Na Lucy Ngowi
DODOMA: WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu. Ridhiwani Kikwete amefanya mazungumzo na ujumbe wa Ubalozi wa Jamhuri ya Watu wa China.
Ujumbe huo umeongozwa na Balozi wa China Nchini, Chen Mingjian Ofisini kwake Dodoma.

Ridhiwani amesema katika kikao hicho balozi Mingjian alijitambulisha na kutaka kuendelea kuimarisha mahusiano baina ya nchi ya China na Tanzania.
Amesema amekumbusha maeneo muhimu ya ushirikiano haswa katika mafunzo ya kujenga ujuzi na ufundi huku msisitizo mkubwa ukiwa kuwaandaa vijana watakaopambana na mabadiliko makubwa ya kidunia hasa katika mapinduzi ya teknolojia.
Kwa upande wake Ridhiwani amewaambia Tanzania itaendelea kuenzi uhusiano uliopo.

“Pia tutaendeleza uhusiano huu kwa kuimarisha maeneo yote ambayo yanatukutanisha katika mashirikiano haya.
“Pia tumewashukuru serikali ya China kwa mabadiliko makubwa ambayo yanaelekea kukuza ujuzi kwa vijana wa Kitanzania na nia yao ya kufanya maonyesho makubwa ya Kazi yanayolenga kufunua fursa za vijana wa kitanzania kujiajiri na kufungua milango ya kuajiriwa na makampuni makubwa ya kigeni yakiwemo ya China nchini hapa,” amesema Ridhiwani.