Na Danson Kaijage.
DODOMA: RAIS Samia Suluhu Hassan kesho tarehe 14, Juni 2025 atakagua maendeleo ya ujenzi wa Barabara ya Mzunguko wa nje wa Dodoma Km 112 na Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato.
Katika ziara hiyo, Rais Samia ataambatana na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Akinwumi Adesina.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amesema ziara hiyo itakayoanzia eneo la Mtumba-Veyula – Msalato itahitimishiwa kwa Rais Samia kuzungumza na wananchi katika eneo la Nala na hivyo kuwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kushuhudia utekelezaji wa miradi mikubwa na ya kimkakati inayoendelea mkoani Dodoma.