wamejua aina gani ya meli wanaanza kuijenga au kuinunua.
Kwa upande mwingine Hamissi amesema serikali inajenga kiwanda kikubwa cha kujenga meli Ziwa Tanganyika mkoani Kigoma.
Amesema meli ya uzito wa tani 5000 ndio itakayojengwa katika kiwanda hicho.
“Mpaka sasa tumeshasaini mikataba na wakandarasi hivyo muda wowote ujenzi wa kiwanda hicho utaanza,” amesema.
Kiwanda hicho kinagharimu sh bilioni 322.
Akiwa katika Jukwaa lililoandaliwa na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Naibu Waziri wa Uchukuzi David Kihenzile alisema katika kuboresha sekta ya uchukuzi serikali ina mpango wa kujenga meli mpya mbili za kisasa, jambo litakaloleta mageuzi makubwa nchini.
Pia alisema serikali inajenga kiwanda kipya cha kutengeneza na kukarabati meli ambacho hakijawahi kujengwa katika bara la Afrika.

You Might Also Like

DKT. Biteko Ashiriki Kongamano la Nishati Safi ya Kupikia Zanzibar

CCCC Yaandaa Tamasha La Dragon Boat

Madini Yaweka Rekodi Makusanyo Ya Maduhuli

Atoa Maelekezo Kwa Chuo Cha Hombolo Kuwajengea Uwezo Viongozi Wa Mitaa Na Vijiji -Kapinga

Shemdoe aridhika huduma zinazotolewa na TVLA nanenane

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wajadili uendelezaji mazao ya utalii
Next Article Kagera, Geita kuanza uboreshaji daftari la kudumu la wapiga kura
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Tume ya Kurekebisha Sheria Yaelimisha Umma Kuhusu Haki za Wanyama
Habari August 6, 2025
Bundi Wasaidia Kupambana na Panya: Teknolojia Asilia Inayobadili Maisha ya Wakulima
Habari August 6, 2025
Ofisa wa TARI Kuwapo Kila Kituo cha Umwagiliaji – Naibu Katibu Mkuu
Habari August 6, 2025
Mbinu Mpya za Kilimo kwa Vijana Zapata Umaarufu Nanenane Banda La VETA
Habari August 6, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?