MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Nzega Kujenga Barabara za Lami, Soko la Kisasa ili Kukuza Uchumi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Nzega Kujenga Barabara za Lami, Soko la Kisasa ili Kukuza Uchumi
Habari

Nzega Kujenga Barabara za Lami, Soko la Kisasa ili Kukuza Uchumi

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
TABORA: HALMASHAURI ya Mji wa Nzega inatarajia kuanza utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa kilomita 10.6 za barabara za lami katika maeneo ya pembezoni na nje ya mji.
Kaimu Mkurugenzi wa Mji wa Nzega, Ajalii Malimwengu, amesema  miradi hiyo ni sehemu ya juhudi za Mbunge wa Jimbo la Nzega Mjini, Hussein Bashe, za kuvutia ufadhili kutoka kwenye mradi wa Kuboresha Miundombinu Mijini (TACTC) unaofadhiliwa na Benki ya Dunia.
Amesema mradi huo unalenga kuboresha usafiri wa watu na bidhaa, kuimarisha usalama, na kuinua hadhi ya mji huo.
Pia amesema Nzega itapata Soko Kuu la kisasa litakalojengwa kwa ajili ya wafanyabiashara, hatua inayotarajiwa kuchochea ukuaji wa biashara na kuongeza kipato cha wafanyabiashara, hivyo kuchangia uchumi wa mji huo.
“Leo tunapitia matokeo ya tathmini kutoka kwa mshauri mwelekezi kabla ya hatua nyingine muhimu kufuata ,” amesema.
 Ametaja barabara zitakazojengwa kuwa ni Barabara ya Ferouz, Swahili–Kachoma, Kalangale Moja na Mbili, pamoja na Barabara ya Dkt. Massam–Chief Ntinginya.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya GaugePro Consult Limited, ameeleza baada ya kufanya ziara ya eneo la mradi, changamoto mbalimbali zimebainika.
Ametaja changamoto hizo ni pamoja na uwepo wa mabomba ya maji, nguzo za umeme, na miti katika maeneo yanayotarajiwa kujengwa.
Amesema ushauri utatolewa kuhusu namna ya kushughulikia changamoto hizo na athari zake za kifedha.
Mshauri kutoka Benki ya Dunia, Dkt. Alphonce Tiba, amesisitiza umuhimu wa kushughulikia masuala ya mazingira na tamaduni ili kuhakikisha mradi unakidhi mahitaji ya jamii.
“Hakikisheni mnashirikisha wadau wote muhimu na kujumuisha maoni yao katika upangaji wa miradi.
Kwa mfano, ujenzi wa soko kuu utawaathiri wafanyabiashara 350 wa sekta sita tofauti, hivyo ni muhimu kufahamu matarajio yao,” Dkt. Tiba amesema.
Kwa upande wake, Kondwanie Chirembo, Mtaalamu Mwandamizi wa Usimamizi wa Hatari za Majanga kutoka Benki ya Dunia, amesisitiza umuhimu wa kufanya uchunguzi wa kina wa udongo ili kuhakikisha uimara wa miradi na kuepuka nyufa katika miundombinu.
Amesema ripoti ya mradi inapaswa kuwa na taarifa wazi juu ya jinsi barabara zitakavyounganishwa na namna zitakavyojengwa ili kufanikisha malengo yaliyokusudiwa.

You Might Also Like

Watahiniwa 72 wa kidato cha nne wafutiwa mtihani kwa udanganyifu, kuandika lugha za matusi

Mipango Zaidi Msiba Wa Cleopa Msuya Kutolewa Na Serikali

Tanzania, Ufini Kushirikiana Teknolojia Za Kisasa Sekta ya Misitu

Mkakati Wa Utekelezaji Wa Sera Ya Malikale Lango La Fursa Za Utalii

Mongela Ajiridhisha Ushindi wa Kishindo , Uchaguzi Serikali za Mitaa,Uchaguzi Mkuu CCM

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article COSOTA Yapokea Migogoro 136 Ndani Ya Miaka Minne
Next Article Tanzania, Japan Kushirikiana Ukuzaji Ujuzi Kwa Vijana
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?